JamiiForums yashinda mapingamizi yaliyowekwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG)

JamiiForums

JF Official Account
Nov 9, 2006
6,202
4,991
Kesi ya Kikatiba: JamiiForums yashinda mapingamizi yaliyowekwa na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG)


Wakuu,

Mtakuwa mnakumbuka kuwa Jamii Media mnamo mwezi Machi mwaka huu walifungua KESI YA KIKATIBA kupinga matumizi ya baadhi ya vifungu vya Sheria ya Makosa ya Kimtandao ya mwaka 2015 kuwa vinavunja Haki ya Kikatiba na hivyo kuitaka Mahakama kuingilia kati nguvu kubwa iliyokuwa ikitumiwa na Jeshi la Polisi ili kulinda usiri na uhuru wa watumiaji wa mitandao nchini.

Serikali, kupitia Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali(AG) iliweka mapingamizi (Preliminary Objections) sita ikitaka kesi nzima ifutwe na Jamii Media walipe gharama zilizoingiwa.

Leo hii, Mahakama Kuu ya Tanzania imezipitia hoja zilizowasilishwa na Serikali na Wanasheria wa Jamii Media na kuamua kuwa mapingamizi yote sita ya Serikali hayana mashiko na hivyo kesi ya msingi itaendelea kusikilizwa haraka iwezekanavyo.
14021567_10208682093162492_5397368467667262646_n.jpg

Pichani ni Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Bw. Maxence Melo akiwa na Wakili wa kampuni, Benedict Ishabakaki muda mchache baada ya kupata maamuzi ya mahakama.

Hii ni hatua kubwa kufikiwa kuelekea Uhuru wa Maoni kwa watumiaji wa Mitandao(Online Freedom of Expression) na jitihada za kulinda watoa taarifa ndani na nje ya mtandao(Whistleblowers).

HAYA NDIYO MAPINGAMIZI(Preliminary Objections) YA SERIKALI DHIDI YA SHAURI LA JAMII MEDIA:

Screen Shot 2017-03-10 at 14.29.49.png
Screen Shot 2017-03-10 at 14.30.05.png



Tutaambatanisha maamuzi ya mahakama(ruling) baadae.

Asanteni



 
Safi sana.

Mungu azidi kuwaongoza wote wenye mapenzi Mema na Taifa hili.

Ni matumaini yangu kwa uwezo wa Allah, Mahakama itatenda haki ktk kesi ya msingi.
 
Tuna imani hii kesi itasikilizwa na uamuzi ambao uko fair utatolewa kulinda usiri na uhuru wetu.

Naamini hata viongozi wa serikali wanajua manufaa ya JF.

Tuko pamoja JF Team
 
Back
Top Bottom