Janja ya CHENGE, yamng'oa Sitta na mafisadi washangilia ushindi

Tonge

JF-Expert Member
May 7, 2010
695
12
Duuuuuuuuuh kweli dunia tambara bovu, Kwa maoni yangu Sitta si mtu wa kunyimwa uspika katika bunge hili ila kwa kitendo cha Chenge kuandaa press conference ya kumponda sitta tena kwa taarifa iliyoandikwa kwa mkono ni dhahiri kulikuwa kuna kundi lilijipanga ili kuonyesha kuwa Chenge na Sitta wanaugomvi au kumchafua Sitta ili kamati kuu ya CCM iwateme wote na nafasi yake ichukuliwe na Ana Makinda maana hawa Ana Abdallah na Kate Kamba ni wasindikizaji tu.

Mafisadi kwao huu ni USHINDI wa kishindo na sasa wanakunywa mvinjo, Nimekuwa nikifuatilia mara kibao bunge lililopita na mara nyingi Makinda anapokuwa spika huwa haruhusu mijadala au hoja toka kwa wabunge pinzani (Marehemu Wagwe na Makinda, Zitto na Mkinda) nahisi kama ndie yeye ambaye angekuwa spika kipindi hicho basi hoja kama za RICHMOND, MEREMETA NA RADA tusingezijua kwani angezikatalia kujadiliwa au kupelekwa bungeni, CCM kweli ni CHAMA CHA MAFISADI na hawana uchungu na nchi hii bali ni kuchukua chao mapaemaaaaaaaaaa.Mh mzee wa VIJISENTI tambua kuwa watanzania wa leo sio waleeeeeee wa zama za Julius, tunaelewa na tuna upeo wa kutambua janja zenu nyie mafisadi.

Mh Sitta aluta continua "mapambano yanaendelea" na kwa kuwa sasa wewe sio spika huu ndio wakati wako wa kupenyeza hoja bungeni na kuzichangia hasa zile zinazo husu ufisadi nchini kwani tuna imani unajua mengi na una siri kubwa za kina Lowasa, Rostam na Chenge(mafisadi).

Mh Chenge hivi huoni hata aibu, umempa Hosea vijisenti na kakutetea kwamba wewe ni mtu safi kwenye skendo ya RADA, umeona sasa Uingereza wamemuumbua? Chenge hizi kweli wewe ni mtanzania? maana inaonyesha kuwa huna uchungu na nchi hii na wananchi wake,tumekuchoka CHENGE.
 
CCM ina wenyewe - Pole sana kaka yangu Six. Jamaa ndiyo wameshakumaliza na kukushindilia kabisaa kwani hutakaa ugombee tena nafasi yoyote kubwa zaidi ukiwa ndani ya CCM zaidi ya huo ubunge wa Urambo.

Wewe na wenzako mlikuwa targeted muda mrefu tangu Richmood, nafikiri sasa umeamini tena kwamba ndani ya CCM hakuna HAKI. Wazo la kutetea maslahi ya nchi na kupinga UFISADI lilikuwa zuri sana lakini bahati mbaya halikuwa na baraka na chama chako na hiyo ndiyo adhabu iliyokutafuna.

Utapata muda sasa wa kuwatumikie wananchi wa Urambo kwa ukaribu zaidi, MAFISADI huwawezi sababu wako ndani ya mfumo ktk chama chako, kumbuka maneno ya waziri Mkuu wako Pinda ambaye alikwambia Bungeni kwamba " Mafisadi wana Nguvu sana"

Mwisho nakuomba wewe uwe kiongozi wa wabunge wa CCM na wa Upnzani TABORA ili muuendeleze mkoa wetu kwani upo nyuma sana kimaendeleo, ungana na wezako wa TABORA MJINI, NZEGA, SIKONGE, IGUNGA, URAMBO MAGHARIBI muwe kitu kimoja.
 
Sidhani kama sita ndio kapotezwa jumla.
Kuna posibility kubwa sana akawa waziri wa wizara nyeti.
 
Back
Top Bottom