Wakuu bado nipo hapa Dodoma kwa takriban wiki sasa. Lengo ni kuwajuza kinachojiri katika mchakato wa CCM wa kumchagua mgombea wake wa Urais.
Jana lile Jasusi na Kachero Mstaafu wa Idara Ya Usalama Wa Taifa, Colonel Apson Mwang'onda limewasili hapa Dodoma. Amefikia Kitori Hotel iliyopo eneo la Iringa Road hapa Dodoma.
"Nimekuja hapa kwa kazi moja tu kuhakikisha Edward Lowassa kamwe Hachaguliwi kuwa Rais wa nchi hii", nilimnukuu Jasusi huyo akijigamba kwa Mtu wake wa karibu aliyekuwa naye hotelini hapo.
Inaelekea Jasusi huyu (Apson) amebadili msimamo kwani miezi michache tu iliyopita alikuwa anampigania Lowassa usiku na mchana ili awe Rais wa Awamu ya Tano.
Lakini sasa amemgeuka. Sababu ya kumgeuka inasemekana ni baada ya kunusa harufu ya kubaini kuwa Lowassa siyo chaguo la Wenye nchi na jina lake halitorudi katika vikao vya uteuzi vya CCM.
Ama kweli Majasusi hawatabiriki, wanabadilika kama Vinyonga. Leo wapo huku, kesho wanahamia kule. Utafiti wangu unaonyesha kuwa Sababu kubwa za Apson kukorofishana na Lowassa ni Fitina za Rostam Aziz ambaye hataki hata kumsikia Apson kuwepo katika timu yao ya kampeni.
Rostam hampendi na anamtuhumu sana Apson kwamba ni Kibaraka wa Serikali.
Hivyo alimtimua katika vikao vya Team Lowassa. Ntaendelea kuwajuza.
Jana lile Jasusi na Kachero Mstaafu wa Idara Ya Usalama Wa Taifa, Colonel Apson Mwang'onda limewasili hapa Dodoma. Amefikia Kitori Hotel iliyopo eneo la Iringa Road hapa Dodoma.
"Nimekuja hapa kwa kazi moja tu kuhakikisha Edward Lowassa kamwe Hachaguliwi kuwa Rais wa nchi hii", nilimnukuu Jasusi huyo akijigamba kwa Mtu wake wa karibu aliyekuwa naye hotelini hapo.
Inaelekea Jasusi huyu (Apson) amebadili msimamo kwani miezi michache tu iliyopita alikuwa anampigania Lowassa usiku na mchana ili awe Rais wa Awamu ya Tano.
Lakini sasa amemgeuka. Sababu ya kumgeuka inasemekana ni baada ya kunusa harufu ya kubaini kuwa Lowassa siyo chaguo la Wenye nchi na jina lake halitorudi katika vikao vya uteuzi vya CCM.
Ama kweli Majasusi hawatabiriki, wanabadilika kama Vinyonga. Leo wapo huku, kesho wanahamia kule. Utafiti wangu unaonyesha kuwa Sababu kubwa za Apson kukorofishana na Lowassa ni Fitina za Rostam Aziz ambaye hataki hata kumsikia Apson kuwepo katika timu yao ya kampeni.
Rostam hampendi na anamtuhumu sana Apson kwamba ni Kibaraka wa Serikali.
Hivyo alimtimua katika vikao vya Team Lowassa. Ntaendelea kuwajuza.