Janga kubwa katika Tanzania ni viongozi kutaka kuwa ma-celebrities

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Ndugu zangu,

Awali ya yote naomba niseme naijua kiasi fulani historia ya taifa hii. Kwa mtazamo wangu, kuna 'legacy tricks' zinazotoka toka kipindi cha ujamaa ambazo tumezishikilia, hasa systems za nchi hii, kwa kuwa kwa mtazamo wao zilifanya kazi huko nyuma kwa hiyo hawataki kuziacha.

Hii tabia ya kutaka viongozi wawe maarufu kuliko mtu mwingine yoyote inatuharibia sana. Kwa mtazamo wao katika kila ngazi, kiongozi ndiyo wanataka awe maarufu na anayekubalika zaidi. Matokeo yake, mtu mwingine yoyote anayechipuka anayetaka kuwaibia umaarufu wao wanamuona ni tishio kwa usalama wa nchi. Ndiyo maana tunaona viongozi wanashindana na madogo katika majukwaa ya muziki, katika vyombo vya habari, katika michezo, katika mitandao ya kijamii, nk. Hatujui nafasi ya kila mmoja wetu katika jamii hii ni ipi.

Nimeileta hii mada maana mnaweza kuiona ni ndogo lakini inatuharibia katika sekta nyingi sana kuanzia elimu, uhuru wa vyombo vya habari na hadi katika sanaa na michezo. Hizi sekta hazitakuja kukua kamwe kama hili suala halitarekebishwa na tukaachana na dhana hii potofu.
 
Ndugu zangu,

Awali ya yote naomba niseme naijua kiasi fulani historia ya taifa hii. Kwa mtazamo wangu, kuna 'legacy tricks' zinazotoka toka kipindi cha ujamaa ambazo tumezishikilia, hasa systems za nchi hii, kwa kuwa kwa mtazamo wao zilifanya kazi huko nyuma kwa hiyo hawataki kuziacha.

Hii tabia ya kutaka viongozi wawe maarufu kuliko mtu mwingine yoyote inatuharibia sana. Kwa mtazamo wao katika kila ngazi, kiongozi ndiyo wanataka awe maarufu na anayekubalika zaidi. Matokeo yake, mtu mwingine yoyote anayechipuka anayetaka kuwaibia umaarufu wao wanamuona ni tishio kwa usalama wa nchi. Ndiyo maana tunaona viongozi wanashindana na madogo katika majukwaa ya muziki, katika vyombo vya habari, katika michezo, katika mitandao ya kijamii, nk. Hatujui nafasi ya kila mmoja wetu katika jamii hii ni ipi.

Nimeileta hii mada maana mnaweza kuiona ni ndogo lakini inatuharibia katika sekta nyingi sana kuanzia elimu, uhuru wa vyombo vya habari na hadi katika sanaa na michezo. Hizi sekta hazitakuja kukua kamwe kama hili suala halitarekebishwa na tukaachana na dhana hii potofu.
Kiongozi akipenda kua maarufu kuliko mtu yoyote inakusumbua nini kama kiongozi akiwa anapenda sifa au kutaka umaarufu kwa mambo ya kujenga jamii. Kwa mfano, jpm alikua kiongozi anaependa sifa na kua superstar kwa mambo ya kujenga jamii. Mi naona nikitu kizuri kama ukikichukulia kwa mtazamo chanya.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
 
Bora u celeb

Kuliko wao wanavyotaka kuwa mabilionea

Ova
 
Bora u celeb

Kuliko wao wanavyotaka kuwa mabilionea

Ova
Ndiyo huko huko mkuu, hawataki mwingine awe na hela kuwazidi au labda uwe mtu wao, hivi hivi utasumbuka sana. Haya mambo sijui kwa nini hamyaangalii kwa undani wake.
 
Kiongozi akipenda kua maarufu kuliko mtu yoyote inakusumbua nini kama kiongozi akiwa anapenda sifa au kutaka umaarufu kwa mambo ya kujenga jamii. Kwa mfano, jpm alikua kiongozi anaependa sifa na kua superstar kwa mambo ya kujenga jamii. Mi naona nikitu kizuri kama ukikichukulia kwa mtazamo chanya.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app
Ndiyo mwanzo wa kutotaka kukosolewa na kutaka kuonekana malaika na mtakatifu. Kazi ya kiongozi wa kisiasa ni kufanya kazi uliyochaguliwa au kuteuliwa kuifanya, kukubaliwa kwako kutaonekana kwenye sanduku la kura siyo kumeza na kuminya uhuru wa watu kufanya taaluma zao ili wewe tu uwe juu.

Kutumia madaraka vibaya inatakiwa kuwa ni kosa la juu sana kwenye nchi ya kidemokrasia ila wewe mara ya mwisho umesikia lini nchi hii mtu ameshitakiwa kwa kutumia madaraka yake vibaya, ukimuacha Sabaya aliyetolewa kafara? Ila kila siku viongozi wanafanya hivyo hadi imeonekana ni kawaida tu.
 
Kiongozi akipenda kua maarufu kuliko mtu yoyote inakusumbua nini kama kiongozi akiwa anapenda sifa au kutaka umaarufu kwa mambo ya kujenga jamii. Kwa mfano, jpm alikua kiongozi anaependa sifa na kua superstar kwa mambo ya kujenga jamii. Mi naona nikitu kizuri kama ukikichukulia kwa mtazamo chanya.

Sent from my SM-A025F using JamiiForums mobile app

Umaarufu huja automatically na sio kwa shuruti. Matokeo yake ndio akaishia kuwa na umaarufu wa kidictator uchwara.
 
Back
Top Bottom