ebwana weee jembe... Ngoja nifanyie kazi, ntaifanya my blue print kwenye matumizi yangu ya mwezi... Santaa..Mkuu, ni kupangilia tu, ingawaje huo mshahara sio mkubwa, lakini huwezi ku-suffer on ur way on getting perfect job for u. Binafsi, natumia about TZS 150,000/= kwa mwezi na napiga menu ya maana kabisa kuliko anayetumia 300,000/= kwa mwezi.
Here is how I do (Huwa nafanya yafuatayo mara nipatapo salary yangu):
- Nanunua mchele 15 kg@ 1,500/- = TZS 22,500/-
- Nampa mshikaji wa bucha sh. 28,000/ kwa mwezi ~hapo ni nyama 0.5kg (stake) na 0.5kg(maini). Hizo ni kwa wiki, ambapo natumia 7,000/- kwa wiki na 28,000/- kwa mwezi. Nilichofanya baada ya kuhamia hapa kitaa, nikajenga mazoea na mshikaji wa bucha hadi akawa rafiki yangu na hivyo, ninapomwachia 28,000/- nina uhakika wa kwenda kuchukua nyama kila wiki bila longolongo!
- Watu wa mwambao bila nazi, msosi hauendi...na siku kuna nazi(ya tui) za bakhresa, nina shida gani!!!! Natumia pakti mbili kwa wiki @600, therefore nanunua za mwezi mzima kwa sh. 4,800/-
- Huwa nanunua mafuta ya kula tena yale yale ambayo maskini kama mimi wanayaogopa....ya alizeti kwa sh.18,000/ (lita 3) ambayo nayatumia si chini ya miezi 4 (means kwa mwezi na-spend sh 4,500/-)
- Nanunua in advance sukari 2kg @2000= TZS 4,000/- .
- Nanunua Soya 3 packets @2,000~~~~ TZS 6,000/- kwa mwezi (huwa situmii kabisa majani ya chai)
- Maharage 2kg@ 1,800/= (3,600/- kwa mwezi).... nyama peke yake huwa haipandi kwahiyo lazima nipate maharage kidogo.
- Tambi kwa ajili ya weekend 8pc @ 1000= 8,000/-
- Mafuta ya taa 6lts @ 2000 = 12,000
- Njegele 1,200/- kila weekend...napenda sana hii ki2 na tambi!= 4,800/- kwa mwezi
22,500 + 28,000+4800+4500+4000+6000+3600+8000+12,000+4,800= 98,200/=
Hapo unakuta natumia kama laki tu, lakini napata vitu vyote muhimu for my favorite meal !! Addition point ni kwamba, ninapoenda job, huwa sinywi chai asubuhi, BALI HUWA NAKULA MSOSI!!!
Nimeeleweka?
Sinywi chai; NAPIGA MSOSI! Always, ingawaje sikai mbali na town, huwa naamka saa 11 alfajiri na kuanza kupika WALIIIIIIIII......! Nikishapiga menu yangu ya adabu asubuhi, wala sihangaiki lunch time; by the way, nikishatulia kwenye kiti changu huwa sipendi usumbufu!
Eti unakuta mtoto wa kiume anasema "eti siwezi kula asubuhi.....!" mtu ukiwa na hayo mawazo then be prepared kuolewa mambo yatakapobana! Nasikitika sana kwamba hamna daladala ambazo naweza kulipa in advance, otherwise, I'd do it....sipendi stress kwenye maisha, hususani kwa vitu vya kipuuzi kama basic needs!
Try it, utakuja gundua maisha is very easy sema hatuyajulii tu!!!
Unaweza kumPM invisible au maxence atakupa maelekezo. Kila la heri.hii ndo JF bana,yan ni kila ki2,.mi nawashukuru wote na nmeenda leo ofic moja nkaanza kazi,kweli salary ni 400000 hyo haikatwi chochote ila inaongezwa na 37000 kama communication expenses na transport. Jaman mi nataka kujua how ntaweza kuichangia JF coz mi kwangu ndo kila ki2 yan nikiumwa-najiuliza hapa,nikikwazwa na mpnz,.hapa ndo solution,kaz nmepata hapahapa. Nawashukuru sana tena sana.
hongera kwa kupata kazi sasa kishumbua mahoko inatakiwa utoe 2% ya gross yako uichangie JF ni hayo tu..
ebwana weee jembe... Ngoja nifanyie kazi, ntaifanya my blue print kwenye matumizi yangu ya mwezi... Santaa..