Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,794
Hii kwanza ni kashfa kubwa kwake kwa chama cha ngumi Tanzania, wadau ndugu jamaa na marafiki.... Kwamba kazi yake rasmi sasa sio mchezo wa ngumi tena au ngumi mateke bali ameajiriwa kutesa na pengine kuua kabisa...
Akiwa ni kijana aliyependa sans mchezo wa kickboxing alifikia kilele cha mafanikio wakati wa kipindi cha Kikwete (rais)... Akiitangaza vema nchi yake kwa mialiko ya mapambano nje ya nchi... Ana mataji ya ushindi mengi tuu
Kipindi hicho hamasa ya michezo ilikuwa juu na vipaji vingi viliibuliwa... Kaseba alikuja kumalizia kipaji chake kwa kuacha kickboxing na kuingia kwenye ngumi za ridhaa kisha akapotea kwenye ramani ya michezo
Kuna video na mada hapa JF, ya mtu anayetuhumu kudhulumiwa mali zake na kutishiwa kuuliwa huku akiwahi kutekwa Beach na kupelekwa kuteswa kwenye nyumba moja huku mtesaji mkuu akiwa ni bondia Japhet kaseba
Kama hili ni kweli na kwa mafanikio aliyopata Kaseba enzi zake leo hii hakupaswa afanye kazi anayotuhumiwa kuifanya.. Kwa nafasi yake alitakiwa awe na uwekezaji fulani kwenye tasnia ya michezo.... Lakini maisha ya mastaa wa kiafrika yanatia simanzi sana....
Kaseba ni mfano wa wanamichezo wengi waliowatajirisha wengine huku wao wakiishia kufanya kazi chafu na kufa fukara....
Kila mtu anatamani kuishi maisha fulani na ku keep status... Lakini ikifika mahali hupati unachotaka kwa njia halali basi hujikuta mtu anajilipua na kufanya kazi yoyote alimradi tu anapata anachotaka
Je tuna wana michezo wangapi leo hii ambao hawajulikani walipo na shughuli wanazofanya? Kuna mambo muhimu kama taifa tumeyapa kisogo na kuamua kuifanya siasa ndio kila kitu....
Tuhuma hizi za Kaseba ni DOA kubwa kwa wanamichezo wetu lakini je... Baada ya hili ninini hatima yake!?
Habari zaidi, soma=>Maovu ya GSM yaanikwa: Wahusishwa na watu wasiojulikana, Makonda aonywa kuwa karibu nao