JATU PLC wataharibu imani ya Watanzania kununua hisa kwa kampuni ndogo za Watanzania

Kimleyo

New Member
Nov 5, 2021
1
5
Jatu PLC imeanza kunuka wizi mapema kabla hakuja kucha tayari wakulima wadogo wanadai hela zao za mazao hawajalipwa kwa muda mrefu huku wakulima wakubwa pia wakidai hela zao.

Bidhaa zimeshuka Bei haswa maharage Wana nunua kwa Bei chini ya kiwango walichosema mbali na kwamba walisema mazao yana bima ila ndio hvyo tena. Ukiwaomba mazao yako ukauze mwenyewe wanasema sera ya uwekezaji haipo hvyo

Wame anzisha mradi Mpya wa Mifugo huku wakulima hawajalipwa hela zao ni dhahiri kwamba hii ni JANJA JANJA inafanyika wameitisha mkutano wa kujadili kinacho endelea lakini naambiwa hua wanafanya hvyo kutuliza upepo.

Nimeenda kuuza hisa zangu kwa faida kabla mambo hayajawa Wana lakini nimekosa imani na kampuni za watanzania kwenye kununua hisa

Nawasiwasi hata zikija kampuni nyingine ambazo hazitokua na utapeli watashindwa kabisaa kupata wanunuzi wa hisa.
 
Karibu vanilla village au Kagera Parachichi au Vitendo Saccoss.. hutojutiA
Vanilla Village

IMG_20210726_210922.jpg
 
Nasubiri comment yenye maelezo chanya juu ya hili maana bado sijaamini.

Wakati tunapambana na Mr Kuku hawa jamaa walikuwepo na hawakuguswa ikiashiria kuwa wako kwenye mstari sahihi...sasa taarifa kama hii inatia shaka kama Watendaji wetu wa serikali kama wana uwezo wa kuona viashiria visivyo sawa.
 
Nasubiri comment yenye maelezo chanya juu ya hili maana bado sijaamini.

Wakati tunapambana na Mr Kuku hawa jamaa walikuwepo na hawakuguswa ikiashiria kuwa wako kwenye mstari sahihi...sasa taarifa kama hii inatia shaka kama Watendaji wetu wa serikali kama wana uwezo wa kuona viashiria visivyo sawa.
Mbona Mr kuku bado anatembea kwenye mstari ule ule
 
Back
Top Bottom