January Makamba, shughulikia suala la umeme kukatikakatika ovyo, hili ni tatizo

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,489
51,070
Sasa hivi TANESCO wanakata umeme, hawatoi taarifa, biashara na shughuli zetu zinasimama. Huu ujinga utaisha lini nchi hii?

Mmeturushia zigo la sisi watumiaji umeme kulipa kodi ya majengo, halafu mnatuambia sisi tumalizane na wenye nyumba HALAFU bado hata umeme huo mnaukatakata. Hivi nyie mnajitambua kweli, mnajielewa? - Mnatutia hasira sana aisee

Tunajua wanasiasa mna majumba ya kupangisha kedekede, kwa hiyo mnanufaika kwa kodi kulipwa na mpangaji kuliko nyie ndo maana hata bungeni hamkupambana kumtetea mpangaji kwa sababu hii sheria inawalinda matajiri na kumuumiza masikini! , maana kwa mijumba yenu mingi mnayomiliki kwa mwaka mnatakiwa kulipa hela ndefu.

Mimi naamini kama kweli mkitaka Mwenye nyumba alipe mnaweza maana mna uwezo wa kujua namba za simu za wenye nyumba, mnaweza kuwakata wao direct kupitia miamala wanayofanya au mnaweza kujua benki account zao na mkawakata kwenye miamala yao badala ya kuja kutukata sisi Wapangaji.

Yaani mgekuwa na lengo la kumlinda mpangaji mngeweza kuweka hata sheria ya kumlinda mpangaji lakini hamjafanya hivyo.

Waziri tunataka umeme wa uhakika, haya mambo ya kukatikakatika yanakera sana.
 
Hajaenda huko kwa sababu hiyo, huyo yupo huko kwa ajili ya gesi tu. Zingine mbwembwe tu
 
Ivi kuunganishia umeme kwa buku 27 ilikuwa kweli au kiini macho CCM walikuwa wanatupiga. Emu aanzie hapo. Ujue mabeberu walishasema TANZAGIZA kusambaza umeme nchi nzima labda mpaka 2060 JPM akakataa kumbe walikuwa real wale mabeberu asee
 
Sasa hivi TANESCO wanakata umeme, hawatoi taarifa, biashara na shughuli zetu zinasimama. Huu ujinga utaisha lini nchi hii?

Mmeturushia zigo la sisi watumiaji umeme kulipa kodi ya majengo, halafu mnatuambia sisi tumalizane na wenye nyumba HALAFU bado hata umeme huo mnaukatakata. Hivi nyie mnajitambua kweli, mnajielewa? - Mnatutia hasira sana aisee

Tunajua wanasiasa mna majumba ya kupangisha kedekede, kwa hiyo mnanufaika kwa kodi kulipwa na mpangaji kuliko nyie ndo maana hata bungeni hamkupambana kumtetea mpangaji kwa sababu hii sheria inawalinda matajiri na kumuumiza masikini! , maana kwa mijumba yenu mingi mnayomiliki kwa mwaka mnatakiwa kulipa hela ndefu.

Mimi naamini kama kweli mkitaka Mwenye nyumba alipe mnaweza maana mna uwezo wa kujua namba za simu za wenye nyumba, mnaweza kuwakata wao direct kupitia miamala wanayofanya au mnaweza kujua benki account zao na mkawakata kwenye miamala yao badala ya kuja kutukata sisi Wapangaji.

Yaani mgekuwa na lengo la kumlinda mpangaji mngeweza kuweka hata sheria ya kumlinda mpangaji lakini hamjafanya hivyo.

Waziri tunataka umeme wa uhakika, haya mambo ya kukatikakatika yanakera sana.
Kuna jambo gumu,sio Covid-19, bali kale kangojwa kengine,kanaharibu thinking and implementing capacities.
 
Tunataka mkataba Kati ya Tanesco na Aggeco wa kuzalisha umeme kwa njia ya majenereta ufufliwe. Ili tuagize mafuta, tule cha juu.

Kama hili halitafanyiwa kazi tutaendelea kukatakata umeme. Na wakizingua tunaenda kuharibu mitambo ya umeme wa maji kule Mtera na bwawa la Nyerere.
 
Back
Top Bottom