Saint Ivuga
JF-Expert Member
- Aug 21, 2008
- 54,363
- 58,385
Makamba amkingia kifua Waziri Ngeleja | Send to a friend |
Monday, 27 June 2011 20:45 |
0digg Kizitto Noya, Dodoma MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Nishati na Madini, Januari Makamba, amesema siyo sahihi kumlaumu Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja na Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco), kwa tatizo la umeme nchini. Akizungumza mjini hapa jana, Makamba alisema sekta ya umeme nchini imepita vipindi vitatu tofauti; kabla ya miaka ya 90 na baada kuanzia mwaka 1996 hadi mwaka 2000, hivyo suala hilo limekuwa na historia. Kimsingi siyo sahihi kumlaumu waziri wala Tanesco yenyewe, matatizo hayo yalikuwapo na waziri ameyakuta. Cha msingi kama Taifa, tushikamane na tuone tatizo hilo kama janga na tuungane kupambana nalo, alisema Makamba. Akifafanua historia hiyo, Makamba alisema uendelezaji umeme nchini kabla ya mwaka 1996, Tanesco ilikuwa ikijiendesha kwa ufanisi mkubwa ikiwa inamilikiwa na serikali kwa asilimia zote. Kipindi kilichofuata ni mwaka 1997 hadi 2006, Tanesco iliwekwa katika orodha ya mashirika yanayotakiwa kubinafsishwa, lakini hakuna hatua iliyochukulia hadi mwaka 2006 uamuzi huo ulipobatilishwa, alisema Makamba na kuongeza: Wakati wote huo ikisubiri kubinafsishwa, hakuna uwekezaji uliofanyika katika shirika hilo wakati uchumi wa taifa ulikuwa unaendelea kukua kwa kasi kubwa kufikia kiwango cha asilimia saba na mahitaji ya umeme, yakiongezeka maradufu. Kwa mujibu wa Makamba, baadhi ya miradi iliyotokana na uwekezaji mkubwa ni migodi ya madini na kampuni za simu, lakini wakati huohuo taifa lilikumbwa na ukame katika vyanzo vyake vya kuzalisha umeme wa maji, ikiwamo Mtera na Kidatu na taifa likaingia gizani. Alisema mipango mingi iliyobuniwa ianze kutekelezwa 2008 ambayo ilitarajiwa itakapokamilika ingezalisha megawati 645, hadi sasa ni miwili ndiyo imefankiwa; Ubungo (Megawati 100) na Tegeta (Megawati 45). unatarajiwa kukamilishwa na mkopo kutoka China wa dola 400 milioni za Marekani. Uwezo wa kitaifa hivi sasa wa kuzalisha umeme kama vyanzo vyote vya kuzalisha umeme vitafanya kazi ni megwati 1,100, ambacho Makamba alisema hakitoshi wateja wanaokadiriwa kufikia milioni sasa. Kwa mujibu wa Makamba, tatizo la umeme litakwisha iwapo serikali itaweka juhudi za makusudi kuwekeza katika uzalishaji umeme na kuweka kando tofauti za kisiasa. Alisema, iwapo juhudi zitafanyika haraka za kufanya uwekezaji mkubwa katika uzalishaji wa umeme kitaifa, kwa kutumia vyanzo vingine mbali na maji yanayozalisha asilimia 55 ya umeme wote nchini, taifa litaondokana na uhaba wa umeme. |