Japhet Justine, Mkurugenzi mkuu wa benki mdogo kuwahi kutokea Tanzania!

Mikopo Chefuchefu

JF-Expert Member
May 15, 2017
3,373
6,756
Japhet Justine kwa mara nyingine tena amevunja rekodi za nchi hii baada ya kuteuliwa kuwa mkurugenzi mkuu wa benki ya wanawake (TWB)...

Kiumri, ni kijana mdogo kabisa ( his age is around 34 yrs) kuwahi kushika cheo cha juu kama hicho katika sekta ya benki hapa nchini.

Ni kijana mdogo kiumri ila kichwani yuko very very smart...

Alimaliza shahada yake ya Bcom pale UDSM mwaka 2008, baadaye akafanya kazi ya uhasibu British council kabla ya kuhamia benki ya NMB. Huko nako alifanya vyema mpaka akapanda cheo na kufikia hatua ya kuongoza idara kubwa ya benki hiyo ya NMB.

Baada ya hapo pia alifanya kazi na benki ya ABC katika cheo kikubwa kabisa akiongoza kanda ya Mara....

Taarifa zinaonesha kuwa amepata pia mafunzo kwa ngazi ya masters nchini Afrika kusini.

justine.jpg
Justine 2.jpg


Kabla ya Justine kuvunja rekodi hii, taarifa (nilizonazo) zinaonesha kuwa Patrik Schoeneborn ndiye alikuwa mkurugenzi mkuu mdogo kuliko wote hapa nchini, akiwa ni raia wa Ujerumani na mkurugenzi mkuu wa benki ya Access kabla ya kurudishwa kwao Ujerumani kushika nyadhifa za juu kwenye group!


Patric Schoeneborn.jpg



Tunamtakia utendaji mwema kijana mwenzetu Justine katika kuingoza benki ya wanawake!
 
miaka 34 ceo mshahara milion 15... samatta miaka 20 tp mazembe mshahara milion 20.. na baadae genk mshahara kwa wiki hatari..

hasheem miaka 20 nba mshahara milion 200...

diamond miaka 28 utajiri wa bilion...

kweli shule zinachelewesha maisha.. miaka 34 eti ni mdogo wakati umri wa kustaafu huo akifika samatta
 
miaka 34 ceo mshahara milion 15... samatta miaka 20 tp mazembe mshahara milion 20.. na baadae genk mshahara kwa wiki hatari..

hasheem miaka 20 nba mshahara milion 200...

diamond miaka 28 utakiri wa bilion...

kweli shule zinachelewesha maisha.. miaka 34 eti ni mdogo wakati umri wa kustaafu huo akifika samatta
Mimi mwenyewe nashangaa miaka 34, huyo si mzee kabisa, mimi nikajua miaka 24 hivi
 
miaka 34 ceo mshahara milion 15... samatta miaka 20 tp mazembe mshahara milion 20.. na baadae genk mshahara kwa wiki hatari..

hasheem miaka 20 nba mshahara milion 200...

diamond miaka 28 utakiri wa bilion...

kweli shule zinachelewesha maisha.. miaka 34 eti ni mdogo wakati umri wa kustaafu huo akifika samatta
Kwahiyo ulikuwa unashauri wamchukue Samata ndio awe mkurugenzi?
 
Tuongelee mafanikio yake kazini, sio sifa za kuteleza tu. Hiyo benki iko hoi, mtuambie jambo la ubunifu alilolifanya ili kuibadilisha.
 
Back
Top Bottom