KIDUNDULIMA
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 966
- 536
Jana kwa mara ya kwanza nilibahatika kupanda basi moja na mwana JF. Niligundua kuwa ni mwana JF pale ambambo alipokuwa anatumia laptop yake na kuaccess internet. Nilipochungulia niliona ana access mtandao wa JF ingawa user name yake sikuiona. Kilichonishangaza sana ni kuwa kabla ya kujua kuwa ni mwan JF wote wawili (mimi na yeye) tulijitolea kumsaidia jamaa mmoja aliyekuwa ameibiwa pesa hivyo kukosa nauli. Bahati mbaya sana sikutaka kureveal my true identity mbele yake kutokana na nafasi yangu katika JMT. Pamoja na kuwa tulisalimiana hakuna majadiliano zaidi yaliyofanyika kuhusu JF.
Hayo ndiyo yaliyotokea saa 12.30 jioni wakati naelekea Moro kwa basi la Hood.
Hayo ndiyo yaliyotokea saa 12.30 jioni wakati naelekea Moro kwa basi la Hood.