Kijogoodi
JF-Expert Member
- Mar 29, 2021
- 1,363
- 2,372
Mbunge wa Bumbuli January Makamba alikuwa Waziri wa Mazingira katika serikali ya awamu ya 5 kwa miaka minne mpaka alipotenguliwa mwaka 2019.
Inasemekana January Makamba kwa kuwa alikuwa Waziri wa Mazingira kwa hiyo kimya kimya alikuwa anapinga mradi wa Bwawa la Nyerere kuwa eti utasababisha ukataji wa miti na hivyo kupelekea uharibifu wa mazingira nchini.
Leo ameteuliwa kuwa Waziri wa Nishati huku Bwawa la Nyerere litakalozalisha zaidi ya megawatt 2115 likiwa limefikia 52% ya utekelezaji wake na tarehe 15/11/2021 litaanza kujazwa maji rasmi.
Je, January Makamba ataenda kumalizia ujenzi wa hili bwawa au ataenda kufutilia mbali ujenzi wake iki kuokoa mazingira kama msimamo wake ulivyo tangu zamani?
Yetu macho na masikio.
Inasemekana January Makamba kwa kuwa alikuwa Waziri wa Mazingira kwa hiyo kimya kimya alikuwa anapinga mradi wa Bwawa la Nyerere kuwa eti utasababisha ukataji wa miti na hivyo kupelekea uharibifu wa mazingira nchini.
Leo ameteuliwa kuwa Waziri wa Nishati huku Bwawa la Nyerere litakalozalisha zaidi ya megawatt 2115 likiwa limefikia 52% ya utekelezaji wake na tarehe 15/11/2021 litaanza kujazwa maji rasmi.
Je, January Makamba ataenda kumalizia ujenzi wa hili bwawa au ataenda kufutilia mbali ujenzi wake iki kuokoa mazingira kama msimamo wake ulivyo tangu zamani?
Yetu macho na masikio.