secret file
JF-Expert Member
- Sep 10, 2019
- 5,843
- 8,609
Mlipaswa muache kesi isikilizwe on merit..Bismillahir Rahmaanir Rahiim
SHURA YA MAIMAMU TANZANIA
LEO TAREHE 28.04.2021, SERIKALI IMEKATA RUFAA MAHAKAMA YA RUFAANI DHIDI YA MASHEIKH
Tarehe 23.04.2021, Mahakama Kuu ilitoa hukumu ya ushindi kwa Masheikh wa kesi 14, Kati ya 25, zilizokuwa zinawakabili Masheikh.
Baada ya uamuzi huo shauri lilipangwa liendelea leo kwa kusikilizwa kesi 11, zilizobaki.
Katika hali ya kuonesha nia ya serikali ya kuendelea na msimamo wake dhidi ya Masheikh hao leo hawakufika Mahakamani kama ilivuotarajiwa na badala yake wametuma hati ya kukata rufaa dhidi ya hukumu iliyowapa ushindi wa kesi 14, Masheikh.
Kufuati hatua hiyo shauri hilo litasitishwa kuendelea Mahakama Kuu mpaka litakapo sajiliwa Mahakama ya Rufani na kukapangiwa majaji wa kusikiliza na hatimaye kutolewa uamuzi.
Wito wa Shura ya Maimamu Tanzania kwa wananchi ni ule ule wa kuwa karibu na kesi hizi kubwa ili kuona na kupata fursa ya kutafakari mgumo wetu wa sheria, uongozi na mustakbali wa Taifa letu .
Ibrahim Z. Mkondo
Msemaji wa Shura ya Maimamu Tanzania.
0713118812*
msinge challenge hati za mashtaka kupelekea baadhi ya makosa kufutwa.....
mapungufu hayo mawakili wenu wangeyaleta kwenye final submission.....
ona sasa kesi haiendelei mpaka rufaa isikilizwe!!??