Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Kalamu,
Huko huko. Kama ndiko nyumbani basi kaa mkao wa kuhama. Maana rais kishasema afadhali wachimbe dhahabu kuliko kulima.
Mwanakijiji,
Hisa zao zinauzwa Toronto, New York na London. Mtanzania yeyote atakayekuwa na hisa huko ujue ana mkono mrefu---yaani kishaiba nyumbani kuwekeza kwenye kampuni hiyo. Huyu jamaa kamwajiri kijana wa George Kahama pale DSM na kila mara rais Kikwete anapokuja Marekani wanakutana. Sijui wana dili gani. Lakini kama alivyosema Dua, huyu ni kibaka wa kutupa mbali.
Wazo la kununua share ni zuri lakini linataka watu ambao wako committed ili kulifanikisha. Tunaweza kupata angalau Watanzania 10 000 ambao wanaweza kuwekeza lets say kila mmoja share 1000. Kwa hiyo kila mtu atakuwa na at least Canadian $ 6000 kwa bei ya leo ili kuifikia hiyo 2%. Mwanakijiji mimi naona tuanze kukusanya list tujipange kila mwezi kuanza kununua shares, tukijipa muda i.e. kila mwezi kununua share at least Canadian $ 200 kwa wanaojiweza zaidi wanunue zaidi nafikiri tutafanikiwa. Inabidi tuwe na Broker mmoja pale Toronto ili asituchaji bei mbaya kwa kila transaction. Target ikiwa minimum of 1000 shares kwa kuanzia.
Floated shares zipo 527 376 629. share ambazo ni outstanding ni 86 455 185. Ukitaka kuona zaidi symbol ya kampuni hii ni TNX. Bei ya leo Canadian $ 6.04 kwa share.
Inabidi tuangalie hizo outstanding shares pengine ndio kwa ajili ya wabongo inabidi kufuatilia hili.
Kichuguu
Nenda kwenye Toronto stock Exchange au FTSE ya hapa London halafu kuna sehemu wanauliza unataka share zipi utaona mahali wameandika jina la kampuni ausymbol ya kampuni. hapo weka TNX halafu utaona hizo bei za leo.
Au gonga hapa:http://uk.moneycentral.msn.com/investor/quotes/quotes.asp?Symbol=CA:TNX
Bila kuwa na nia ya ku-undermine hii move hebu wajameni tueleweshane hapa kaswali alikouliza Mwanasiasa' ni hisa kiasi gani zinahitajika kuwa kwenye board ya maamuzi?
Kichuguu
Nenda kwenye Toronto stock Exchange au FTSE ya hapa London halafu kuna sehemu wanauliza unataka share zipi utaona mahali wameandika jina la kampuni ausymbol ya kampuni. hapo weka TNX halafu utaona hizo bei za leo.
Au gonga hapa:MSN Deutschland | News, Wetter, Sport & Hotmail Login
MKJJ,
Nimeshindwa kusoma ripoti hii; nadhani lazime ni sign-in kwenye website yako.
Yaleyale ya Carl Peters na Chief Mangungo wa Msovero?Wajinga ndio waliwao.
Serikali ya awamu ya tatu ilifanya watanzania wote tuwe wajinga kwa hiyo hivi sasa tunaliwa kiulaini na huyu jamaa.
This thug cannot be our friend even a single minute; ni friend wa Mkapa, Sumaye, Kikwete na Lowassa. Wakati Kikwete alipokohoa kuwa anataka kupitia upya mikataba yote ya madini, akanyamazishwa.
Tanzania pale hatuna sheria kamili ya ardhi, bado ardhi nyingi ni mali ya Taifa. Yeye alivyopata haki ya kumilki ardhi yenye madini bado ni kitendawili kweli kweli. Huu ndio ule ukoloni uliojulikana miaka hiyo ya sabini kuwa ukoloni mamboleo. Zamani walikuja kwa na kutunyanganya ardhi kwa nguvu na ikilazimika kwa mtutu wa bunduki. Leo hii wanakuja na kuwalaghai viongozi wetu wapumbavu na kisha kutunyananya ardhi; tatizo la afrika limekuwa ni kwenye ardhi miaka nenda rudi. Ni kama vile sisi wenyewe hatujui matumizi ya ardhi nzuri.