January Makamba, Tanesco Hakuna nguzo wala meta kwa wateja wapya nchi nzima , habari hizi unazo?

Ilitakiwa kuunganishiwa umeme iwe bure kabisa,why nilipie Meter,nguzo? Mimi nataka huduma hata ukiniletewa Umeme kwa wireless ni sawa,kama hauwezi una niletea kwa nguzo basi gharama ilitakiwa agharamikie TANESCO na si mteja....Unaweka meter kwa ajili ya kumanage mapato yako sasa inakuwaje gharama ya meter ije kwangu wakati ni kwa faida ya tanesco?
 
Kwa masikitiko makubwa sana Tanesco nchi nzima hakuna nguzo wala mita kwa wateja wapya. Tatizo ni nini?

Cha kushangaza na kufurahisha mteja mpya akishapimiwa umeme kama line yake inahitaji nguzo mteja haruhusiwi kulipia wala hapewi control number.

Kalemani alikuwa anapata wapi nguzo na mita? Mameneja wa Tanesco mikoa na wilaya nchi nzima wamepigwa marufuku kutoa namba za kulipia line mpya inayohitaji nguzo.

Je, hali hii itaendelea hadi lini? Makamba watanzania wanakuangalia na wanajuta awamu sita inakoelekea na umezidisha maneno kuliko matendo.

Toa taarifa kwa vyombo vya umma na vyombo vya habari kuelezea hali halisi ya Tanesco na ni nini wateja wapya wanachotakiwa kufanya au wasubiri hadi lini wawese kulipia umeme.
Hiyo nafasi ni nzito sana kwake sidhani kama anaiweza na kuimudi hata kidogo....
 
Alikuwa muongo sana,huu ndio ukweli.
Sasa tunakutana na ukweli ule ukweli unatuumiza mpaka kichefu chefu. Siasa za kudanganyika wanyongwaji hazipo tena.

Ukiangalia ni kama vile Sukuma gang, limeumia sana, Ma-rope kuwa waziri, lazima kitendo cha kutolewa yule mchato uwaziri wa Nishati kimewatingisha.

Everyday is Saturday................................:cool:
 
Ukiangalia ni kama vile Sukuma gang, limeumia sana, Ma-rope kuwa waziri, lazima kitendo cha kutolewa yule mchato uwaziri wa Nishati kimewatingish
Kweni Msambaa kuwa Waziri kuna shida gani?

Hii Tanzania ni yetu sote, January aangalie watu wanaohujumu Shirika la Ugavi, awape onyo au ikibidi warudishe Kitaa wawe Machinga.
 
Sasa tunakutana na ukweli ule ukweli unatuumiza mpaka kichefu chefu. Siasa za kudanganyika wanyongwaji hazipo tena.

Ukiangalia ni kama vile Sukuma gang, limeumia sana, Ma-rope kuwa waziri, lazima kitendo cha kutolewa yule mchato uwaziri wa Nishati kimewatingisha.

Everyday is Saturday................................:cool:
Acheni Ukabila Nchi ilisha washinda
Mmepewa Kitonga chakutawala na Uwezo ni mdogo
 
Kiuhalisia hii Wizara imezamishwa na Kalemani, alipolazimisha gharama ya kuunganisha umeme tzs 27,000/- wakati akijua fika gharama za vifaa husika ni zaidi ya tzs 150,000/- Hii ilikuwa hujuma kwa shirika LA Tanesco na kama yasemwayo ni kweli nilitegemea lazima iwe hivyo
Wewe unaongea kama afisa wa tanesco. Sisi walalahoi tulimuelewa Kalemani.
 
Huyu jamaa anafanya kazi gani? aliyepita mbona aliunganisha umeme maelfu ya vijiji kwa bei karibu na bure bila malalamiko yeyote na umeme ulikuwa haukatiki ovyo kama kwa huyu jamaa, leo ni story tuu za management science na wabia wanaolipwa mabilioni kwa umeme usioonekana, sometimes ni rahisi sana kumjua msanii maana umeme hakuna tunalishwa story tuu na lawama kibao za awamu iliyopita, naanza kuamini huyu jamaa ni zero
 
Kweni Msambaa kuwa Waziri kuna shida gani?

Hii Tanzania ni yetu sote, January aangalie watu wanaohujumu Shirika la Ugavi, awape onyo au ikibidi warudishe Kitaa wawe Machinga.
Aangalie wapi, mhujumu ni yeye mwenyewe, tumechoka na excuses za kipuuzi
 
Kiuhalisia hii Wizara imezamishwa na Kalemani, alipolazimisha gharama ya kuunganisha umeme tzs 27,000/- wakati akijua fika gharama za vifaa husika ni zaidi ya tzs 150,000/- Hii ilikuwa hujuma kwa shirika LA Tanesco na kama yasemwayo ni kweli nilitegemea lazima iwe hivyo
Kiuhalisia kuunganishiwa umeme iwe bure kabisa kwasababu unalipia huduma na tozo kibao kila ukinunua token
 
Kiuhalisia hii Wizara imezamishwa na Kalemani, alipolazimisha gharama ya kuunganisha umeme tzs 27,000/- wakati akijua fika gharama za vifaa husika ni zaidi ya tzs 150,000/-

Hii ilikuwa hujuma kwa shirika LA Tanesco na kama yasemwayo ni kweli nilitegemea lazima iwe hivyo
Je unajuwa Tanesco wanaigiza Trilioni kwa Mwaka, kuwapa wateja kuuganishwa umeme kwa Tsh 27,000 ni sawa na Coca Cola kutoa bure fridge ili vinjwaji viuzwe.
 
Kiuhalisia hii Wizara imezamishwa na Kalemani, alipolazimisha gharama ya kuunganisha umeme tzs 27,000/- wakati akijua fika gharama za vifaa husika ni zaidi ya tzs 150,000/-

Hii ilikuwa hujuma kwa shirika LA Tanesco na kama yasemwayo ni kweli nilitegemea lazima iwe hivyo
Bhangi,hazijawahi kumwacha mtu salama,pole sana kwa matatizo hayo,
 
Back
Top Bottom