TUSHIRIKISHANE JamiiForums yazindua rasmi mradi wa "Tushirikishane"

View attachment 381424 KIPITA SHOTO MJINI NZEGA


Nikiwa kama mwananzego(mkazi) wa mji wa nzega nimefurahi sana kupata majibu kutoka kwa mwanachama mwenzetu hapa jamii Forum anajiita GIDEON ANYONA safi ila na swali

Leo hii jamii Forum wamekuja na huu mradi katika jimbo la nzega wameanzisha huu mjadala tumeweza yasema tunayoona kero na Gideon amajibu niwapongeze jamii Forum kwa hili kwani tumepata pakusemea

Swali langu kwa huyu Gideon taminije usemayo ni tarifa sahihi?

Pili ikiwa usemayo ni tarifa sahihi je ni wapi mwananzego asiyejua tumia jamii Forum akaona tunayoyajadili hapa anaweza kwenda nakuzikuta hizi tarifa sahihi?

Tatu unaweza kuwa msaad kwangu na wananzega wengine watumiao hii mitandao ya kijamii tunaomba utupatie tofuti ya halmashauri ya mji nzega ili tuingie tuone yaliyomo maaana nimehangaika sana kutafuta tarifa za ulichonijibu sijaona

Asante
Taarifa sahii zipo Ofisi ya Mbunge na Halmashauri ya Mji.
 
Mh Mbunge Hussein Bashe akikagua ujenzi wa bweni shule ya sekondari ya Bulunde.
Ahadi ya Mh Mbunge ni Nzega kutoa elimu ya A-level ndani ya miezi 9 ijayo.
1471168222364.jpg
 
Asante sana kwa majibu mazuri swali tarifa zipo je mnahakikishaje sisi wananzengo hizi tarifa zinatufikia kwa wakati kwa lengo la kuondoa tarifa potofu potofu mitaani kwani wanaichi wengi si wafikaji wa ofisi za halmashauri au ofisi za Mbunge
Mwanazengo kanuni ya Information siku zote huwa inatafutwa. Taarifa ikishawekwa sehemu sahii ni jukumu la mtu ambae anaitaka taarifa ile kuitafuta.

Kwa mfano vitabu uandikwa na mtu akitaka taarifa kwenye kitabu huwa anaenda library au bookshop. Hizo ndio sehemu sahii za kupata vitabu.
Kwa taarifa za Jimbo mwananchi akizitaka atazipata Ofisi ya Mbunge au Halmashauri kwani mikutano ya adhara haitoshi kuwaelezea wananchi shughuli zinazofanywa na mbunge wao.
 
IMG_20160815_182644.jpg


SIJUI NILITAJE HILI KUWA NI KIVUTIO CHA MAONYESHO KUWA ZAMANI NZEGA KULIKUWAGA NA TANKI LA MAJI AU NINI MAAANA TUKISEMA TANKI LA MAJI TUNAKOSEA KWANI MAJI HAYAPATIKANI TENA KATIKA TANKI HILI KWA SASA

JAMANI


kama ni kero na tatizo linaloitaji ufumbuzi wa haraka katika mji wa nzega basi ni tatizo la maji

Na kiongozi au uongozi utakaondoa tatizo la maji mjini nzega kamwe hautosaulika kamwe na wakazi wa nzega
 
Hongereni sana jf kwa hatua hii!, tangu mwanzo jf ilikuwa ni kwa keyboard, sasa it is for read, tumetouch base ground zero!, tuwahamasishe na wana jf wengine, tusiishie kwenye keyboards, twendeni ground zero, huko ndiko kwenye uwanja wa Mapambano!.

Hongera sana Max, Mike, Asha na timu nzima ya jf!.

Pasco
 
IMG_20160823_145349.jpg
yani ingekuwa raha sana kwa mji wa nzega unakuta ubao za matangazo zenye tarifa kama hizi nazingine hususani maeneo ya mkusanyiko wa watu wengi mfano kituo cha mabasi, gulioni, mnadani yani ukifika tu unaona ubao mkubwa wa matangazo wa ofisi ya Mbunge umejaa tarifa mbali mbali za Mbunge na wanainchi kwa ujumla kuhusu jimbo lao nk, si mpaka mwanainchi aje ofisi ya Mbunge ndio akute ubao wa matangazo asome
 

Attachments

  • IMG_20160823_145349.jpg
    IMG_20160823_145349.jpg
    123 KB · Views: 92
IMG_20160823_145622.jpg
tarifa kama hizi, kwenye ubao wa matangazo ofisi ya Mbunge zipo swali wangapi wanafika kuzisoma, zaidi mtaani tunaongopeana tu Mala hivi Mala vile kwani wananzengo hakuna utaratibu wa kutafuta habari ila hizi tarifa zingekuwepo sehemu ya mkusanyiko wa watu wengi mfano, kituo cha mabasi, gulioni, mnadani, katika vituo vya afya, sokoni zingepata msukumo nakufukia watu wengi zaidi na zaidi
 
Changamoto kubwa ni jinsi gani matangazo haya yanaweza kutunzwa pasipo kuaribiwa kwani uzoefu unaonyesha watu upendelea kuchana matangazo sana
 
Ikiwa mikutano ya Kisiasa taarifa zake huwafikia wananchi basi na taarifa hizi za kimaendeleo zitumie njia hizo hizo katika kuwafikia Wananchi, kama Local radio kufanya Matangazo mara kwa mara
 
Ikiwa mikutano ya Kisiasa taarifa zake huwafikia wananchi basi na taarifa hizi za kimaendeleo zitumie njia hizo hizo katika kuwafikia Wananchi, kama Local radio kufanya Matangazo mara kwa mara
Ni wazo zuri lakini ni gharama pia kutoa matangazo kubandika kila sehemu. At the moment tu rasilimali fedha ndogo sana na majukumu ni mengi.
Tunawanafunzi wengi yatima , tunawagonjwa na majukumu mengi kwahiyo kila shillingi tunaitumia ipasavyo.

Kikubwa lazima watu pia waamke. Uwezi tafuta almasi ukiwa umelala. Taarifa nyingi ziko ofisini kwa mbunge na Halmashauri. Tunajitaidi lakini pia ni jukumu la kila mtu kama wewe hapo mwenye ufahamu nawe ukawaambia ndugu na marafiki waje kupata taarifa
 
Back
Top Bottom