SoC01 Jamii yetu ijifunze kitu kupitia hatua zilizotekelezwa katika kufikia maendeleo ya Bara Ulaya

Stories of Change - 2021 Competition

Theb

JF-Expert Member
Jan 25, 2019
3,929
7,268
Habara za siku wa ndugu..?

Napenda kuwapa haka kaandiko tena tujifunze kidogo kupitia maendeleo ya wenzetu wa bara ulaya. Andiko hili litaangazia baadhi ya mapinduzi yaliyotekelezeka kule ulaya na yakawapa maendeleo waliyoyafikia ambayo sote tuna ya husudu. Baadhi ya mapinduzi hayo ni kama mapinduzi ya kwenye kilimo, mapinduzi kwenye mfumo wa utawala, teknolojia na viwanda.

Mapinduzi katika kilimo

Mnamo karne ya 17 kuendelea mpaka karne ya 19 barani ulaya walifanya mapinduzi makubwa kwenye kilimo.
Mfano. Waliboresha baadhi ya mbegu. Waliboresha mfumo wa umwagiliaji mashambani na waliweza kuachana na mifumo ya uzalishaji wa kizamani kwa ujumla na kuanza kuzalisha kwa kutumia zana za kisasa.


Mapinduzi katika viwanda.

Hapa pia watu wa bara ulaya walifanikiwa kufanya mapinduzi makubwa kwenye viwanda. Mnaomo karne ya 18 ilianzia Wingereza na kusambaa mataifa mengine. Kwenye viwanda walifanya maboresho yafuatayo. Matumizi ya mashine zilizoboreshwa zaidi viwandani, mfumo wa wafanyakazi ukabadilishwa ikawa na kuzingatia ujuzi wa mtu na zingine matumizi ya umeme kwenye uzalishaji pamoja na makaa ya mawe viwandani kuendesha mashine yakatejelezeka.


Mapinduzi katika sayansi na teknolojia

Pia waliweza kufanya mapinduzi kwenye sayansi na teknolojia. Mfano walianza kuboresha huduma za mawasiliano na kutengeneza magari, mashine, na vitu vingine



Mapinduzi katika mfumo wa utawala.

Barani ulaya pia walifanikiwa kufanya mapinduzi ya kimfumo kwenye utawala. Waliachana na mfumo wa kidikteta kwa baadhi ya mataifa na kuanza mfumo wa kidemokrasia. Hapa tunaona mfano french revolution nakadhalika.


Faida za mapinduzi hayo ambazo zinafanania na sababu za kuleta maendeleo kwenye jamii yoyote ile

(i). Miundombinu bora yenye ufanisi na kuwezesha shughuli za mawasiliano na usafirishaji.

Hapa tunaangazia barabara, usafiri wa anga, njia za reli, usafirishaji wa majini na mawasiliano kwa ujumla. Hivi vyote hurahisisha shuhuli za uzalishaji na kuchochea maendeleo


(ii). Uongozi bora katika jamii.

Ili jamii yoyote ipate maendeleo lazima iwe na viongozi bora wenye kutambua na kuongoza vema taifa au jamii na kusimamia maslahi na utekelezaji wa miradi na huduma za kimaendeleo.
Mfano viongozi lazima wawe na sifa zoote za kiongozi bora, wasiwe wala rushwa, wawe wavumilivu na waaminifu, wazalendo na wawajibikaji.

(iii). Elimu bora yenye kutuletea wataalamu mbalimbali.
Pia taifa lolote ili lipate maendeleo lazima liwe na mfumo bora wa elimu itakayo saidia kuzalisha au kutengeneza wataalamu wa idara zote. Hapa mfano wahandisi, waalimu, watu wa afya, mafundi, wanasayansi, wataalamu katika kilimo, wataalanu katika michozo na burudani nakadhalika. Yote hii itarahisisha kupata nguvu kazi kutoka kwa watu wa taifa husika.

(iv). Idadi ya watu iongezeke.
Pia lazima tuwe na idadi kubwa ya watu ambao hao ndio nguvu kazi ya taifa letu. Hivyo hasi lazima tuboreshe huduma za kiafya, elimu za uzazi ili kupunguza idadi kubwa ya wanaofariki. Hii itasaidia pia kupata soko la ndani katika uzalishaji wa mazao na bidhaa za viwandani.

(v). Matumizi sahihi na bora ya rasilimali tulizonazo.
Pia ili tupate kupiga hatua kimaendeleo lazima tuzitumie rasilimali zetu kwa manufaa ya taifa kwa ubora na usahihi utakao tupatia maendeleo. Mfano wa rasilimali zetu nchini ni madini, makaa ya mawe, mafuta kama yakigundulika, milima moja wapo mlima Kilimanjaro na aridhi pia tuliyonayo.

(vi). Hali ya hewa iliyopo nchini.
Nchi yetu imebahatika kupata kuwa na aina tofauti za hali ya hewa mfano kuna ukanda unakua na baridi, joto na hali ya kawaida. Hii husaidia ustawishaji wa mazao tofauti tofauti nchini yatakayo saidia kukuza kilimo na biashara.

(vii). Sayansi na teknolojia itumike katika shughuli zote za uzalishaji. Mfano uboreshaji wa mbegu na zana za kilimo , viwandani pia.

Yafuatayo ni mambo yanayokuwa kikwazo katika maendeleo ya jamii yoyote ile.

(i). Ubaguzi uwe wa kijinsia, kidini kikabila au kimaeneo.

(ii). Uongozi mbovu au usimamizi mbovu.

(iii). Kukosa wataalamu wa ndani na kutegemea wataalamu wa nje tu.

(iv). Miundo mbinu mibovu

(v). Kutokubali mawaza mbadala. Hususani kwa viongozi wetu miaka nenda suala la kukosoana lina onekana ni uadui. Hatuwezi kuwa bora bila kukosoana na kuongezeana fikra tofauti tofautim

(vi). Kutokujali haki za binadamu. Hili nalo ni.tatizo hususani nchi zetu za Afrika watawala wengi hawajali haki za raia wao kitu kinachopelekea wawekezaji kuogopa kuwekeza na kutilia mashaka juu ya usalama wao.

(vii). Kukosa viongozi wenye maono katika kuliendeleza taifa. Taifa lolote lazima liwe na viongozi wenye maono kimaendeleo. Mwl Nyerere aliwahi kusema tuna maadui wa kubwa watatu ambao ni umaskini, ujinga, na maradhi bado nchi yetu haijawa na huduma bora jambo.linaloongeza umasini.

Hitimisho.

Nimeonesha kwa uchache mapinduzi yaliyotokea barani ulaya ambayo yamepelekea wao kupiga hatua kimaendeleo katika jamii zao. Hivyo hasi jamii zetu za bara la Afrika hatuna budi kutekeleza mapinduzi hayo hususana kwenye, kilimo nchini, mfumo wa kuongoza nchi zetu, mifumo ya elimu zetu, sayansi na teknolojia na mapinduzi ya viwanda. Asilimia kubwa ya bishaa tunazotumia nchini huzalishwa mataifa ya ughaibuni hilo liangaliwe kwa upana bila kujali maslahi ya watu wachache au kikundi fulani.

Yapo mengi ila hapa nimetoa kidogo ya yale mengi
 
Shida bado kuna yule adui alotajwa na Mwl nyerere anayeitwa ujinga huyu yupo saana humu nchini kwa idadi kubwa ya wananchi.
Mimi sijui kama ni uzembe ama ni mkakati watu wabaki na ujinga ,, Jamiiforums imeanzishwa muda mrefu sana na watu wamekua wakishauri Sana nini kifanyike tukomboe elimu yeti,lakini hakuna kinachofanyika,, sijui ni PRIDE hawataki kuonekana wamekopi mawazo kutoka Jamii Forum, kwa sababu itawafanya waonekane hawana creativity?

Lingine umegusia mapinduzi ya kilimo,mwenyewe ukiwa na nafasi tafuta humu uone jinsi watu walivyolipigia kelele hili swala hakuna kinachofanyika,,,topic za kushauri serikali saa nyingine naona ni kama wastage of time, inaishia kwenye makabati ya Jamiiforums
 
Mimi sijui kama ni uzembe ama ni mkakati watu wabaki na ujinga ,, Jamiiforums imeanzishwa muda mrefu sana na watu wamekua wakishauri Sana nini kifanyike tukomboe elimu yeti,lakini hakuna kinachofanyika,, sijui ni PRIDE hawataki kuonekana wamekopi mawazo kutoka Jamii Forum, kwa sababu itawafanya waonekane hawana creativity?

Lingine umegusia mapinduzi ya kilimo,mwenyewe ukiwa na nafasi tafuta humu uone jinsi watu walivyolipigia kelele hili swala hakuna kinachofanyika,,,topic za kushauri serikali saa nyingine naona ni kama wastage of time, inaishia kwenye makabati ya Jamiiforums
Kweli. Sema uongozi kuna haja ya kuongozwa na itikadi tofauti tofauti maana itasaidia mabadiliko kiutendaji zaidi na italeta ushindaji wa kweli katika kutekeleza malengo ya muda mfupi na mrefu.
 
Waweza kupiga kura kwa kulisoma andiko

Jinsi ya kupiga kura angalia picha inaonesha mwisho wa andiko kuna option ya vote
Polish_20210812_082721846.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kumbuka pia kuwa, wakati huo wao walipokuwa wanapitia hatua hizi, hapakuwa na vizingiti vingine kwao mbali na natural circumstances tu. Sisi kwa wakati huu inabidi tupambane na viwili, natural circumstances pamoja na upinzani kutoka kwa mahasimu wetu wa kisiasa na kiuchumi. Kazi sana
 
Kumbuka pia kuwa, wakati huo wao walipokuwa wanapitia hatua hizi, hapakuwa na vizingiti vingine kwao mbali na natural circumstances tu. Sisi kwa wakati huu inabidi tupambane na viwili, natural circumstances pamoja na upinzani kutoka kwa mahasimu wetu wa kisiasa na kiuchumi. Kazi sana
Mkuu bata wao kwa wao ushindani ulikuepo. Ukishaamua kuingia mfumo wa ubepari lazima ushindani uwepo maana ndio hali halisi ya mfumo huo. Walipigana vita wao kwa wao, walipitia magonjwa mengi mfano black death nk ila walipambana saana yaani kila tuwazalo walipitia wakapambana ndio maana wametuacha saana maana wana uzoefu mkubwa kila idara
 
Kumbuka pia kuwa, wakati huo wao walipokuwa wanapitia hatua hizi, hapakuwa na vizingiti vingine kwao mbali na natural circumstances tu. Sisi kwa wakati huu inabidi tupambane na viwili, natural circumstances pamoja na upinzani kutoka kwa mahasimu wetu wa kisiasa na kiuchumi. Kazi sana
Mkuu usisahau na kura yako hapa
 
Mkuu bata wao kwa wao ushindani ulikuepo. Ukishaamua kuingia mfumo wa ubepari lazima ushindani uwepo maana ndio hali halisi ya mfumo huo. Walipigana vita wao kwa wao, walipitia magonjwa mengi mfano black death nk ila walipambana saana yaani kila tuwazalo walipitia wakapambana ndio maana wametuacha saana maana wana uzoefu mkubwa kila idara
Kipindi hicho wao walikuwa kwenye level moja ya maendeleo, kila mmoja ndiyo alikuwa anaanza kutafuta. Tofauti na ilivyo kwa sasa, wao tayari walishaendelea na wana teknloloji kubwa sana wakati sisi hatuna.

Mjerumani kwa mfano, anasemekana kuwa anajua jiolojia ya Afrika nzima, wapi kuna madini na kiasi gani wakati sisi madini tunayo na hatujui kiasi tulichonacho kama vile wanavyojua wao. Inasemekana kuwa kwa sasa Tanzania hatuja-exhaust hata 10% ya resources za madini zilizopo chini kwenye ardhi, na inasemekana kuna baadhi ya sehemu ambazo kama utataka kuzi-ehaust, basi inabdii uwahamishe watu labda wakaishi hata baharini. Sasa unaweza ku-imagine kwamba una mali za kiwango hiki na kuna watu wana nguvu ambao wanajua kuwa unazo na wakati wewe ni mnyonge.

Miaka kama 100 mbele, kuna uwezekano watanzania wakaamua wenyewe kwa hiari yao kutawaliwa na angalau Taifa moja lenye nguvu ambalo litawasaidia kulinda rasilimali zao zsisiporwe, badala ya kuendelea kuwa huru halafu kila mmoja mwenye nguvu anakuja kuchukua kwa namna anavyopenda mwenyewe.

Bora mkawa mko chini hata ya taifa kama Marekani, halafu likasaidia kuzilinda raslimali zenu huku na lenyewe likitumia, kuliko mko huru halafu kila mmoja anakuja kujichotea kama anavyopenda mwenyewe. Mimi huwa na-foresee situation kama hiyo huko mbele ya safari. Kuna uwezekano ipo siku tutakuja kuamua kutawaliwa kwa hiari yetu wenyewe
 
Kipindi hicho wao walikuwa kwenye level moja ya maendeleo, kila mmoja ndiyo alikuwa anaanza kutafuta. Tofauti na ilivyo kwa sasa, wao tayari walishaendelea na wana teknloloji kubwa sana wakati sisi hatuna.
Mjerumani kwa mfano, anasemekana kuwa anajua jiolojia ya Afrika nzima, wapi kuna madini na kiasi gani wakati sisi madini tunayo na hatujui kiasi tulichonacho kama vile wanavyojua wao. Inasemekana kuwa kwa sasa Tanzania hatuja-exhaust hata 10% ya resources za madini zilizopo chini kwenye ardhi, na inasemekana kuna baadhi ya sehemu ambazo kama utataka kuzi-ehaust, basi inabdii uwahamishe watu labda wakaishi hata baharini. Sasa unaweza ku-imagine kwamba una mali za kiwango hiki na kuna watu wana nguvu ambao wanajua kuwa unazo na wakati wewe ni mnyonge. Miaka kama 100 mbele, kuna uwezekano watanzania wakaamua wenyewe kwa hiari yao kutawaliwa na angalau Taifa moja lenye nguvu ambalo litawasaidia kulinda rasilimali zao zsisiporwe, badala ya kuendelea kuwa huru halafu kila mmoja mwenye nguvu anakuja kuchukua kwa namna anavyopenda mwenyewe. Bora mkawa mko chini hata ya taifa kama Marekani, halafu likasaidia kuzilinda raslimali zenu huku na lenyewe likitumia, kuliko mko huru halafu kila mmoja anakuja kujichotea kama anavyopenda mwenyewe. Mimi huwa na-foresee situation kama hiyo huko mbele ya safari. Kuna uwezekano ipo siku tutakuja kuamua kutawaliwa kwa hiari yetu wenyewe
Shida ni kwamba hatuna mipango na hatujaamua kudhubutu katika kudadisi na viongozi wetu wanaruka hatua katika kutimiza malengo. Mfano china ilikua sawa na mataifa ya Afrika miaka ya nyuma nadhani lipo wazi lakn wenzetu waliwekeza kwa kutumia muda mwingi, mipango ya muda mrefu, kuboresha elimu kwa ajili ya.kutengeneza wataalamu mbalimbali.kwa dhumun la kukitegemea, pia uongozi wao.ukaweka sheria za kuilinda China na sio kumlinda mtu.mmoja. Ugonjwa wa Afrika hatuna viongozi wanaopenda kulinda nchi.zaidi ya kujilinda wao.na vyama vyao. Waambie watawala tuwe na katiba kama za wenzetu hata kama ya china ingekua tumenyonga viongozi wa ngapi kwa ubadhirifu wa mali za uma???

Njoo mfano mwingine japana ilipopigwa na U. S Hiroshima na Nagasaki walipata anguko kubwa saana katika uchumi wao.lakini walijua wafanye nini. Waliweka bajeti kubwa katika elimu wakapeleka vijana wao nje ya japani kujifunza mambo mbali mbali ili baadae warudi japani na kuikomboa nchi yao. Walifanikiwa saana wajapani kwa mipango.yao.

Mwaka 2018 japani ilitenga bajeti ya wizara ya Elimu tu ambayo inaizidi bajeti ya kwetu.

Tutaweza kupiga hatua ikiwa tutakubali kufanya maboresho katika kila.idara nchini.
 
Shida ni kwamba hatuna mipango na hatujaamua kudhubutu katika kudadisi na viongozi wetu wanaruka hatua katika kutimiza malengo. Mfano china ilikua sawa na mataifa ya Afrika miaka ya nyuma nadhani lipo wazi lakn wenzetu waliwekeza kwa kutumia muda mwingi, mipango ya muda mrefu, kuboresha elimu kwa ajili ya.kutengeneza wataalamu mbalimbali.kwa dhumun la kukitegemea, pia uongozi wao.ukaweka sheria za kuilinda China na sio kumlinda mtu.mmoja. Ugonjwa wa Afrika hatuna viongozi wanaopenda kulinda nchi.zaidi ya kujilinda wao.na vyama vyao. Waambie watawala tuwe na katiba kama za wenzetu hata kama ya china ingekua tumenyonga viongozi wa ngapi kwa ubadhirifu wa mali za uma???

Njoo mfano mwingine japana ilipopigwa na U. S Hiroshima na Nagasaki walipata anguko kubwa saana katika uchumi wao.lakini walijua wafanye nini. Waliweka bajeti kubwa katika elimu wakapeleka vijana wao nje ya japani kujifunza mambo mbali mbali ili baadae warudi japani na kuikomboa nchi yao. Walifanikiwa saana wajapani kwa mipango.yao.

Mwaka 2018 japani ilitenga bajeti ya wizara ya Elimu tu ambayo inaizidi bajeti ya kwetu.

Tutaweza kupiga hatua ikiwa tutakubali kufanya maboresho katika kila.idara nchini.
Napenda sana namna ulivyo positive kwenye fikra zako, na mimi pia ninapenda sana iwe kama unavyotamani wewe, ila uhalisia nikiuangalia unanipa picha nyingine tofauti. Katika hali kama hiyo, kitu pekee kinachoweza kufanya kazi ni muujiza wa mwenyezi Mungu. Tumeshafikia kwenye era ya zama za kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia ambazo haziruhusu tena tuweze kutoka kirahisi kama walivyowahi kutoka wenzetu waChina na waJapan. Hapa tulipo tu ndani ya jamii ya nchi yetu kwa sasa, kuna baadhi ni mamluki wapo kwa ajili ya lengo moja tu, kuhujumu utawala wa nchi ikiwa ni pamoja na Serikali iliyopo madarakani. Sasa mimi huwa najiuliza kwa hali hii namna ilivyo, tutatokatokaje hapa?
 
Napenda sana namna ulivyo positive kwenye fikra zako, na mimi pia ninapenda sana iwe kama unavyotamani wewe, ila uhalisia nikiuangalia unanipa picha nyingine tofauti. Katika hali kama hiyo, kitu pekee kinachoweza kufanya kazi ni muujiza wa mwenyezi Mungu. Tumeshafikia kwenye era ya zama za kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia ambazo haziruhusu tena tuweze kutoka kirahisi kama walivyowahi kutoka wenzetu waChina na waJapan. Hapa tulipo tu ndani ya jamii ya nchi yetu kwa sasa, kuna baadhi ni mamluki wapo kwa ajili ya lengo moja tu, kuhujumu utawala wa nchi ikiwa ni pamoja na Serikali iliyopo madarakani. Sasa mimi huwa najiuliza kwa hali hii namna ilivyo, tutatokatokaje hapa?
Ndugu naamini inawezekana ila kwa mipango ya muda mrefu, kuiweka Tanzania mbele na sio maslahi ya chama chochote cha siasa hili kwa kuweka sheria ambazo itabidi hakuna mtu yoyote atakua juu ya sheria hata raisi ikiwezekana awajibishwe akiboronga, kukubali na kuwekeza katika elimu namaanisha elimu iboreshwe serikali itenge majebi kubwa kwa ajili ya elimu ambayo utatupatia wataalamu wengi.

Kama.tunanunua ndege kwa mabilions cash lakin tunashindwa kuandaa vijana hata 500 tu wapelekwe hata nchi za ughaibuni kujifunza mambo muhimu afu waje na maujuzi yote na wakirudi wawezeshwe na wao wawe tayari kuitumikia nchi kwa ujuzi watakao pata. Sasa njoo angalia bajeti yetu kijana anaesoma huko shule za kata.aje kupambana na mchina au mjerumani wa kada sawa na yake akihitimu chuo..?

Tuna vijana mainjinia je wana ufanisi sawa na vijana wa nchi zingine???
 
Napenda sana namna ulivyo positive kwenye fikra zako, na mimi pia ninapenda sana iwe kama unavyotamani wewe, ila uhalisia nikiuangalia unanipa picha nyingine tofauti. Katika hali kama hiyo, kitu pekee kinachoweza kufanya kazi ni muujiza wa mwenyezi Mungu. Tumeshafikia kwenye era ya zama za kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia ambazo haziruhusu tena tuweze kutoka kirahisi kama walivyowahi kutoka wenzetu waChina na waJapan. Hapa tulipo tu ndani ya jamii ya nchi yetu kwa sasa, kuna baadhi ni mamluki wapo kwa ajili ya lengo moja tu, kuhujumu utawala wa nchi ikiwa ni pamoja na Serikali iliyopo madarakani. Sasa mimi huwa najiuliza kwa hali hii namna ilivyo, tutatokatokaje hapa?
 
Napenda sana namna ulivyo positive kwenye fikra zako, na mimi pia ninapenda sana iwe kama unavyotamani wewe, ila uhalisia nikiuangalia unanipa picha nyingine tofauti. Katika hali kama hiyo, kitu pekee kinachoweza kufanya kazi ni muujiza wa mwenyezi Mungu. Tumeshafikia kwenye era ya zama za kiuchumi, kisiasa na kiteknolojia ambazo haziruhusu tena tuweze kutoka kirahisi kama walivyowahi kutoka wenzetu waChina na waJapan. Hapa tulipo tu ndani ya jamii ya nchi yetu kwa sasa, kuna baadhi ni mamluki wapo kwa ajili ya lengo moja tu, kuhujumu utawala wa nchi ikiwa ni pamoja na Serikali iliyopo madarakani. Sasa mimi huwa najiuliza kwa hali hii namna ilivyo, tutatokatokaje hapa?
 
Back
Top Bottom