nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
08 OCTOBER 2012
Na Yusuph Mussa, Korogwe
MJUMBE wa Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. January Makamba, amesema chama hicho hakiwezi kuanguka katika Uchaguzi Mkuu 2015 na wanaosema kimefikia ukingoni kuongoza dola wamepotea.
Bw. Kamanda aliyasema hayo jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkoa wa Tanga uliofanyika katika ukumbi wa Mamba Club mjini Korogwe.
"Kuna maneno yanasemwa mitaani kwa bahati mbaya hata baadhi ya wana CCM wenzetu wanaogopa na wanayaamini kuwa ya kweli lakini mimi nimekuja kama mjumbe, nataka kuwapa siri ya Kamati Kuu, kamwe CCM haiwezi kuachia dola mwaka 2015.
"Hali ya unyonge kuwa tutashindwa mwaka 2015 imepandikizwa, wapo wanaosema CCM inakimbiwa na vijana lakini ukiangalia mkutano huu hakuna chama kinachoweza kuwakusanya vijana kama hivi zaidi yetu," alisema.
Alisema moja ya mikakati ya kuifanya CCM isiondolewe madarakani ni vijana kuisemea mahali popote ambapo vyama vya upinzani vinaonekana kuungwa mkono na vijana kwasababu ya mikutano mingi waliyoifanya.
Naye Bw. Yusuph Makamba aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, alitumia fursa hiyo kutangaza kujiuzulu nafasi ya Kamanda wa UVCCM, mkoani hapa na kutaka uchaguzi huo utumike kuwaweka viongozi wenye mvuto ili chama hicho kiweze kuibuka na ushindi mnono katika Uchaguzi Mkuu 2015.
"Ili mchezaji aonekana mzuri lazima awe na pumzi ya kucheza dakika 90, lakini kama hana uwezo huo msimpe nafasi hiyo na kama anacheza lakini anaonekana kuchoka, lazima apumzishwe na kupewa nafasi yake mtu mwingine," alisema Bw. Kamamba.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoani hapa ambaye alimaliza muda wake, Bw. Rodgers Shemwelekwa, aliwataka vijana waache kuchagua wagombea wanaotoa rushwa ili wachaguliwe.
"Msikubali kupewa fedha na wagombea ili wawatumie kama ngazi ya kupata madaraka ya uongozi," alisema.
Na Omari Mngindo, Bagamoyo
WANAMICHEZO watatu wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wamefanikiwa kuchaguliwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani hapa.
Wanamichezo hao ni John Bolizozo Katibu anayemaliza muda wake wa uongozi ndani ya Chama Cha Mpira wa Miguu wilayani hapa (BFA), Mousin Bharwan mlezi wa timu zinazotoka ndani ya kijiji cha Vigwaza na Yussuf Kikwete mdau wa michezo Bagamoyo mjini.
Katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo Cha Sanaa na kusimamiwa na Mbunge wa Jimbo la Kibiti Abdul Marombwa, pia ulishuhudiwa na Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa na Katibu wa (CCM), Joyce Massi ambapo Bolizozo ameshinda nafasi ya Uenezi akiwaacha wapinzani wake Emmanuel Panduka na Kassim Gogo.
Bharwan ameibuka kidedea nafasi ya Mkutano Mkuu Taifa ambaye ameshinda nafasi hiyo kwa kujinyakulia kura 753 na kuwaongoza wenzake wanne ambao ni Shumina Sharif, Yussuf Kikwete, Aeshi Khatibu na Issa Kibwana nao wamechaguliwa nafasi hiyo iliwaniwa na wagombea 15.
Wakizungumza baada ya matokeo hayo, Bharwan alianza kwa kuwashukuru wajumbe wa Mkutano huo kwa kuweza kumchagua na kwamba atatumia nafasi hiyo kuhamasisha michezo ikiwa ni kutekeleza ilani ya chama hicho.
"Katika Ilani ya chama chetu inagusia michezo, nitatumia nafasi hii kuhamasisha michezo mbalimbali ndani ya wilaya yetu kwa kuwapatia vijana fursa ya kimichezo kwani utakumbuka kuwa michezo kwa sasa ina nafasi kubwa ya ajira," alisema Bharwan.
Naye Bolizozo alisema baada ya mafanikio makubwa yaliyopatikana ndani ya BFA akiwa Katibu atageuzia makali hayo katika nafasi ya Uenezi ili kuhakikisha vijana wanapata nafasi nzuri ya kushiriki michezo sanjali na kuhamasisha kujiunga na chama hicho.
"Nitatumia nafasi hii kuchagiza uendelezwaji wa michezo ndani ya Wilaya ikiwa ni kuunga mkono ilani ya CCM inayotaka kuendelezwa kwa michezo kwa wananchi bila kubagua itikadi za kisiasa," alisema Bolizozo.
Na Yusuph Mussa, Korogwe
MJUMBE wa Kamati Kuu (CC) ya Halmashauri Kuu (NEC) ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Bw. January Makamba, amesema chama hicho hakiwezi kuanguka katika Uchaguzi Mkuu 2015 na wanaosema kimefikia ukingoni kuongoza dola wamepotea.
Bw. Kamanda aliyasema hayo jana wakati akifungua Mkutano Mkuu wa Uchaguzi wa Umoja wa Vijana (UVCCM), Mkoa wa Tanga uliofanyika katika ukumbi wa Mamba Club mjini Korogwe.
"Kuna maneno yanasemwa mitaani kwa bahati mbaya hata baadhi ya wana CCM wenzetu wanaogopa na wanayaamini kuwa ya kweli lakini mimi nimekuja kama mjumbe, nataka kuwapa siri ya Kamati Kuu, kamwe CCM haiwezi kuachia dola mwaka 2015.
"Hali ya unyonge kuwa tutashindwa mwaka 2015 imepandikizwa, wapo wanaosema CCM inakimbiwa na vijana lakini ukiangalia mkutano huu hakuna chama kinachoweza kuwakusanya vijana kama hivi zaidi yetu," alisema.
Alisema moja ya mikakati ya kuifanya CCM isiondolewe madarakani ni vijana kuisemea mahali popote ambapo vyama vya upinzani vinaonekana kuungwa mkono na vijana kwasababu ya mikutano mingi waliyoifanya.
Naye Bw. Yusuph Makamba aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, alitumia fursa hiyo kutangaza kujiuzulu nafasi ya Kamanda wa UVCCM, mkoani hapa na kutaka uchaguzi huo utumike kuwaweka viongozi wenye mvuto ili chama hicho kiweze kuibuka na ushindi mnono katika Uchaguzi Mkuu 2015.
"Ili mchezaji aonekana mzuri lazima awe na pumzi ya kucheza dakika 90, lakini kama hana uwezo huo msimpe nafasi hiyo na kama anacheza lakini anaonekana kuchoka, lazima apumzishwe na kupewa nafasi yake mtu mwingine," alisema Bw. Kamamba.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoani hapa ambaye alimaliza muda wake, Bw. Rodgers Shemwelekwa, aliwataka vijana waache kuchagua wagombea wanaotoa rushwa ili wachaguliwe.
"Msikubali kupewa fedha na wagombea ili wawatumie kama ngazi ya kupata madaraka ya uongozi," alisema.
#############################
Wanamichezo watatu waula CCM
WANAMICHEZO watatu wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani, wamefanikiwa kuchaguliwa kushika nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani hapa.
Wanamichezo hao ni John Bolizozo Katibu anayemaliza muda wake wa uongozi ndani ya Chama Cha Mpira wa Miguu wilayani hapa (BFA), Mousin Bharwan mlezi wa timu zinazotoka ndani ya kijiji cha Vigwaza na Yussuf Kikwete mdau wa michezo Bagamoyo mjini.
Katika uchaguzi huo uliofanyika kwenye Ukumbi wa Chuo Cha Sanaa na kusimamiwa na Mbunge wa Jimbo la Kibiti Abdul Marombwa, pia ulishuhudiwa na Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo Dkt. Shukuru Kawambwa na Katibu wa (CCM), Joyce Massi ambapo Bolizozo ameshinda nafasi ya Uenezi akiwaacha wapinzani wake Emmanuel Panduka na Kassim Gogo.
Bharwan ameibuka kidedea nafasi ya Mkutano Mkuu Taifa ambaye ameshinda nafasi hiyo kwa kujinyakulia kura 753 na kuwaongoza wenzake wanne ambao ni Shumina Sharif, Yussuf Kikwete, Aeshi Khatibu na Issa Kibwana nao wamechaguliwa nafasi hiyo iliwaniwa na wagombea 15.
Wakizungumza baada ya matokeo hayo, Bharwan alianza kwa kuwashukuru wajumbe wa Mkutano huo kwa kuweza kumchagua na kwamba atatumia nafasi hiyo kuhamasisha michezo ikiwa ni kutekeleza ilani ya chama hicho.
"Katika Ilani ya chama chetu inagusia michezo, nitatumia nafasi hii kuhamasisha michezo mbalimbali ndani ya wilaya yetu kwa kuwapatia vijana fursa ya kimichezo kwani utakumbuka kuwa michezo kwa sasa ina nafasi kubwa ya ajira," alisema Bharwan.
Naye Bolizozo alisema baada ya mafanikio makubwa yaliyopatikana ndani ya BFA akiwa Katibu atageuzia makali hayo katika nafasi ya Uenezi ili kuhakikisha vijana wanapata nafasi nzuri ya kushiriki michezo sanjali na kuhamasisha kujiunga na chama hicho.
"Nitatumia nafasi hii kuchagiza uendelezwaji wa michezo ndani ya Wilaya ikiwa ni kuunga mkono ilani ya CCM inayotaka kuendelezwa kwa michezo kwa wananchi bila kubagua itikadi za kisiasa," alisema Bolizozo.