GUSSIE
JF-Expert Member
- Dec 2, 2014
- 3,866
- 11,100
Mwenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi bwana James Mbatia akiongea na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Leo hii ametolea ufafanuzi wa mambo mbalimbali yaliyojitokeza kwenye hotuba ya Rais na kauli ya Spika Job Ndugai
Mosi, Suala la akiba ya pesa za kigeni ameiomba serikali wabadili kauli yao ya kuwa tuna dola za marekani bilioni elfu sita yaani kimahesabu ni trilioni sita, China tu kama Taifa lenye pesa nyingi za kigeni wana dola za marekani trilioni tatu tu
Mheshimiwa Mbatia amesisitiza mahesabu ni tatizo kubwa sana kwa viongozi wetu kwani hata pesa za mkopo wa uviko wanazojengea vyoo vya wanafunzi wanamshukuru Rais kwa msaada wakati hilo ni deni la Taifa, Hata Rais akiondoka kama alivyoondoka Magufuli na deni kubwa la Taifa, Deni la Taifa ameliacha kwa wananchi na serikali yao
Wananchi ndio watatakiwa kulipa madeni haya tena kwa pesa za kigeni, Hivyo James Mbatia anashangaa Rais kusema Tutaendelea kukopa bila kuangalia nani atalipa madeni haya ambayo pesa zake hazizalishi kitu, Mbatia amesisitiza ni lazima kuangalia uwezo wa wananchi kulipa madeni hayo
James Mbatia, Ni aibu kwa viongozi karne hii ya ishirini na moja kujenga vyoo kwa pesa za mkopo wa uviko halafu wanaandika kwenye ukuta wa Choo "Ahsante uviko 19" kama jambo la Furaha kumbe ni vichekesho
James Mbatia, Ni aibu viongozi wa serikali toka ngazi ya Taifa mpaka kata kila wakati kusema ahsante Rais umetoa pesa za flyover, mara barabara mara afya wakati ni pesa za watanzania na hata kama ni mkopo ni deni la watanzania. Rais yeye hana pesa za kujenga barabara au flyovers labda kama Rais anauza madawa ya kulevya
Pili, Ni upunguani umeshajijenga na tunazidi kuharibu watoto wa Taifa hili kutokana na upunguani wa viongozi wetu ambao wanashindwa kuelewa maana ya mkopo na deni la Taifa, James Mbatia amesisitiza baada ya watu kujibu hoja za Job Ndugai wao wanatafuta personal attack kwa Ndugai
James Mbatia, Anasisitiza upunguani wa viongozi ndio unapelekaea watu kushindwa kujibu hoja na kukimbilia kumtukana Job Ndugai, Tatizo la upunguani linawafanya viongozi washindwe kupima hoja kama Job Ndugai amekosea, Je usahihi ni upi amehoji bwana Mbatia
Tatu, James Mbatia amesisitiza somo la hesabu hata Bungeni ni tatizo kwa wabunge wengi sana, Ndio maana mambo yanaposomwa kuhusu hesabu wengi hawaelewi, James Mbatia amesisitiza Kuwa viongozi wanaandaliwa
Mosi, Suala la akiba ya pesa za kigeni ameiomba serikali wabadili kauli yao ya kuwa tuna dola za marekani bilioni elfu sita yaani kimahesabu ni trilioni sita, China tu kama Taifa lenye pesa nyingi za kigeni wana dola za marekani trilioni tatu tu
Mheshimiwa Mbatia amesisitiza mahesabu ni tatizo kubwa sana kwa viongozi wetu kwani hata pesa za mkopo wa uviko wanazojengea vyoo vya wanafunzi wanamshukuru Rais kwa msaada wakati hilo ni deni la Taifa, Hata Rais akiondoka kama alivyoondoka Magufuli na deni kubwa la Taifa, Deni la Taifa ameliacha kwa wananchi na serikali yao
Wananchi ndio watatakiwa kulipa madeni haya tena kwa pesa za kigeni, Hivyo James Mbatia anashangaa Rais kusema Tutaendelea kukopa bila kuangalia nani atalipa madeni haya ambayo pesa zake hazizalishi kitu, Mbatia amesisitiza ni lazima kuangalia uwezo wa wananchi kulipa madeni hayo
James Mbatia, Ni aibu kwa viongozi karne hii ya ishirini na moja kujenga vyoo kwa pesa za mkopo wa uviko halafu wanaandika kwenye ukuta wa Choo "Ahsante uviko 19" kama jambo la Furaha kumbe ni vichekesho
James Mbatia, Ni aibu viongozi wa serikali toka ngazi ya Taifa mpaka kata kila wakati kusema ahsante Rais umetoa pesa za flyover, mara barabara mara afya wakati ni pesa za watanzania na hata kama ni mkopo ni deni la watanzania. Rais yeye hana pesa za kujenga barabara au flyovers labda kama Rais anauza madawa ya kulevya
Pili, Ni upunguani umeshajijenga na tunazidi kuharibu watoto wa Taifa hili kutokana na upunguani wa viongozi wetu ambao wanashindwa kuelewa maana ya mkopo na deni la Taifa, James Mbatia amesisitiza baada ya watu kujibu hoja za Job Ndugai wao wanatafuta personal attack kwa Ndugai
James Mbatia, Anasisitiza upunguani wa viongozi ndio unapelekaea watu kushindwa kujibu hoja na kukimbilia kumtukana Job Ndugai, Tatizo la upunguani linawafanya viongozi washindwe kupima hoja kama Job Ndugai amekosea, Je usahihi ni upi amehoji bwana Mbatia
Tatu, James Mbatia amesisitiza somo la hesabu hata Bungeni ni tatizo kwa wabunge wengi sana, Ndio maana mambo yanaposomwa kuhusu hesabu wengi hawaelewi, James Mbatia amesisitiza Kuwa viongozi wanaandaliwa