Januari Makamba: Tanzania hatuna uhaba wa mafuta, tumeshaagiza mengine ya Mei, Juni 2022

BigTall

JF-Expert Member
Mar 9, 2022
422
1,049
1649247357082.png

Serikali kupitia Wizara ya Nishati imesema mpaka sasa Tanzania haina Uhaba wa Mafuta, hivyo hakuna Sababu ya Watanzania kuwa na Taharuki ya Ukosefu wa Nishati hiyo Muhimu.

Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Waziri wa Nishati, Januari Makamba katika mkutano wake na Waagizaji na Wasambazaji wa Mafuta hapa nchini.

Waziri Makamba amesema hakuna sababu kwa Wananchi kuwa na Taharuki ya Uhaba wa Mafuta kwa sababu bado ipo shehena ya kutosha ya Mafuta Kwenye Maghala yaliyopo na yale ambayo yanashushwa Bandarini.

"Hadi kufikia leo tunayo mafuta ya kutosha kutumika kwa takribani Siku 27, pia Serikali imeshaagiza mafuta yatayotumika Mwezi wa tano na wa sita ambayo yapo kwenye Mchakato," amesema Waziri wa Nishati January Makamba.

Source: Wasafi FM
 
Issue sio uhaba.. Tuna taka serikali oone jinsi ya kuzuia bei isipande. Ondoeni tozo kwenye mafuta,

Sitisheni makato ya REA, sitisheni makato ya EWURA, serikali wekeni ruzuku kwenye mafuta ya magari na mafuta ya kula. Bei za vitu zitashuka. Hatutaki siasa kwenye maisha yetu.

Kama hamkusoma uchumi vyuoni, pigeni chabo Kenya wamefanyaje kwenye mafuta.. Sii kutuambia vitu bita panda bei. Rais ana takiwa kuwa mfariji wa Taifa na sio kututisha.
 
Chama kina wenyewe na chama ndio kimeshika hatamu, wenye chama ndio wenye nchi.
Swali linabaki tu kuwa nje ya Watz milioni 60 wenye nchi ni wangapi? Hawa watu wamejisahau sana
 
Serikali kupitia Wizara ya Nishati imesema mpaka sasa Tanzania haina Uhaba wa Mafuta, hivyo hakuna Sababu ya Watanzania kuwa na Taharuki ya Ukosefu wa Nishati hiyo Muhimu...
Ishu ni bei sio uhaba
 
Issue sio uhaba.. Tuna taka serikali oone jinsi ya kuzuia bei isipande. Ondoeni tozo kwenye mafuta,
Ditisheni makato ya REA, sitisheni makato ya EWURA, serikali wekeni ruzuku kwenye mafuta ya magari na mafuta ya kula. Bei za vitu zitashuka. Hatutaki siasa kwenye maisha yetu.
Mkuu kwa serikali zetu za kimatumbi licha ya ushauri mzuri kama huu they will turn on a deaf ear and blind eye. Hali kusema kweli ni ngumu. It just need a sincere political will, strategy and sacrifice from the people on top there.
 
Kuna bwana mmoja jana alinambia baada ya mama samia anaandaliwa huyu upara nilicheka sana
Kwanini ucheke mkuu? Tanzania yeyote anaweza kuwa Rais na mambo yakaenda. Kwani kuna ugumu gani. Kikubwa tuna mweyez Mungu ndio Rais wetu na kila kitu bila yeye wote tungeshaangamia zamani.

Mlete hapa raia wa uswiz au Qatar aje aishi masaa machache kama sisi kama atatoboa. We have God who protects us. Mungu na mkono kwenda kinywani ya tosha. Bila hivyo hata ukifanyaje hatuwez kusonga mbele kama hiki chama kitaendelea kung'ang'ania madaraka.
 
-Kama tunayo stock ya kutosha siku 27 kwenye maghala, kwa nini Eura wanapandisha bei ya mafuta leo hii.

-Serikali inawaambia Wananchi kuwa stock hii imeagizwa kwa bei mpya au bei ya zamani?

-Kwa nini Serikali isitumie fedha za mfuko Mkuu(Consolidated Fund to cushion world fuel price increase) kutoa ruzuku kwa waagizaji wa petrol.

-Kupanda kwa bei ya mafuta ni mateso kwa wapiga kura.

-Serikali ifanye bajeti reallocation kwa kupunguza gharama zisizo muhimu na fedha zitolewa ruzuku kwa waagizaji wa bidhaa za petrol ili kuwapunguzia makali ya maisha wananchi wa kawaida.

-Ili kusaidia Wananchi, Serikali inaweza kufikiria kupunguza VAT kwenye bidhaa za petrol.
 
Kwanini ucheke mkuu? Tanzania yeyote anaweza kuwa Rais na mambo yakaenda. Kwani kuna ugumu gani. Kikubwa tuna mweyez Mungu ndio Rais wetu na kila kitu bila yeye wote tungeshaangamia zamani. Mlete hapa raia wa uswiz au Qatar aje aishi masaa machache kama sisi kama atatoboa. We have God who protects us. Mungu na mkono kwenda kinywani ya tosha. Bila hivyo hata ukifanyaje hatuwez kusonga mbele kama hiki chama kitaendelea kung'ang'ania madaraka.
Mambo ya Mungu tena mkuu kwa hoja hii sitii neno hapa maana naona we wawaza kidini dini tu
 
Na bei imepanda sababu ya wingi wa mafuta ?

Obviously hata kama tungekuwa tuna pipa moja kama kila tone lingeuzwa milioni hamsini tungesema hatuna uhaba kutokana na affordability....
 
Mapaka kazini!

"Mafuta yapo ya kutosha lakini kuhusu kupanda kwake bei mtajijua wenyewe"😁😁😁
ummY_jc.jpg
 
Back
Top Bottom