Jasho La Mkulima

Augustine Moshi

JF-Expert Member
Apr 22, 2006
2,554
1,382
Serikali Iache Kudhalilish Wakulima.

Wakulima wadogo wanapata taabu sana. Kuna wazee miaka 65 au zaidi bado ni wakulima wa jembe la mkono. Hawawezi kung'atuka kwani hawana pensheni.

Sasa katika umri huo, mzee anachohitaji sio mahindi ya ugali tu, bali sukari ya chai na hata fedha za kinywaji. Wenyewe hudai wakijaribu kunywa maji ya bomba huwa hayapiti kabisa.

Wakulima huwa wanaishiwa sana. Sasa akilima mahindi yakifika wakati wa kuliwa mabichi, huamua auze kiasi ili apate fedha za sukari, kwani hajanywa chai miezi, na koo limekauka kabisa. Fikiria anavyoudhika kunapotokea kijana mdogo, DC ambaye amejua kutoa kamasi mwenyewe juzi tu, anamwambia "Huna ruhusa kuuza mahinda mabichi"! Kwani ni mahindi ya serikali?

Sasa mahindi yakivunwa, wakulima hula mengine, kiasi huuza kupata fedha, na mengine hutengenezea viburuduisho kama kimpumu na kiamble. Sasa ka DC tena kanakuja na vimgambo vyake kanasema hakuna ruhusa kutengenezea mahindi kinywaji. Ni mahindi ya serikali? Kwani wakulima ni watoto wadogo wasiojua wanachohitaji ni nini? Serikali inawadhalilisha wakulima kwa hatua hizi za uonevu. Ni lini wakulima wa Tanzania watapata UHURU?

Mkulima ana haki ya kulima zao lolote analotaka (mradi lisiwe kitu kama zao la bhangi amabalo limekatazwa na Bunge), kuuza mazao yake wakati wowote anaopenda na kwa yoyote amtakaye, na kutumia yaliyobaki kwa namna yoyote anayopenda, ikiwa ni pamoja na kuyanywa pombe kama akijisikia kufanya hivyo. Ni yake, ana uhuru nayo.

Serikali iache kuwakandamiza wakulima kwa kuwanyima uhuru wao wa kisheria wa kujiamulia mambo yao wenyewe. Ma DC waache tabia chafu ya kutunga na kutekeleza sheria zao wenyewe, na sheria yoyote itungwayo na serikali za mitaa isipingane na uhuru wa msingi wa kila mtu, ambao uko kwenye katiba.

Augustine Moshi
 
Serikali Iache Kudhalilish Wakulima.

Wakulima wadogo wanapata taabu sana. Kuna wazee miaka 65 au zaidi bado ni wakulima wa jembe la mkono. Hawawezi kung'atuka kwani hawana pensheni.

Sasa katika umri huo, mzee anachohitaji sio mahindi ya ugali tu, bali sukari ya chai na hata fedha za kinywaji. Wenyewe hudai wakijaribu kunywa maji ya bomba huwa hayapiti kabisa.

Wakulima huwa wanaishiwa sana. Sasa akilima mahindi yakifika wakati wa kuliwa mabichi, huamua auze kiasi ili apate fedha za sukari, kwani hajanywa chai miezi, na koo limekauka kabisa. Fikiria anavyoudhika kunapotokea kijana mdogo, DC ambaye amejua kutoa kamasi mwenyewe juzi tu, anamwambia "Huna ruhusa kuuza mahinda mabichi"! Kwani ni mahindi ya serikali?

Sasa mahindi yakivunwa, wakulima hula mengine, kiasi huuza kupata fedha, na mengine hutengenezea viburuduisho kama kimpumu na kiamble. Sasa ka DC tena kanakuja na vimgambo vyake kanasema hakuna ruhusa kutengenezea mahindi kinywaji. Ni mahindi ya serikali? Kwani wakulima ni watoto wadogo wasiojua wanachohitaji ni nini? Serikali inawadhalilisha wakulima kwa hatua hizi za uonevu. Ni lini wakulima wa Tanzania watapata UHURU?

Mkulima ana haki ya kulima zao lolote analotaka (mradi lisiwe kitu kama zao la bhangi amabalo limekatazwa na Bunge), kuuza mazao yake wakati wowote anaopenda na kwa yoyote amtakaye, na kutumia yaliyobaki kwa namna yoyote anayopenda, ikiwa ni pamoja na kuyanywa pombe kama akijisikia kufanya hivyo. Ni yake, ana uhuru nayo.

Serikali iache kuwakandamiza wakulima kwa kuwanyima uhuru wao wa kisheria wa kujiamulia mambo yao wenyewe. Ma DC waache tabia chafu ya kutunga na kutekeleza sheria zao wenyewe, na sheria yoyote itungwayo na serikali za mitaa isipingane na uhuru wa msingi wa kila mtu, ambao uko kwenye katiba.

Augustine Moshi
 
Back
Top Bottom