January Makamba, uliteuliwa ili usimamie ukatwaji wa umeme?

DENLSON

JF-Expert Member
Apr 28, 2013
944
1,253
Ni ajabu sana kwamba kwa miaka 5 hatuwahi kuwa na tatizo la umeme kukatika mara kwa mara kama ilivyo sasa. Wote tunajua umeme ulikuwa ukikatika lakini sio kwa kasi hii iliyopo sasa hasa baada ya uteuzi wa January Makamba kama Waziri wa Nishati.

Uteuzi wako ulifuatiwa na uamuzi wa wewe kuvunja bodi ya Tanesco kisha kuingia mkataba wa bilioni 63 za kitanzania kwa madai ya kuboresha mfumo, mfumo ambao wewe hukuwahi kujua mapungufu yake wala uimara wake ila ghafla ndani ya mwezi mmoja tu tokea uingie ofisini unavunja bodi na kuingia mkataba wa mabilioni ya shilingi na kibaya zaidi hatua hizo zilifuatiwa na ukatikaji wa umeme nchi nzima.

Tanesco wakatoka na kauli kwamba hakuna mgao bali ni magengenezo ya kawaida, Waziri ukasema ni kwa wiki mbili tu leo ni zaidi ya miezi mitatu umeme haumalizi siku bila kukata, Je Mh January uliteuliwa ili ukasimamie zoezi la ukataji wa umeme?
 
January kaletwa hapo na Samia ili watengeneze njia ya kuleta uwekezaji wa kipigaji na ndiyo kinachofanyika angalia Viongozi na watendaji wote wabobezi wa hiyo fani tokea bodi mkurugenzi na waziri wote ni wabobezi some with geniune PhDs wameondolewa na Samia bila sababu ni kupisha njia ya uupigaj

Kipindi cha JPM umeme ukikatika kwa masaa mawili mtu anatumbuliwa either na rais au waziri mkasema JPM ni dikteta,, hakukuwa na mgao wala kukatika kwa zaidi ya masaa mawili Utendaji kazi na Uwizi na Upigaji wa mtz unahitaji kiongozi makini kama the late JPM

Vumilieni ila wa kumlaumu ni Samia na wanaomshauri leo mnagaragazwa na porojo za umeme na uwekezaji wake huko Rufiji mkilala gizani,, toeni wahuni hao.

Kama raisi ni Samia na waziri wa nishati ni January Makamba basi mmepigwa za uso
 
Sijui ni jambo gani huwa anamwambia mkuu naye anamuamini

Maana umeme unakatika kila mara na mkuu haonekani kuguswa kabisa na hali hii.
Mkuu hawezi kuguswa kwani anaona kazi ya kuwafanya wananchi wahitaji uwekezaji kwenye umeme ikubalike

Tunataki raisi mwanamke lkn siyo Samia jamani huyu siyo mnyamwezi hana utz in her bottom floor of heart
 
Kuhusu suala la umeme nilishakata shauri sitakaa niiamini Serikali ya CCM katika hilo, nadhani hilo eneo lina mazingira fulani ya upigaji ambao kila anayekaa hapo anasahau kilichompeleka.
Nadhani kuajiriwa Tanesco is akin to buying someone kilevi cha bure; ni mwendo wa kulewa na kuzidi kulewa. Unaambiwa mizizi ya sakata la umeme, root cilia zake ziko London & Washington.
 
Back
Top Bottom