Alhamisi, Desemba 15, 2022
JamiiForums, UTPC kunoa waandishi 500 wa habari-uchunguzi
Mkurugenzi wa JamiiForums, Maxence Melo na Mkurugenzi wa Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania ( UTPC), Kenneth Simbaya wasaini mkataba wa ushirikiano kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa waandishi wa habari za uchunguzi.
UTPC na Jamii Forums wamesema wameingia katika Ushirikiano wa Kimkakati kwa lengo la kuwajengea uwezo Waandishi wa Habari Nchini katika kuandaa Habari za Kiuchunguzi (IJ) na zenye Maslahi ya Umma (PIJ) ili kuchochea Uwajibikaji na utawala bora
Pia, Waandishi watajengewa uwezo kuhusu Usalama wa Kidijitali, matumizi sahihi na bora ya Vifaa na Mifumo ya Kidijitali na namna bora ya kutumia Uwanja wa Kidijitali kuendeleza kazi zao
Aidha, Mkurugenzi wa JamiiForums amesema litaanzishwa shindano la #StoriesOfChange litakalowalenga Waandishi wa Habari na Washindi watatuzwa baada ya mchujo.
Ushirikiano huu ni miaka 2, utaanza rasmi Januari 2023 na unaweza kuhuishwa baada ya kufanya tathmini.