mbingunikwetu
JF-Expert Member
- Feb 17, 2015
- 13,663
- 18,037
Mtu unaweza kumfanyia jambo baya mwenzako halafu unasahau. Ukifika wakati wa kuvuna uovu uliopanda mtu hulalamika sana na kutafuta huruma kwa watu!! Lakini ni wazi kuwa Mbatia alishiriki kumng'oa Mrema pale NCCR Mageuzi akishirikiana na wenzake!! Alichokifanya kinamrudia. Namshauri aende kuomba radhi kwa Mrema kwanza.
Kumbukeni pia Sharif Hamad (marehemu) alishiriki kumtoa Mapalala (mwanzilishi wa CUF) pale CUF tena kwa kumdhalilisha mno. Yaliyomtokea Sharif Hamad pale CUF naye kujikuta ametolewa kwa hila na yule mnyamwezi wa Tabora (aliyetengua barua ya kujiuzulu) wote bado tunayakumbuka.
Wazungu husema "what goes around comes around). Mbatia asishangae yanayomkuta, ni mavuno halali ya upandaji wake katika siasa, kama ambavyo Sharif Hamad naye alivuna kwa stahili yake mapando aliyopanda katika sisa.
Ni onyo pia kwa chama kikongwe!! kitafakari kinavyopanda kwenye siasa.
Kumbukeni pia Sharif Hamad (marehemu) alishiriki kumtoa Mapalala (mwanzilishi wa CUF) pale CUF tena kwa kumdhalilisha mno. Yaliyomtokea Sharif Hamad pale CUF naye kujikuta ametolewa kwa hila na yule mnyamwezi wa Tabora (aliyetengua barua ya kujiuzulu) wote bado tunayakumbuka.
Wazungu husema "what goes around comes around). Mbatia asishangae yanayomkuta, ni mavuno halali ya upandaji wake katika siasa, kama ambavyo Sharif Hamad naye alivuna kwa stahili yake mapando aliyopanda katika sisa.
Ni onyo pia kwa chama kikongwe!! kitafakari kinavyopanda kwenye siasa.