JamiiForums yamtumbua mtangazaji wa Nirvana (EATV), alazimika kuacha kazi ghafla..

Interest

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
3,433
7,055
Naweza nisiwe sahihi..

Juzi kati hapa nikiwa napitia nyuzi kwenye Jukwaa hili la Celebrities ambalo ni mahsusi kwa ajili ya habari za watu maarufu, nilikutana na uzi huu - Huyu mtangazaji kipindi cha Nirvana jamani? ambao ni wa mwezi May mwaka huu (mjadala ulioendelezwa hadi mwezi Juni/Julai 2016).

Ndani ya huo mjadala, wachangiaji walifunguka vya kutosha namna wanavyomuona mtangazaji huyu mwenye manjonjo na wengi walionesha kumtilia shaka 'usalama wake'..

Pengine, narudia pengine, uzi huo ulimfikia mlengwa na kum-frustrate sana kwani siku chache zijazo zikaja taarifa za ghafla kwamba jamaa ameamua 'kustaafu' kufanya kipindi hicho na leo (Jumanne Julai 19, 2016) anafanya show ya kuagwa na kumtambulisha mtangazaji mpya..

Kama niwazacho ni sahihi, basi ni sahihi kusema JamiiForums imemtumbua huyu jamaa wa Fashoooooon!

Kwa wasiomfahamu Deogratious Kithama (mkali wa fashoooon);
nirvana.jpg


Moja ya kazi zake za hivi karibuni;


#Ndukiiiii
 
Kipimo kile kile muwapimiacho wengine ndicho mtakacho pimiwa. Kama kuna vidhibitisho zaidi ya hivyo vya hisia wekeni hapa. Mwenyewe kasema atakua kwenye media kwa kipindi kirefu... Sasa wewe mleta post sijui una maanisha nini
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom