JamiiForums
JF Official Account
- Nov 9, 2006
- 6,202
- 5,012
Umoja wa Klabu za Wanahabari Tanzania (Union of Tanzania Press Clubs) umetoa tuzo ya mwaka 2019 ya Daudi Mwangosi kwa taasisi ya JamiiForums leo hii katika ukumbi wa Raha Leo pale Zanzibar.
Tuzo hii imepewa jina la mwanahabari nguli aliyefariki akiwa katika harakati za kutimiza majukumu yake ya kuhabarisha umma, Marehemu Daudi Mwangosi.
Tuzo hii hutolewa kila mwaka kwa mwanahabari au taasisi ambayo imetimiza vigezo vya juu vya utoaji habari na kuchochea uhuru wa kutoa na kupokea taarifa.
Mwaka huu, tuzo hii imetolewa visiwani Zanzibar ambapo Mkurugenzi Mkuu, Maxence Melo ameipokea kwa niaba ya Watendaji wote wa taasisi.
JamiiForums inapenda kutoa shukrani za dhati kwa UTPC kwa kuwapa heshima hii na inaahidi kuendelea kupigania uhuru wa kujieleza, haki ya kupata habari, usiri wa taarifa binafsi na ulinzi wa kidijitali.
Kwa nafasi ya pekee, tunathamini na kutambua mchango wa watumiaji na wadau wa JamiiForums katika kupata tuzo hii.
Kwa niaba ya JamiiForums Mkurugenzi Mkuu, Maxence Melo - ametoa shukrani mbalimbali baada ya kupokea tuzo amabazo tutapandisha si punde.
Sehemu ya Hotuba ya Maxence Melo:
Anaanza na Salamu kwa mgeni rasmi na wageni wote.
Sisi kama JamiiForums (wadau na waendeshaji) tunashukuru sana kwa fursa hii. Nichukue nafasi hii kwa kusema wanahabari tunakutana na changamoto kubwa sana. Inatia faraja kuwa tunayopitia yanaonwa na yanaleta tija.
UTPC wamekuwa wakinialika kwenye siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani lakini miaka 2 iliyopita nimeshindwa kwenda kwa sababu huwa kesi yetu ilikuwa inatajwa ama kusikilizwa mahakamani tarehe hiyo.
Na leo nimeomba ruhusa mahakamani. Naishukuru Mahakama na dola kwa ruhusa.
Tasnia ya Habari imekutana na changamoto ya sheria mpya na mabadiliko ya mifumo. Unaweza pitia mambo ukadhani kwamba “It’s not worth it” lakini haya ndo mambo tunayotakiwa kuyasimamia.
JF imepitia changamoto. Lakini tumeweza kukabiliana na hali. Tusimamie maadili, tunachokiamini. Kwa sisi JF kama ‘Alternative media’ kuonekana na UTPC tunasema Asanteni sana.
Tuwapongeze wanaotumia mitandao kwa ujumla pia.
Nawapongeza watendaji, bodi ya wakurugenzi na zaidi niwapongeze wanahabari, members wa JamiiForums (wanaotumia mtandao wetu wa JF na walio katika kurasa zetu za kijamii).
Nawapongeza wanahabari wa Tanzania kwa uvumilivu katika tunayoyapitia. Tunapitia changamoto nyingi lakini tunaendelea kufanya kazi kwa weledi kabisa.
Asante kwa ubalozi wa Sweden!
Maxence Melo amesema tuzo hiyo si ya JamiiForums pekee bali ni kichocheo kwa wanahabari wote kwa maelezo kuwa tasnia ya habari Tanzania haiko salama licha ya uvumilivu mkubwa walionao wanahabari.
Hii ni tuzo ya tatu kwa Jamii Forums, 2019. Tuzo ya kwanza ilitolewa kwa Mkurugenzi wake, Maxence Melo na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu na ya pili ikitolewa na CPJ
Tuzo hii imepewa jina la mwanahabari nguli aliyefariki akiwa katika harakati za kutimiza majukumu yake ya kuhabarisha umma, Marehemu Daudi Mwangosi.
Tuzo hii hutolewa kila mwaka kwa mwanahabari au taasisi ambayo imetimiza vigezo vya juu vya utoaji habari na kuchochea uhuru wa kutoa na kupokea taarifa.
Mwaka huu, tuzo hii imetolewa visiwani Zanzibar ambapo Mkurugenzi Mkuu, Maxence Melo ameipokea kwa niaba ya Watendaji wote wa taasisi.
JamiiForums inapenda kutoa shukrani za dhati kwa UTPC kwa kuwapa heshima hii na inaahidi kuendelea kupigania uhuru wa kujieleza, haki ya kupata habari, usiri wa taarifa binafsi na ulinzi wa kidijitali.
Kwa nafasi ya pekee, tunathamini na kutambua mchango wa watumiaji na wadau wa JamiiForums katika kupata tuzo hii.
Kwa niaba ya JamiiForums Mkurugenzi Mkuu, Maxence Melo - ametoa shukrani mbalimbali baada ya kupokea tuzo amabazo tutapandisha si punde.
Sehemu ya Hotuba ya Maxence Melo:
Anaanza na Salamu kwa mgeni rasmi na wageni wote.
Sisi kama JamiiForums (wadau na waendeshaji) tunashukuru sana kwa fursa hii. Nichukue nafasi hii kwa kusema wanahabari tunakutana na changamoto kubwa sana. Inatia faraja kuwa tunayopitia yanaonwa na yanaleta tija.
UTPC wamekuwa wakinialika kwenye siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari duniani lakini miaka 2 iliyopita nimeshindwa kwenda kwa sababu huwa kesi yetu ilikuwa inatajwa ama kusikilizwa mahakamani tarehe hiyo.
Na leo nimeomba ruhusa mahakamani. Naishukuru Mahakama na dola kwa ruhusa.
Tasnia ya Habari imekutana na changamoto ya sheria mpya na mabadiliko ya mifumo. Unaweza pitia mambo ukadhani kwamba “It’s not worth it” lakini haya ndo mambo tunayotakiwa kuyasimamia.
JF imepitia changamoto. Lakini tumeweza kukabiliana na hali. Tusimamie maadili, tunachokiamini. Kwa sisi JF kama ‘Alternative media’ kuonekana na UTPC tunasema Asanteni sana.
Tuwapongeze wanaotumia mitandao kwa ujumla pia.
Nawapongeza watendaji, bodi ya wakurugenzi na zaidi niwapongeze wanahabari, members wa JamiiForums (wanaotumia mtandao wetu wa JF na walio katika kurasa zetu za kijamii).
Nawapongeza wanahabari wa Tanzania kwa uvumilivu katika tunayoyapitia. Tunapitia changamoto nyingi lakini tunaendelea kufanya kazi kwa weledi kabisa.
Asante kwa ubalozi wa Sweden!
Maxence Melo amesema tuzo hiyo si ya JamiiForums pekee bali ni kichocheo kwa wanahabari wote kwa maelezo kuwa tasnia ya habari Tanzania haiko salama licha ya uvumilivu mkubwa walionao wanahabari.
Hii ni tuzo ya tatu kwa Jamii Forums, 2019. Tuzo ya kwanza ilitolewa kwa Mkurugenzi wake, Maxence Melo na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu na ya pili ikitolewa na CPJ