wakusoma
JF-Expert Member
- Feb 25, 2008
- 1,085
- 1,049
Sehemu ya tatu
abu cha ukachero wa kachero wa Tanzania – 3
Habari Zinazoendana
Share
…………….
KATIKA wiki mbili zilizopita tumechapisha sehemu mbili za uchambuzi wa wa kitabu kipya kinachoitwa MATEKA MPAKANI kilichoandikwa na kachero wa Tanzania, Frown Kageuka (pichani) kumuenzi mwenzake aliyeuawa mpakani mwa Tanzania na Uganda na majasusi wa aliyekuwa Rais wa Uganda, Idi Amin. Leo tunaendelea na sehemu ya tatu ya mfululizo wa uchambuzi wa kitabu hicho.
……………
TULIFIKA Makindye usiku, eneo hilo lilifanana sana na Manzese ya Dar es Salaam. Kwa hakika safari yetu ilikuwa ndefu sana kwa hiyo nilihisi tumeingia ndani sana ya nchi ya Uganda na labda tulikuwa karibu na Kampala.
Tuliteremshwa ‘kikuku’ na kuingizwa katika nyumba moja ambayo nilihisi ni mahabusu. Tuliachwa humo tukiwa bado na kamba miguuni na mikononi hadi alfajiri. Usiku wote hatukuweza kuongea lakini asubuhi nilijua tupo wote pamoja baada ya Koplo Sudi kumwambia Sajini Binda kwamba ana njaa sana. Kwa kweli hata mimi nilikuwa na njaa sana lakini hatukuwa na la kufanya. Jua lilipoanza kuonesha makali yake tulifunguliwa kamba tulizofungwa na askari mmoja mwenye cheo cha Sajin.
“Mnataka chai au uji? Aliuliza Sajini huyo ambaye alionyesha ni katili sana. “Chochote unachoona tunastahili,” nilijib kwa upole. “Mimi nawapa uchaguzi nyinyi wafungwa,” alijibu Sajin huyo na kuondoka.
Dakika kama tano hivi baadaye mlango ulifunguliwa na Sajini yule yule aliyekuwapo awali, akaingia ndani akifuatiwa na askari mmoja asiye na cheo ambaye amebeba birika na vikombe vitatu vya bati.
“Haya punguzeni njaa kwa mlo huu nyie wafungwa” alitamka Sajin huyo kwa kebehi huku mwenzake akiweka birika na vikombe karibu yetu na kuondoka.
“Kwani sisi ni wafungwa?” niliuliza kwa upole huku nikimkazia macho. “Eh! Kumbe nyinyi ni kina nani?” alijibu Sajenti huyo huku akinitolea macho. “Sisi sio wafungwa bwana. Tunashangaa jinsi mlivyotukamata na kutuleta hapa.” “Hayo mimi sijui, ninachokijua nyingi ni askati mateka kutoka Tanzania kwa hiyo ni wafungwa.”
“Sisi sio askari bwana, kama mmeambiwa hivyo mmedanganywa kabisa. Mmeshindwa kuwapata askari halisi mkatukamata sisi raia na kutuita askari. Huo ni uonevu mkubwa,” nilimwambia kwa upole.
“Nyinyi watu wa Tanzania Kiswahili kirefu sana, kama siyo askari mmmefikaje hapa Makindye?” aliuliza kwa mshangao huku akituthitibishia hapo tulipo ni Makindye.
“Lakini kama sisi ni wanajeshi kama mnavyotaka tuwe, basi inabidi mtupe huduma sawa na mkataba wa Geneva unaohusu wafungwa wa kivita.” “Wewe mbona unaongea sana? Au ndiyo mkubwa?” aliniuliza kwa ukali na kuondoka zake.
“Inaonyesha hawa wanampango mbaya na sisi, hapa walipotuleta ni ndani kabisa ya nchi yao, ni maili chache tu kufika mjini Kampala. Sijui kama tutarudi salama. Iddi Amin hajawahi kuachia mtu salama na hasa waliokamatwa kimya kimya kama sisi. Ni lazima tufanye kitu ili tujiokoe” niliwaeleza wenzangu kwa sauti ya chini lakini kabla hawajanijibu mlango ulifunguliwa. Askari mmoja aliyevalia rasmi kipolisi jeshi (Military Police) alituamuru tutoke nje haraka. Hapo nje tuliwakuta askari wengine sita waliokuwa na bunduki aina ya AK 47 kila mmoja.
Tulifungwa pingu mikononi na kuongozwa hadi kwenye uwanja ambao bila ya kuamiwa nilijua ni sehemu ya kuulia watu kwa kupigwa risasi. Tulifungwa katika miti iliyokuwa mbele ya magunia mengi ya mchanga ambayo nilijua ni maalumu kwa kuzuia risasi isiende mbali ya hapo.
Baada ya kufungwa kamba kuzunguka mti nilijiona nimeshakuwa mfu. Koplo Sudi na Sajini Binda walianza kulia kama watoto wadogo. Niliogopa sana hali hiyo, kwa vile nilijua Waganda hao watagundua mimi ni kiongozi wao kutokana na ujasiri wa kutoogopa kifo na pia hiyo ilinithibitishia kwamba wenzangu sasa watakuwa tayari kutoa siri zetu zote. Dakika kama mbili baadaye askari jeshi watatu walisimama hatua kama tano mbele yetu na kutulenga kwa bunduki zao.
Wakati nikianza kumuomba Mungu anisamehe makosa yangu niliyomkosea ili anipokee huko mbinguni, ghafla ilifika gari moja aina ya Jeep ikiwa na askari mmoja mwenye cheo cha kanali na mwingine aliyevaa Kaunda suti ya rangi ya kijivu ambaye nilimuhisi ni afisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ya Iddi Amin inayoitwa SRB. Maofisa hao waliteremka kwenye gari na kutusogelea.
“Naona nyinyi ni vijana wadogo sana, kwa hiyo najua hampendi kufa au siyo?” aliuliza kanali huyo huku akitukazia macho. Wote tulikaa kimya bila kutoa jibu lolote wala kukohoa.
“Nani mkubwa kati yenu kwa cheo? Aliuliza ofisa aliyevaa kiraia lakini naye hakupata jibu.
“Nataka kuwahakikishieni kitu kimoja, atakayekuwa mkweli hatutamuua na kwa kuwa tutamhoji kila mtu peke yake inabidi hapa tuwafunge mmoja mmoja. Mtu mjeuri hapa ndio utakuwa mwisho wake” alitamka kanali huyo kwa ukali. “O.K fungua hawa wawili abakie huyu,” aliamuru aliyevaa kiraia.
Mimi na Koplo Sudi tulifunguliwa na kurudishwa mahabusu, Sajini Binda tukamwacha akiwa bado amefungwa. “Hata kama ukisema ukweli haiwezi kuwazuia kutuua. Kumbuka kiapo chako usiwe mwoga.” Nilimkumbusha Koplo Sudi. “Lakini, lakini afande….” “Shii, kumbuka kiapo , usiwe mwoga, kama ni kifo acha tukikabili.” Nilisisitiza.
Kabla ya Koplo Sudi hajaendelea kutamka neno linguine tukasikia mlio wa risasi tatu ambazo zilitufanya tupate kiwewe cha ghafla.
“Wameshamuua, wameshamuua.” Alilalamika Koplo Sudi. Mimi sikumjibu lolote bali nilimkazia macho tu, alipoona hivyo aliinuka haraka alipokaa na kuniangukia miguuni kwangu huku akilia.
“Watatuua wote afande,” alilalamika. “Wacha tufe lakini kumbuka kiapo, usiwe mwoga,” nilimjibu huku na mimi nikitoa mchozi wa chuki.
“Nisaidie afande, naogopa sana.” Alizidi kulalamika. “Nyamaza!” nilimwamuru kwa ukali, akanyamaza. Punde kidogo mlango ulifunguliwa na polisi jeshi mmoja. “Nani ndiye Koplo Sudi?” aliuliza askari huyo akiwa amesimama mlangoni. Koplo Sudi hakujibu bali aliongeza kasi ya kulia na kumfanya askari huyo aje juu.
“Nauliza nani ndiye Koplo Sudi sitaki kusikia kilio.” Alifoka. “Ni mimi, ni mimi.” Hatimaye alijibu. “Kuja hapa haraka.” Aliamuru kwa ukali. Koplo Sudi aliinuka na kumfuata.
Alipotoka mlango ukafungwa, nikabaki ndani peke yangu. Sasa nikajua siri zimeanza kutoka, kama wamemjua Koplo Sudi bila shaka Sajini Binda amekwishawaeleza mengi. Hofu ikazidi kuniingia, nikajua sasa watanishughulikia mimi kikamilifu wapate siri. Niliwaza sana bila kupata jibu lolote, tama ya kujiokoa ikaanza kujengeka polepole akilini mwangu.
“Wakishajua mimi ndiye kiongozi hasira zao zote zitaniangukia mimi.” Nilijisemea peke yangu kama mwehu. Dakika kama ishiriki baadaye nikasikia mlio wa risasi mbili nikajua Koplo Sudi naye ameshauawa. Hofu ikanizidi, nikajua zamu yangu ya kutolewa roho imekaribia. Nilimkumbuka Mungu, nikamwomba aniokoe na kifo hicho, nikalia sana, lakini sikulia kwa hofu ya kifo bali nilimlilia Mungu aniepushie balaa hilo. Kilio change kilikatizwa ghafla na sauti ya polisi jeshi aliyekuwa mlangoni.
“Unalia huku umepiga magoti na mikono juu unamwomba Mungu eee! Alitamka askari huyo kunigutua. Haraka nilifuta machozi yangu, kwa kweli nilipata nguvu mpya, hofu ya kifo ilinitoka kabisa, nilihisi ni sababu ya kilio changu kwa Mungu.
“Wewe ndiyo Luteni, siyo?” aliniuliza huku akitabasamu. “Umetumwa unite au uniulize swali?” nilijibu kwa upole huku nikitabasamu.
“Haya unaitwa,” alitamka huku akiendelea kutabasamu. Niliinuka haraka tukaongozana hadi kule kwenye uwanja wa mauaji ambako nilipaita machinjioni. Nilipofika hapo nikafungwa kamba kama awali kisha askari wanne wenye silaha wakajipanga mbele yangu wakingoja amri ya kunifyatulia risasi. Baada ya kufungwa kamba nikaoiona tena ile gari aina ya Jeep ikija na baadaye ikasimama palepale iliposimama mwanzoni. Yule kanali na mwenzake aliyevaa kiraia ambaye nilimuhisi ni afisa usalama wa taifa kutoka SRB, walinisogelea tena kama walivyofanya mwanzoni. Muda wote huo nilikuwa naichunguza ile miti kuona kama ina damu ili nipate uhakika kama wenzangu kweli wameuawa.
Hata hivyo sikuona damu yoyote katika miti hiyo kwa hiyo nikahisi umetumika ujanja wa kututisha lakini kama wametumia mbinu hiyo basi wamesahau kupata miti hiyo japo rangi inayofanana na damu.
“Wewe ndiyo Luteni Njata au siyo?” aliniuliza huyo aliyevaa kiraia. “Unaniambia au unaniuliza?” nilimjibu bila hofu. “Wenzako wote wamekubali kushirikiana nasi na wamejibu vizuri lakini tumewaua kwa ujeuri wao.” Alieleza kanali huyo.
Maneno haya niliyatafakari na kugundua wenzangu hawajauawa bali wamenigeresha mimi kwa milio ya risasi tu. “Sasa jibu maswali yetu vizuri na kwa usahihi, udanganyifu wowote utakaofanya utasababisha uwafuate wenzako huko ahera, umenielewa?” alitamka.
“Nimekuelewa bwana.” Nilijibu kwa upole. “Wewe tumeambiwa ndiyo kiongozi wa wenzako na cheo chako ni luteni, kweli?”. “Kweli” nilijibu kwa upole huku nikimkazia macho. “Unaongoza askari wangapi pale Murongo?” ofisa aliyevaa kiraia aliniuliza.
“Nawaongoza hao hao wawili waliowaambia mimi ni kiongozi wao.” “Yaani wewe ni kiongozi wa askari wawili tu, kambi gani hiyo ya watu wawili?” aliuliza kanali. “Kwani wameaambia tupo wangapi?” “Ah? Yaani wewe badala ya kutujibu maswali yetu, unatuuliza sisi maswali tukujibu?” alifoka huyo aliyevaa kiraia.
“Siyo hivyo wakubwa, maswali yenu mengine najua majibu mnayo wenyewe, sasa mimi nashangaa mkiniuliza. Mnanichelewesha bure kunipiga risasi, niuweni roho zenu zitulie.” Nilijibu kwa utulivu mkubwa uliowafanya wanishangae. “Wewe huogopi kufa?” aliniuliza kanali huku akinikazia macho.
“Kila mtu atakufa hapa duniani hata kama utamtanguliza mwenzio kufa ujue iko siku na wewe utamfuata.” Nilijibu na kuwafanya wazidi kunishangaa. “O.k. sawa bwana, sasa pale Murongo kuna kambi ya jeshi?” aliuliza kanali. “Hakuna” nilijibu kwa mkato.
“Kumbe nyinyi ni askari mnaofanya nini pale kijijini?” alifoka aliyevaa kiraia. “Tunataka kufundisha askari raia yaani mgambo.” “Mmeshaanza kuwafundisha?” alizidi kuuliza. “Bado labda mwezi ujao tutaanza.” “Kitu gani kinachowafanya muanze kufundisha mwezi ujao?” ofisa huyo aliuliza. “Bado hatujakamilisha mipango ya kupata vifaa na watu wa kuwafundisha.” “Unaona unavyojibu vizuri? Wewe sasa utakuwa rafiki yetu hatuwezi kukuua.” Alitamka kanali huku akitabasamu.
“Pale Murongo kuna redio ya mawasiliano?” alizidi kuuliza ofisa huyo huku akiandika. “Ipo.” Nilijibu nikijua wenzangu wameshaeleza yote. “Ipo sehemu gani pale Murongo?” aliuliza kanali.
“Kwa kweli ni vigumu, labda twendeni nikawaonyeshe huko huko,” nilijibu kwa upole na kuwafanya wacheke sana. “Wewe mjanja sana, kweli wewe ni ofisa wa jeshi,” alisifu ofisa huyo aliyevaa kiraia.
“Hebu mfungueni kamba, huyu sasa ni rafiki yetu, ameonesha ushirikiano, tutawarudishia Murongo,” aliamuru kanali kisha wakaingia kwenye gari yao na kuondoka. Polisi jeshi mmoja alinifungua kamba na baadaye wakanirudisha mahabusu ambako niliwakuta Sajini Binda na Koplo Sudi wakinywa uji. Sikuwasemesha kitu nilikaa kwa huzuni huku nikiwakazia macho.
“Mmewaeleza mambo mengi sana mkifirikia ni njia ya kujinusuru katika mikono yao, siyo?” niliwauliza kwa upole lakini sikupata jibu. “Tuone sasa kama kweli wataturudisha Murongo baada ya kuwapa wanachokitaka,” nilizidi kueleza.
“Nani kati yenu aliulizwa juu ya masafa (frequency) ya redio yetu ya mawasiliano?” niliwauliza lakini hakuna aliyenijibu.
Hali hiyo ilinithibitishia kwamba wameeleza mambo mengi sana na sasa wanaona aibu hata kuongea na mimi. “Ndiyo maana hawakuniuliza maswali mengi kwa kuwa mengi wamekwishaelezwa na hawa.” Niliwaza.
Jioni ilipofika tulitolewa humo mahabusu tukiwa tumefungwa vitambaa vyeusi usoni na pingu mikononi, tukaingizwa ndani ya lori moja. Dakika chache baadaye lori hilo liliondoka kuelekea tusipopafahamu lakini tulitumia muda wa dakika kama ishirini au ishirini na tano hivi ndipo lori hilo liliposimama. Tuliteremshwa na kuongozwa hadi kwenye ngazi fulani ambako tuliteremka chini hadi kwenye chumba kimoja chenye hewa nzito na harufu mbaya ya mikojo na damu.
Humo tulifunguliwa vitambaa tulivyofungwa lakini ikawa sawa na tulivyofungwa kutokana na giza la humo ndani. Hali ya mahabusu ile ya Makindye ilikuwa ni afadhali kuliko hii inayotisha. Tulitulia kimya sakafuni bila kusemezana kitu kutokana na utisho wa humo ndani. Hata hivyo kwa kawaida maongezi yananoga unapoongea na mtu huku unamuona, sasa hii giza imevunja hata hamu ya kuongea.
Tulikaa humo ndani bila kufahamu kama ni jioni, usiku au asubuhi imefika. Kwa kadiri nilivyotafakari jinsi tulivyokamatwa na tulivyofanyiwa ni dhahifi kifo kilikuwa bado kinatuandama. Uchovu na njaa ndiyo vitu vya kwanza kutishia maisha yetu hasa mimi ambaye nilikuwa sijaonja kitu chochote kwa siku mbili. Wakati tukiwa bado hatujui la kufanya tulisikia sauti kutoka kwenye kipaza sauti kidogo kilichokuwa humo ndani.
“Luteni Njata na Sajini Binda kuja nje haraka.” Sauti hiyo iliamuru na wakati huo huo mlango mzito wa chuma ulijifungua tukaona mwanga kidogo mbele yetu. Mimi na Sajini Binda tuliinuka na kuuendea mlango huo lakini Koplo Sudi alimshika Sajini Binda huku akilia sana akimuomba asimuache. Nilishangaa sana kwa nini amshikilie Sajini binda badala ya mimi mkubwa wao. Hata hivyo baadaye nilihisi labda kwa vile mimi amekwishaniudhi kwa kusaliti kiapo cha jeshi letu. Sajini Binda alipoona Koplo Sudi hamuachi, akaamua kutoka naye. Tulitokea kwenye ukumbi mrefu ambako tuliwakuta vijana wawili waliovalia Kaunda suti zao maridadi wakitusibiri.
“Mmeitwa wawili mnakuja watatu, nyinyi watu vipi?” alifoka mmoja wao ambaye ni mfupi kidogo kuliko mwenzake. “Huyu mwenzetu anaogopa kubaki peke yake” alijibu Sajini Binda.
“O.K. njooni huku.” Alitamka huku akitangulia mbele. Kwa kweli humo ndani kulionesha wazi ni sehemu ya mauaji. Tuliongozana na maofisa hao katika ukumbi huo mrefu uliokuwa unawake taa hadi kwenye mlango mwingine wa chuma uliokuwa upande wa kushoto. Ofisa huyo aliugonga mlango huo kwa kutumia chuma cha kufungia nje na baada ya sekunde chache ukafunguliwa.
Bila kuongea na aliyeufungua mlango huo, akatuonyesha ishara tuingie ndani. Sajini Binda na Koplo Sudi walitangulia kuingia wakifuatiwa na mimi. Maofisa waliotuleta wakafunga mlango huo kwa nje na kuondoka zao. Humo ndani tulikuta ukumbi mrefu kidogo uliojaa harufu mbaya zaidi kuliko kule tulipowekwa mwanzo. Kulikuwa na nyororo nyingi zilizofungwa ukutani ambazo zilinijulisha ni za kufungia watu. Mbele kidogo ya ukumbi tulikuta watu wanne wamefungwa nyororo mikononi wakiwa wamesimama wima lakini vichwa vyao upande wa sura wameangushia vifuani mwao huku damu zikiwatoka mdomoni, puani na masikioni. Walionesha uhai umekwishawatoka. Kuona hivyo, Koplo Sudi alianza kutapika hatimaye akazirai.
Wakati tunamhudumia Koplo Sudi kwa kumpepea kwa mashati yetu tuliyoyavua, mlango uliokuwa juu ya ngazi mbele yetu ukafunguliwa. Wanaume sita vipande vya baba wakaingia na kusimama mbele yetu. Miamba hiyo ya watu ilikuwa vidari wazi na walivaa chupi tupu. Hakika unaweza kuzimia kabla hawajakugusa. Jinsi maumbile yao yalivyo na sura zao mbaya za kutisha ni dhahiri wamewekwa maalumu kwa ajili ya utesaji hadi kuua. Moyoni nilijua wazi tupo katika jengo maalumu la Idara ya Ujasusi ya Iddi Amin (SRB) la kuhojia watu. Tukaamriwa tuvue nguo zetu zote tubaki kama tulivyozaliwa. Baadaye watu hao wakaanza kutupiga mgongoni kwa kutumia waya fulani bila ya kutusemesha kitu. Ulikuwa ni muda wa adha kubwa ambayo tangu nizaliwe sijawahi kuipata. Koplo Sudi alizimia tena akifuatiwa na Sajini Binda lakini wauaji hao waliendelea kuwapiga hadi mimi nikaona niwaokoe.
abu cha ukachero wa kachero wa Tanzania – 3
Habari Zinazoendana
Share
…………….
KATIKA wiki mbili zilizopita tumechapisha sehemu mbili za uchambuzi wa wa kitabu kipya kinachoitwa MATEKA MPAKANI kilichoandikwa na kachero wa Tanzania, Frown Kageuka (pichani) kumuenzi mwenzake aliyeuawa mpakani mwa Tanzania na Uganda na majasusi wa aliyekuwa Rais wa Uganda, Idi Amin. Leo tunaendelea na sehemu ya tatu ya mfululizo wa uchambuzi wa kitabu hicho.
……………
TULIFIKA Makindye usiku, eneo hilo lilifanana sana na Manzese ya Dar es Salaam. Kwa hakika safari yetu ilikuwa ndefu sana kwa hiyo nilihisi tumeingia ndani sana ya nchi ya Uganda na labda tulikuwa karibu na Kampala.
Tuliteremshwa ‘kikuku’ na kuingizwa katika nyumba moja ambayo nilihisi ni mahabusu. Tuliachwa humo tukiwa bado na kamba miguuni na mikononi hadi alfajiri. Usiku wote hatukuweza kuongea lakini asubuhi nilijua tupo wote pamoja baada ya Koplo Sudi kumwambia Sajini Binda kwamba ana njaa sana. Kwa kweli hata mimi nilikuwa na njaa sana lakini hatukuwa na la kufanya. Jua lilipoanza kuonesha makali yake tulifunguliwa kamba tulizofungwa na askari mmoja mwenye cheo cha Sajin.
“Mnataka chai au uji? Aliuliza Sajini huyo ambaye alionyesha ni katili sana. “Chochote unachoona tunastahili,” nilijib kwa upole. “Mimi nawapa uchaguzi nyinyi wafungwa,” alijibu Sajin huyo na kuondoka.
Dakika kama tano hivi baadaye mlango ulifunguliwa na Sajini yule yule aliyekuwapo awali, akaingia ndani akifuatiwa na askari mmoja asiye na cheo ambaye amebeba birika na vikombe vitatu vya bati.
“Haya punguzeni njaa kwa mlo huu nyie wafungwa” alitamka Sajin huyo kwa kebehi huku mwenzake akiweka birika na vikombe karibu yetu na kuondoka.
“Kwani sisi ni wafungwa?” niliuliza kwa upole huku nikimkazia macho. “Eh! Kumbe nyinyi ni kina nani?” alijibu Sajenti huyo huku akinitolea macho. “Sisi sio wafungwa bwana. Tunashangaa jinsi mlivyotukamata na kutuleta hapa.” “Hayo mimi sijui, ninachokijua nyingi ni askati mateka kutoka Tanzania kwa hiyo ni wafungwa.”
“Sisi sio askari bwana, kama mmeambiwa hivyo mmedanganywa kabisa. Mmeshindwa kuwapata askari halisi mkatukamata sisi raia na kutuita askari. Huo ni uonevu mkubwa,” nilimwambia kwa upole.
“Nyinyi watu wa Tanzania Kiswahili kirefu sana, kama siyo askari mmmefikaje hapa Makindye?” aliuliza kwa mshangao huku akituthitibishia hapo tulipo ni Makindye.
“Lakini kama sisi ni wanajeshi kama mnavyotaka tuwe, basi inabidi mtupe huduma sawa na mkataba wa Geneva unaohusu wafungwa wa kivita.” “Wewe mbona unaongea sana? Au ndiyo mkubwa?” aliniuliza kwa ukali na kuondoka zake.
“Inaonyesha hawa wanampango mbaya na sisi, hapa walipotuleta ni ndani kabisa ya nchi yao, ni maili chache tu kufika mjini Kampala. Sijui kama tutarudi salama. Iddi Amin hajawahi kuachia mtu salama na hasa waliokamatwa kimya kimya kama sisi. Ni lazima tufanye kitu ili tujiokoe” niliwaeleza wenzangu kwa sauti ya chini lakini kabla hawajanijibu mlango ulifunguliwa. Askari mmoja aliyevalia rasmi kipolisi jeshi (Military Police) alituamuru tutoke nje haraka. Hapo nje tuliwakuta askari wengine sita waliokuwa na bunduki aina ya AK 47 kila mmoja.
Tulifungwa pingu mikononi na kuongozwa hadi kwenye uwanja ambao bila ya kuamiwa nilijua ni sehemu ya kuulia watu kwa kupigwa risasi. Tulifungwa katika miti iliyokuwa mbele ya magunia mengi ya mchanga ambayo nilijua ni maalumu kwa kuzuia risasi isiende mbali ya hapo.
Baada ya kufungwa kamba kuzunguka mti nilijiona nimeshakuwa mfu. Koplo Sudi na Sajini Binda walianza kulia kama watoto wadogo. Niliogopa sana hali hiyo, kwa vile nilijua Waganda hao watagundua mimi ni kiongozi wao kutokana na ujasiri wa kutoogopa kifo na pia hiyo ilinithibitishia kwamba wenzangu sasa watakuwa tayari kutoa siri zetu zote. Dakika kama mbili baadaye askari jeshi watatu walisimama hatua kama tano mbele yetu na kutulenga kwa bunduki zao.
Wakati nikianza kumuomba Mungu anisamehe makosa yangu niliyomkosea ili anipokee huko mbinguni, ghafla ilifika gari moja aina ya Jeep ikiwa na askari mmoja mwenye cheo cha kanali na mwingine aliyevaa Kaunda suti ya rangi ya kijivu ambaye nilimuhisi ni afisa wa Idara ya Usalama wa Taifa ya Iddi Amin inayoitwa SRB. Maofisa hao waliteremka kwenye gari na kutusogelea.
“Naona nyinyi ni vijana wadogo sana, kwa hiyo najua hampendi kufa au siyo?” aliuliza kanali huyo huku akitukazia macho. Wote tulikaa kimya bila kutoa jibu lolote wala kukohoa.
“Nani mkubwa kati yenu kwa cheo? Aliuliza ofisa aliyevaa kiraia lakini naye hakupata jibu.
“Nataka kuwahakikishieni kitu kimoja, atakayekuwa mkweli hatutamuua na kwa kuwa tutamhoji kila mtu peke yake inabidi hapa tuwafunge mmoja mmoja. Mtu mjeuri hapa ndio utakuwa mwisho wake” alitamka kanali huyo kwa ukali. “O.K fungua hawa wawili abakie huyu,” aliamuru aliyevaa kiraia.
Mimi na Koplo Sudi tulifunguliwa na kurudishwa mahabusu, Sajini Binda tukamwacha akiwa bado amefungwa. “Hata kama ukisema ukweli haiwezi kuwazuia kutuua. Kumbuka kiapo chako usiwe mwoga.” Nilimkumbusha Koplo Sudi. “Lakini, lakini afande….” “Shii, kumbuka kiapo , usiwe mwoga, kama ni kifo acha tukikabili.” Nilisisitiza.
Kabla ya Koplo Sudi hajaendelea kutamka neno linguine tukasikia mlio wa risasi tatu ambazo zilitufanya tupate kiwewe cha ghafla.
“Wameshamuua, wameshamuua.” Alilalamika Koplo Sudi. Mimi sikumjibu lolote bali nilimkazia macho tu, alipoona hivyo aliinuka haraka alipokaa na kuniangukia miguuni kwangu huku akilia.
“Watatuua wote afande,” alilalamika. “Wacha tufe lakini kumbuka kiapo, usiwe mwoga,” nilimjibu huku na mimi nikitoa mchozi wa chuki.
“Nisaidie afande, naogopa sana.” Alizidi kulalamika. “Nyamaza!” nilimwamuru kwa ukali, akanyamaza. Punde kidogo mlango ulifunguliwa na polisi jeshi mmoja. “Nani ndiye Koplo Sudi?” aliuliza askari huyo akiwa amesimama mlangoni. Koplo Sudi hakujibu bali aliongeza kasi ya kulia na kumfanya askari huyo aje juu.
“Nauliza nani ndiye Koplo Sudi sitaki kusikia kilio.” Alifoka. “Ni mimi, ni mimi.” Hatimaye alijibu. “Kuja hapa haraka.” Aliamuru kwa ukali. Koplo Sudi aliinuka na kumfuata.
Alipotoka mlango ukafungwa, nikabaki ndani peke yangu. Sasa nikajua siri zimeanza kutoka, kama wamemjua Koplo Sudi bila shaka Sajini Binda amekwishawaeleza mengi. Hofu ikazidi kuniingia, nikajua sasa watanishughulikia mimi kikamilifu wapate siri. Niliwaza sana bila kupata jibu lolote, tama ya kujiokoa ikaanza kujengeka polepole akilini mwangu.
“Wakishajua mimi ndiye kiongozi hasira zao zote zitaniangukia mimi.” Nilijisemea peke yangu kama mwehu. Dakika kama ishiriki baadaye nikasikia mlio wa risasi mbili nikajua Koplo Sudi naye ameshauawa. Hofu ikanizidi, nikajua zamu yangu ya kutolewa roho imekaribia. Nilimkumbuka Mungu, nikamwomba aniokoe na kifo hicho, nikalia sana, lakini sikulia kwa hofu ya kifo bali nilimlilia Mungu aniepushie balaa hilo. Kilio change kilikatizwa ghafla na sauti ya polisi jeshi aliyekuwa mlangoni.
“Unalia huku umepiga magoti na mikono juu unamwomba Mungu eee! Alitamka askari huyo kunigutua. Haraka nilifuta machozi yangu, kwa kweli nilipata nguvu mpya, hofu ya kifo ilinitoka kabisa, nilihisi ni sababu ya kilio changu kwa Mungu.
“Wewe ndiyo Luteni, siyo?” aliniuliza huku akitabasamu. “Umetumwa unite au uniulize swali?” nilijibu kwa upole huku nikitabasamu.
“Haya unaitwa,” alitamka huku akiendelea kutabasamu. Niliinuka haraka tukaongozana hadi kule kwenye uwanja wa mauaji ambako nilipaita machinjioni. Nilipofika hapo nikafungwa kamba kama awali kisha askari wanne wenye silaha wakajipanga mbele yangu wakingoja amri ya kunifyatulia risasi. Baada ya kufungwa kamba nikaoiona tena ile gari aina ya Jeep ikija na baadaye ikasimama palepale iliposimama mwanzoni. Yule kanali na mwenzake aliyevaa kiraia ambaye nilimuhisi ni afisa usalama wa taifa kutoka SRB, walinisogelea tena kama walivyofanya mwanzoni. Muda wote huo nilikuwa naichunguza ile miti kuona kama ina damu ili nipate uhakika kama wenzangu kweli wameuawa.
Hata hivyo sikuona damu yoyote katika miti hiyo kwa hiyo nikahisi umetumika ujanja wa kututisha lakini kama wametumia mbinu hiyo basi wamesahau kupata miti hiyo japo rangi inayofanana na damu.
“Wewe ndiyo Luteni Njata au siyo?” aliniuliza huyo aliyevaa kiraia. “Unaniambia au unaniuliza?” nilimjibu bila hofu. “Wenzako wote wamekubali kushirikiana nasi na wamejibu vizuri lakini tumewaua kwa ujeuri wao.” Alieleza kanali huyo.
Maneno haya niliyatafakari na kugundua wenzangu hawajauawa bali wamenigeresha mimi kwa milio ya risasi tu. “Sasa jibu maswali yetu vizuri na kwa usahihi, udanganyifu wowote utakaofanya utasababisha uwafuate wenzako huko ahera, umenielewa?” alitamka.
“Nimekuelewa bwana.” Nilijibu kwa upole. “Wewe tumeambiwa ndiyo kiongozi wa wenzako na cheo chako ni luteni, kweli?”. “Kweli” nilijibu kwa upole huku nikimkazia macho. “Unaongoza askari wangapi pale Murongo?” ofisa aliyevaa kiraia aliniuliza.
“Nawaongoza hao hao wawili waliowaambia mimi ni kiongozi wao.” “Yaani wewe ni kiongozi wa askari wawili tu, kambi gani hiyo ya watu wawili?” aliuliza kanali. “Kwani wameaambia tupo wangapi?” “Ah? Yaani wewe badala ya kutujibu maswali yetu, unatuuliza sisi maswali tukujibu?” alifoka huyo aliyevaa kiraia.
“Siyo hivyo wakubwa, maswali yenu mengine najua majibu mnayo wenyewe, sasa mimi nashangaa mkiniuliza. Mnanichelewesha bure kunipiga risasi, niuweni roho zenu zitulie.” Nilijibu kwa utulivu mkubwa uliowafanya wanishangae. “Wewe huogopi kufa?” aliniuliza kanali huku akinikazia macho.
“Kila mtu atakufa hapa duniani hata kama utamtanguliza mwenzio kufa ujue iko siku na wewe utamfuata.” Nilijibu na kuwafanya wazidi kunishangaa. “O.k. sawa bwana, sasa pale Murongo kuna kambi ya jeshi?” aliuliza kanali. “Hakuna” nilijibu kwa mkato.
“Kumbe nyinyi ni askari mnaofanya nini pale kijijini?” alifoka aliyevaa kiraia. “Tunataka kufundisha askari raia yaani mgambo.” “Mmeshaanza kuwafundisha?” alizidi kuuliza. “Bado labda mwezi ujao tutaanza.” “Kitu gani kinachowafanya muanze kufundisha mwezi ujao?” ofisa huyo aliuliza. “Bado hatujakamilisha mipango ya kupata vifaa na watu wa kuwafundisha.” “Unaona unavyojibu vizuri? Wewe sasa utakuwa rafiki yetu hatuwezi kukuua.” Alitamka kanali huku akitabasamu.
“Pale Murongo kuna redio ya mawasiliano?” alizidi kuuliza ofisa huyo huku akiandika. “Ipo.” Nilijibu nikijua wenzangu wameshaeleza yote. “Ipo sehemu gani pale Murongo?” aliuliza kanali.
“Kwa kweli ni vigumu, labda twendeni nikawaonyeshe huko huko,” nilijibu kwa upole na kuwafanya wacheke sana. “Wewe mjanja sana, kweli wewe ni ofisa wa jeshi,” alisifu ofisa huyo aliyevaa kiraia.
“Hebu mfungueni kamba, huyu sasa ni rafiki yetu, ameonesha ushirikiano, tutawarudishia Murongo,” aliamuru kanali kisha wakaingia kwenye gari yao na kuondoka. Polisi jeshi mmoja alinifungua kamba na baadaye wakanirudisha mahabusu ambako niliwakuta Sajini Binda na Koplo Sudi wakinywa uji. Sikuwasemesha kitu nilikaa kwa huzuni huku nikiwakazia macho.
“Mmewaeleza mambo mengi sana mkifirikia ni njia ya kujinusuru katika mikono yao, siyo?” niliwauliza kwa upole lakini sikupata jibu. “Tuone sasa kama kweli wataturudisha Murongo baada ya kuwapa wanachokitaka,” nilizidi kueleza.
“Nani kati yenu aliulizwa juu ya masafa (frequency) ya redio yetu ya mawasiliano?” niliwauliza lakini hakuna aliyenijibu.
Hali hiyo ilinithibitishia kwamba wameeleza mambo mengi sana na sasa wanaona aibu hata kuongea na mimi. “Ndiyo maana hawakuniuliza maswali mengi kwa kuwa mengi wamekwishaelezwa na hawa.” Niliwaza.
Jioni ilipofika tulitolewa humo mahabusu tukiwa tumefungwa vitambaa vyeusi usoni na pingu mikononi, tukaingizwa ndani ya lori moja. Dakika chache baadaye lori hilo liliondoka kuelekea tusipopafahamu lakini tulitumia muda wa dakika kama ishirini au ishirini na tano hivi ndipo lori hilo liliposimama. Tuliteremshwa na kuongozwa hadi kwenye ngazi fulani ambako tuliteremka chini hadi kwenye chumba kimoja chenye hewa nzito na harufu mbaya ya mikojo na damu.
Humo tulifunguliwa vitambaa tulivyofungwa lakini ikawa sawa na tulivyofungwa kutokana na giza la humo ndani. Hali ya mahabusu ile ya Makindye ilikuwa ni afadhali kuliko hii inayotisha. Tulitulia kimya sakafuni bila kusemezana kitu kutokana na utisho wa humo ndani. Hata hivyo kwa kawaida maongezi yananoga unapoongea na mtu huku unamuona, sasa hii giza imevunja hata hamu ya kuongea.
Tulikaa humo ndani bila kufahamu kama ni jioni, usiku au asubuhi imefika. Kwa kadiri nilivyotafakari jinsi tulivyokamatwa na tulivyofanyiwa ni dhahifi kifo kilikuwa bado kinatuandama. Uchovu na njaa ndiyo vitu vya kwanza kutishia maisha yetu hasa mimi ambaye nilikuwa sijaonja kitu chochote kwa siku mbili. Wakati tukiwa bado hatujui la kufanya tulisikia sauti kutoka kwenye kipaza sauti kidogo kilichokuwa humo ndani.
“Luteni Njata na Sajini Binda kuja nje haraka.” Sauti hiyo iliamuru na wakati huo huo mlango mzito wa chuma ulijifungua tukaona mwanga kidogo mbele yetu. Mimi na Sajini Binda tuliinuka na kuuendea mlango huo lakini Koplo Sudi alimshika Sajini Binda huku akilia sana akimuomba asimuache. Nilishangaa sana kwa nini amshikilie Sajini binda badala ya mimi mkubwa wao. Hata hivyo baadaye nilihisi labda kwa vile mimi amekwishaniudhi kwa kusaliti kiapo cha jeshi letu. Sajini Binda alipoona Koplo Sudi hamuachi, akaamua kutoka naye. Tulitokea kwenye ukumbi mrefu ambako tuliwakuta vijana wawili waliovalia Kaunda suti zao maridadi wakitusibiri.
“Mmeitwa wawili mnakuja watatu, nyinyi watu vipi?” alifoka mmoja wao ambaye ni mfupi kidogo kuliko mwenzake. “Huyu mwenzetu anaogopa kubaki peke yake” alijibu Sajini Binda.
“O.K. njooni huku.” Alitamka huku akitangulia mbele. Kwa kweli humo ndani kulionesha wazi ni sehemu ya mauaji. Tuliongozana na maofisa hao katika ukumbi huo mrefu uliokuwa unawake taa hadi kwenye mlango mwingine wa chuma uliokuwa upande wa kushoto. Ofisa huyo aliugonga mlango huo kwa kutumia chuma cha kufungia nje na baada ya sekunde chache ukafunguliwa.
Bila kuongea na aliyeufungua mlango huo, akatuonyesha ishara tuingie ndani. Sajini Binda na Koplo Sudi walitangulia kuingia wakifuatiwa na mimi. Maofisa waliotuleta wakafunga mlango huo kwa nje na kuondoka zao. Humo ndani tulikuta ukumbi mrefu kidogo uliojaa harufu mbaya zaidi kuliko kule tulipowekwa mwanzo. Kulikuwa na nyororo nyingi zilizofungwa ukutani ambazo zilinijulisha ni za kufungia watu. Mbele kidogo ya ukumbi tulikuta watu wanne wamefungwa nyororo mikononi wakiwa wamesimama wima lakini vichwa vyao upande wa sura wameangushia vifuani mwao huku damu zikiwatoka mdomoni, puani na masikioni. Walionesha uhai umekwishawatoka. Kuona hivyo, Koplo Sudi alianza kutapika hatimaye akazirai.
Wakati tunamhudumia Koplo Sudi kwa kumpepea kwa mashati yetu tuliyoyavua, mlango uliokuwa juu ya ngazi mbele yetu ukafunguliwa. Wanaume sita vipande vya baba wakaingia na kusimama mbele yetu. Miamba hiyo ya watu ilikuwa vidari wazi na walivaa chupi tupu. Hakika unaweza kuzimia kabla hawajakugusa. Jinsi maumbile yao yalivyo na sura zao mbaya za kutisha ni dhahiri wamewekwa maalumu kwa ajili ya utesaji hadi kuua. Moyoni nilijua wazi tupo katika jengo maalumu la Idara ya Ujasusi ya Iddi Amin (SRB) la kuhojia watu. Tukaamriwa tuvue nguo zetu zote tubaki kama tulivyozaliwa. Baadaye watu hao wakaanza kutupiga mgongoni kwa kutumia waya fulani bila ya kutusemesha kitu. Ulikuwa ni muda wa adha kubwa ambayo tangu nizaliwe sijawahi kuipata. Koplo Sudi alizimia tena akifuatiwa na Sajini Binda lakini wauaji hao waliendelea kuwapiga hadi mimi nikaona niwaokoe.