James Sinclair: A Friend or Foe?

Kalamu,
Huko huko. Kama ndiko nyumbani basi kaa mkao wa kuhama. Maana rais kishasema afadhali wachimbe dhahabu kuliko kulima.
 
wazee ambao mko interested send me your email. Nitakuwa nawapatia vitu exclusive na tunaweza kuandika mengine ambayo hatuwezi kuyaanika hapa maana wanasema "kwenye kuku wengi...." I'll keep your contacts in strict confidence... mwanakijiji@journalist.com
 
Kalamu,
Huko huko. Kama ndiko nyumbani basi kaa mkao wa kuhama. Maana rais kishasema afadhali wachimbe dhahabu kuliko kulima.

Haki ya nani nitaua mtu atakayegusa kashamba kangu pale Kagunga.

Bila kuwa na nia ya ku-undermine hii move hebu wajameni tueleweshane hapa kaswali alikouliza Mwanasiasa' ni hisa kiasi gani zinahitajika kuwa kwenye board ya maamuzi?
Na vipi kama wazalendo wakifanikiwa kuitwaa kampuni hiyo halafu makuwadi wa soko huria wakainyang'anya hizo hati miliki?

Maana kupewa huko siyo kwa sababu ya nia njema bali ni kutokana na wao kutupiwa makombo na huyo mwivi, Kisha tukasikia "tuna tender upya hii kazi" iliyokuwa inafanywa na Sinclair.

Kisha hapo hapo anarudi Sinclair na kampuni nyingine may be this time Dowans Holding.
 
hivi maneno haya yana ukweli gani?

Mwanakijiji,
Hisa zao zinauzwa Toronto, New York na London. Mtanzania yeyote atakayekuwa na hisa huko ujue ana mkono mrefu---yaani kishaiba nyumbani kuwekeza kwenye kampuni hiyo. Huyu jamaa kamwajiri kijana wa George Kahama pale DSM na kila mara rais Kikwete anapokuja Marekani wanakutana. Sijui wana dili gani. Lakini kama alivyosema Dua, huyu ni kibaka wa kutupa mbali.
 
Wajinga ndio waliwao.

Serikali ya awamu ya tatu ilifanya watanzania wote tuwe wajinga kwa hiyo hivi sasa tunaliwa kiulaini na huyu jamaa.

This thug cannot be our friend even a single minute; ni friend wa Mkapa, Sumaye, Kikwete na Lowassa. Wakati Kikwete alipokohoa kuwa anataka kupitia upya mikataba yote ya madini, akanyamazishwa.

Tanzania pale hatuna sheria kamili ya ardhi, bado ardhi nyingi ni mali ya Taifa. Yeye alivyopata haki ya kumilki ardhi yenye madini bado ni kitendawili kweli kweli. Huu ndio ule ukoloni uliojulikana miaka hiyo ya sabini kuwa ukoloni mamboleo. Zamani walikuja kwa na kutunyanganya ardhi kwa nguvu na ikilazimika kwa mtutu wa bunduki. Leo hii wanakuja na kuwalaghai viongozi wetu wapumbavu na kisha kutunyananya ardhi; tatizo la afrika limekuwa ni kwenye ardhi miaka nenda rudi. Ni kama vile sisi wenyewe hatujui matumizi ya ardhi nzuri.
 
Wazo la kununua share ni zuri lakini linataka watu ambao wako committed ili kulifanikisha. Tunaweza kupata angalau Watanzania 10 000 ambao wanaweza kuwekeza lets say kila mmoja share 1000. Kwa hiyo kila mtu atakuwa na at least Canadian $ 6000 kwa bei ya leo ili kuifikia hiyo 2%. Mwanakijiji mimi naona tuanze kukusanya list tujipange kila mwezi kuanza kununua shares, tukijipa muda i.e. kila mwezi kununua share at least Canadian $ 200 kwa wanaojiweza zaidi wanunue zaidi nafikiri tutafanikiwa. Inabidi tuwe na Broker mmoja pale Toronto ili asituchaji bei mbaya kwa kila transaction. Target ikiwa minimum of 1000 shares kwa kuanzia.

Floated shares zipo 527 376 629. share ambazo ni outstanding ni 86 455 185. Ukitaka kuona zaidi symbol ya kampuni hii ni TNX. Bei ya leo Canadian $ 6.04 kwa share.

Inabidi tuangalie hizo outstanding shares pengine ndio kwa ajili ya wabongo inabidi kufuatilia hili.


TNX ni CBOE 10-Year Treasury Yield Index. Mimi huwa natafuta stocks kwa kupitia website hii http://www.marketwatch.com/ Nimejaribu kutafuta hiyo ya TNX sikuiona kama inahusiana chochote na Tanzania. Hebu mwenye kujua symbol kamili ya hii kampuni atuambie.
 
Kichuguu

Nenda kwenye Toronto stock Exchange au FTSE ya hapa London halafu kuna sehemu wanauliza unataka share zipi utaona mahali wameandika jina la kampuni ausymbol ya kampuni. hapo weka TNX halafu utaona hizo bei za leo.
 
Tabasamu

Bila kuwa na nia ya ku-undermine hii move hebu wajameni tueleweshane hapa kaswali alikouliza Mwanasiasa' ni hisa kiasi gani zinahitajika kuwa kwenye board ya maamuzi?

Huwezi kujua nini kinaendelea kwenye kampuni hii kwani wamekuwa wasiri sana; i.e. hata report yao ya mwaka huwezi kuiona mpaka uwe na share kwa hiyo huwezi kujua nani anavuta kamba.

Ngoja mie nitanunua some shares nianze kujua kulikoni na nani ana nini. Itabidi tuvute subira kwa hili lakini mimi nitanunua tu maana nataka kujua nini kinaendelea hapo.

Nikisha nunua nitafahamu nani ana nini na kiasi gani?
 
ninavyojua mimi makampuni yanatofautiana lakini kama kampuni iko listed in UK then ni rahisi ukiwa na shares za paundi kumi basi uko entitled kupata taarifa zote za kampuni

sasa mlioko UK mna siku mbili tuu kwani ni muhimu kumuuliza rais akija huko kuhusu hili

kwa taarfa zaidi basi mnaweza kuingia hapa

http://www.londonstockexchange.com/en-gb/pricesnews/prices/priceshelp/


http://www.fsa.gov.uk/

na kama kampuni iko lREGISTERD in UK basi ni rahisi nadhani unatakiwa kulipia kiasi kidogo tu kupata info zote kuhusus kampuni

bofya hapa:

http://www.companieshouse.com/


na kama hiyo kampuni inatuhuma za unyanyasaji basi mseme kwani ni rahisi kuwaasemea kwa wabunge wao na kuna website maalum ambayo unaweza kumwaga upupu wote kuhusu hiyo kampuni pamoja na watendaji wake

sasa mbaona hamjasema zaidi jinsi MTOTO WA GEORGE KAHAMA anavyohusiana na hawa jamaa?

kwani si alikuwa anafanya kazi pale UBALOZI WA UK-DAR?
 
Kichuguu

Nenda kwenye Toronto stock Exchange au FTSE ya hapa London halafu kuna sehemu wanauliza unataka share zipi utaona mahali wameandika jina la kampuni ausymbol ya kampuni. hapo weka TNX halafu utaona hizo bei za leo.

Au gonga hapa:MSN Deutschland | News, Wetter, Sport & Hotmail Login


Asante nimeipata; ninaweza kuiweka kwenye portfolio yangu Wall Street kwa kutumia symbol ya CA:TNX au TRE. Tatizo ni kuwa siwezi kupata taarifa kamili za kampuni kama vile analyst information, insider actions, financial reports na vitu kama hivyo. Hata hivyo nitajaribu kununua shares kadhaa hasa kwa vile bei yao ni nafuu kweli kwa share. Naona walianza kuuza share kwe bei ndogo sana chini ya dola moja, na bei yao imepanda haraka sana mwaka wa 2005 tu. Hebu ona chart yao hapa chini.

Website yao iko hapa; kuna mahali jamaa huyu anasema "
Tanzanian Mining Laws Model For Other African Countries," what a joke?

112d1171505749-james-sinclair-friend-foe-int-basic.chart.gif

int-basic.chart.gif
 
MKJJ,

Nimeshindwa kusoma ripoti hii; nadhani lazime ni sign-in kwenye website yako.
 
MKJJ,

Nimeshindwa kusoma ripoti hii; nadhani lazime ni sign-in kwenye website yako.

Mwl.Kichuguu,
Inafunguka hapo panapoonekana unahitajika kusaini usipatilie manani,scrol down utaona kuna sehemu mbili ya kudown load na ya open sasa click kwenye hiyo link ya kufungua utaweza kuisoma, inafunguka hata hivyo ni mpaka idownload lakini inafanya haraka.
 
Kichuguu, kuna kitu hujafanya sawa maana nimejaribu kusign out kila mahala na kuingia humu na kufungua hiyo link na nimeweza kuona. So, jaribu tena.. na kama watu wengine mna tatizo hilo hilo, basi nitabadilishe baadaye na kuweka kwenye site nyingine kuna habari nyeti kweli na za kushangaza!
 
Wajinga ndio waliwao.

Serikali ya awamu ya tatu ilifanya watanzania wote tuwe wajinga kwa hiyo hivi sasa tunaliwa kiulaini na huyu jamaa.

This thug cannot be our friend even a single minute; ni friend wa Mkapa, Sumaye, Kikwete na Lowassa. Wakati Kikwete alipokohoa kuwa anataka kupitia upya mikataba yote ya madini, akanyamazishwa.

Tanzania pale hatuna sheria kamili ya ardhi, bado ardhi nyingi ni mali ya Taifa. Yeye alivyopata haki ya kumilki ardhi yenye madini bado ni kitendawili kweli kweli. Huu ndio ule ukoloni uliojulikana miaka hiyo ya sabini kuwa ukoloni mamboleo. Zamani walikuja kwa na kutunyanganya ardhi kwa nguvu na ikilazimika kwa mtutu wa bunduki. Leo hii wanakuja na kuwalaghai viongozi wetu wapumbavu na kisha kutunyananya ardhi; tatizo la afrika limekuwa ni kwenye ardhi miaka nenda rudi. Ni kama vile sisi wenyewe hatujui matumizi ya ardhi nzuri.
Yaleyale ya Carl Peters na Chief Mangungo wa Msovero?
 
Again, we need to focus... so far nimepata watu watatu tu kwenye email ambao wako interested..! hatutafika. Wa ndugu kama tutaamua kufanya hivi it'll take angalau dola 500-1000 kuweza kununua shares...kwa kila mtu.. hatuna haraka...tukitaka kufanya hivi by June basi tujiandae.

How we gonna do that tutaamua. But the first thing is committment and if you think you can put aside that amount of money until June...Ukisave angalau $50.00 a week from March to the end of May you'll hava at least $650 na tukipata angalau watu 50 tu... we'll be able to invest about $32,500 sawa na karibu shilingi milioni 42!! Is that idealistic of course, is that overtly ambitious? absolutely! is it doable?

You betcha!! are there about 50 Tanzanians out there willing to do this in two days I got three!! Watanzania wangapi wako members hapa JF 808! ambao wako active? 270! kati ya hao waliotembelea leo peke yake hadi saa 3.00Asubuhi ni 52! now, you guys tell me.. am I too optimistic? probably.
 
Ili tuweze kufanikiwa, tusiwe na wasiwasi wa fedha kwanza... moyo na kujiandaa ndilo la msingi.

a. Tujue idadi ya Watanzania ambao wako tayari kuingia na kununua hisa (wapo tayari watanzania wenye hisa kwenye kampuni hiyo) tunataka kuhakikisha kuwa wengi wenye hisa kwenye kampuni hiyo kama mtu mmoja mmoja ni Watanzania

b. Tukishajua tuko wangapi ambao tuko tayari kuanza kuweka akiba ya kati ya dola 500 na 1000 basi tunakubaliana wakati muafaka wa kuamua hatua inayofuata.

Kama hatuwezi kupata angalau watu 50... it is not worthy it.

c. Tutajaribu kuwapata watu wa nico au tuf tuone kama na wenyewe wanaweza kuwa wana hisa...

Pesa zinazochumwa nchini mwetu, zirudishwe kwetu.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom