January Makamba ni lini utaanza kufanya ziara kukagua usambazwaji wa umeme?

Kiturilo

JF-Expert Member
Sep 27, 2021
709
2,858
Ni miezi kadhaa sasa imepita tangu waziri mpya wa nishati bwana January Makamba ateuliwe na rais Samia Suluhu kushika nafasi hiyo.

Waziri Makamba tangu ateuliwe amefanya ziara Kigoma tu tena mjini mjini baada ya kupewa maagizo na makamu wa rais afike huko kutatua kero ya kukatika katika umeme.

Baada ya hapo tunamuona waziri Makamba akiwa anajipositi akifanya vikao na wazungu kwenye hoteli kubwa kubwa mara tunasikia anafanya ziara Saudi Arabia kuonana na waziri wa nishati wa nchi hiyo!

Hoja yangu ya kwanza ni kwamba kwenye miradi ya REA vimebaki vijiji elfu 2 tu kuunganishiwa umeme, je kwa hali hii ya waziri kuonekana kwenye mahoteli ya kifahari tu vijiji hivi 2000 vitaisha kupelekewa umeme hadi kufikia mwaka 2025 kama ilani ya uchaguzi inavyotaka?

Hoja yangu ya pili ni kwamba maeneo yanayokatika katika umeme siyo Kigoma tu ulipoelekezwa na mh Makamu wa rais ukafanya ziara, tatizo hili ni kila mahali nchini umeme unakatika kwa sasa je ni lini utaanza kufanya ziara vijijini kuunganisha umeme na kuangalia matumizi ya kodi za watanzania kama zinatumika kwa usahihi?

Ina maana mtu wa kubaini ubadilifu aliyebaki ni waziri mkuu pekee bwana Kassim Majaliwa?
 
Bado anajipanga kukusanya pesa na ahadi toka huko nchi za imarati za kumsaidia kuingia ikulu 2030. huyu jamaa sijui nani aliemleta kwenye siasa na uongozi,.He is a waste of Oxygen.!!
jimboni kwake kumechokaaa...Mbowe Sio Gaidi!!!
 
Bado anajipanga kukusanya pesa na ahadi toka huko nchi za imarati za kumsaidia kuingia ikulu 2030. huyu jamaa sijui nani aliemleta kwenye siasa na uongozi,.He is a waste of Oxygen.!!
jimboni kwake kumechokaaa...Mbowe Sio Gaidi!!!
 
Hivi huyu amefikaje hapo? Unatoa mtu wa maana unatuletea mzurulaji kama JK! Yaani eti anasema ninatoa wazembe, yaani Kalemani umlinganishe na huyu Makamba mzurulaji? Yaani kweli hili Mama Samia umechemka! Saizi anapost mara hupo Saudia badala ya kufatilia upotevu wa umeme na kuboresha usimamizi wa Bwawa na umeme la mwl nyerere! Yaani kwa akili ya mama Makamba anaweza kuingia mkataba wa kizalendo? Kwa kweli nchi hii anajua Mungu!
 
Jamaa anajipanga na mikakati ya mbele huko kuja kuchukua nchi, ameipata nafasi acha aitumie..

Na huko aliko haieleweki ni ziara za kiserikali ama zake binafsi.

Maana utasikia nimekutana/nimealikwa na Rafiki yangu...sasa unajiuliza mambo ya serikali na Urafiki wake wapi na wapi..

Sijui kwa nini amepewa wizara nyeti kama hiyo ambayo ndio uti wa mgongo wa Taifa.
 
Jamaa anajipanga na mikakati ya mbele huko kuja kuchukua nchi, ameipata nafasi acha aitumie..

Na huko aliko haieleweki ni ziara za kiserikali ama zake binafsi.

Maana utasikia nimekutana/nimealikwa na Rafiki yangu...sasa unajiuliza mambo ya serikali na Urafiki wake wapi na wapi..

Sijui kwa nini amepewa wizara nyeti kama hiyo ambayo ndio uti wa mgongo wa Taifa.
Inasikitisha sana mkuu
 
Hivi huyu amefikaje hapo? Unatoa mtu wa maana unatuletea mzurulaji kama JK! Yaani eti anasema ninatoa wazembe, yaani Kalemani umlinganishe na huyu Makamba mzurulaji? Yaani kweli hili Mama Samia umechemka! Saizi anapost mara hupo Saudia badala ya kufatilia upotevu wa umeme na kuboresha usimamizi wa Bwawa na umeme la mwl nyerere! Yaani kwa akili ya mama Makamba anaweza kuingia mkataba wa kizalendo? Kwa kweli nchi hii anajua Mungu!
Kalemani muda huu angekuwa vijijini huko anafunga umeme wa REA kwenye nyumba za nyasi
 
Kama huku Morogoro, yaani mgao wa umeme daily daaah
yes, umeme unakatika daily, ndo maana tulimshangaa kwenye spichi yake ya kwanza akaongelea pipe dreams za kuuza umeme ng'ambo... hujaweza ku electrify nchi yako unaongelea export ya umeme.... are you high?

na alisema umeme ukikatika hataki kuitwa yeye, matatizo ya umeme TANESCO na wateja wamalizane juu kwa juu... sasa kwenye crisis za umeme wananchi wamlilie waziri gani, wa Kilimo ?

Makamba is not up to the job of energy minister.
 
Kama nakumbuka vizuri vipaumbele vya mama katika nishati alisema ni gesi na mafuta….sasa sioni ajabu Waziri wa Nishati wa TZ kukutana na Waziri wa Nishati wa Saudia nchi iliyopiga hatua katika mafuta na gesi...Nadhani ni katika kubadilishana uzoefu.

Miradi ya umeme sawa ipo lakini inakwenda maana tayari ipo katika pipeline/utekelezaji….Ishu nzito zipo katika mafuta na gesi huko baharini kwenye vitalu na exploration.Mtizamo
 
Kama nakumbuka vizuri vipaumbele vya mama katika nishati alisema ni gesi na mafuta….sasa sioni ajabu Waziri wa Nishati wa TZ kukutana na Waziri wa Nishati wa Saudia nchi iliyopiga hatua katika mafuta na gesi...Nadhani ni katika kubadilishana uzoefu.

Miradi ya umeme sawa ipo lakini inakwenda maana tayari ipo katika pipeline/utekelezaji….Ishu nzito zipo katika mafuta na gesi huko baharini kwenye vitalu na exploration.Mtizamo
Kwani huko hakuna balozi wa kushughulikia hilo kwanza kabla ya yeye kwenda?? huyu deal lake ni la pesa anapenda sana kuomba omba, kaenda huko kuorganise pesa za 2030 ....tukiwa wazima utakuja uone. Huyu aliomba pesa 2015 kwa waitaliano hadi Mange akamuumbua ..hili jamaa yaani kwenye uongozi ni zero.Mama kachemka hapo ila sio kosa lake nchi iko chini ya mkwere.
 
Kwani huko hakuna balozi wa kushughulikia hilo kwanza kabla ya yeye kwenda?? huyu deal lake ni la pesa anapenda sana kuomba omba, kaenda huko kuorganise pesa za 2030 ....tukiwa wazima utakuja uone. Huyu aliomba pesa 2015 kwa waitaliano hadi Mange akamuumbua ..hili jamaa yaani kwenye uongozi ni zero.Mama kachemka hapo ila sio kosa lake nchi iko chini ya mkwere.
Taifa tajiri halihitaji kiongozi ombaomba
 
Yupo anafanya makubwa anasahau hata haya madogo na basics ya kuhakikisha umeme wa uhakika hata kwa wale waliounganishwa....

Kuunganishwa is one thing kupata kile ambacho inabidi upate (umeme na sio mgao) is quite another

In short mpaka sasa he is under-performing (according to matokeo) ingawa yeye anasema neema inakuja...
 
Back
Top Bottom