James Mbatia: CHADEMA wamenifanyia fujo kwenye chama changu na jimboni kwangu wakati wote tupo UKAWA, ulisikia nalalamika?

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,890
Salaam Wakuu,

Kuna kipande kidogo cha video kinasambaa Mtandaoni, James Mbatia Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi akielezea kusikitishwa kwake na wanaomuona kwamba anavunja nguvu upinzania.

Hapa chini nmenukuu kile alichokiongea na kukiandika hapa chini.

Ameanza kwa kusema:

1591337059154.png


"Mimi ni Mbunge wa Vunjo, umewahi kunisikia nalalamikia labda CHADEMA kwanini wameweka Mgombea kule Vunjo?

Niwe mkweli tu. Uchaguzi mkuu mwaka 2015 vyama Vingine viliweka Wagombea na wao tumo ndani ya UKAWA tukagawana zile kura za Madiwani CCM ikashinda, ulisikia nmelalamika?

Mwaka juzi nlimwambia Naibu Katibu Mkuu Bara Elizabeth kawaulize Washirika Wenzetu kwanini wanafanya fujo kule Vunjo? Alipowauliza wakasema Mbatia amezoea kudekadeka sana. Ulisikia nalalamika popote?

Ni haki yao na ni haki ya chama kilicho sajiliwa kina haki ya kufanya kazi mahali popote pale.

Mwasisi namba moja wa NCCR Mageuzi mwenye chama Mabere Nyaucho Marando alihamia CHADEMA ulisikia nalalamika popote? Kwanza nliulizwa nikawambia namtakia kila la heri, ni haki yake. Mwesigwa Baregu, ni haki yake.

Nakuhakikishia ukweli wa Mungu Chacha Wangwe akiwa Diwani wa NCCR Mageuzi Tarime Mjini 2003, walienda Viongozi wa CHADEMA wakamchukua wakamfanya Mwenyekiti wa Mkoa wa CHADEMA na wakati yupo NCCR Mageuzi na hatukumfukuza chama. aliendelea kuwa DIWANI"

Mwisho wa kumnukuu.

MY TAKE:
Vya vya siasa vya Tanzania vimetawaliwa na UBINAFSI, KIBURI, KUJIONA BORA na JICHO KWENYE FEDHA ZA BURE.
 
CHADEMA ni kundi la wapigaji. Hawahitaji siasa kuwasaidia wananchi ni biashara. Wana viongozi wenye Busara ndogo. Ktk jamii zote, wizi ni kosa lisilokubalika, lakini eti M/kiti wa CHADEMA akiambiwa kaiba, busara ni kunyamaza halafu, anajibiwa na wanaomuunga mkono. Uzuri mwaka huu kuna kila dalili wanapigwa chini!
 
Ukweli hutuweka huru kuna wakati hata Mimi nashindwa kuwaelewa Chadema wanahitaji nini katika siasa za upinzani.Wakati ule wa ukawa kuna maeneo mengi ya majimbo ambayo waliweka makubaliano lakini Chadema waliendelea kukiuka na kuweka wagombea wao hata kama Chadema haikuwa na nguvu mfano Jimbo la Mtama.Vyama vya upinzani havina Nia thabiti ya kushika dora,na tuchukulie uchaguzi wa mwaka huu wakashinda watashindwa kupata watu makini wa kuendesha serikali kwa uaminifu.Wapinzani wengi tuliowaamini wameunga juhudi mkono sasa unajiuliza kuna upinzani kweli au ni waganga njaa tuu...!!!?
 
Sikukusikia mzee wangu. Endelea na kujenga chama chako.
 
Mbatia anabanwa sehemu moja tu, kwanini hayo yote anayolalamika alifanyiwa na Chadema hakusema wakati ule? au aliamua kusubiri na wewe alipe kisasi?!

Sasa leo kinacho-trend about him ni makubaliano yake aliyoingia na Magufuli, kuiba wabunge na madiwani wa Chadema, hayo ya 2003... angeyasema 2003 angeeleweka.
 
Ktk jamii zote, wizi ni kosa lisilokubalika, lakini eti Mkiti wa CAHDEMA akiambiwa kaiba, busara ni kunyamaza halafu, anajibiwa na wanaomuunga mkono.
Historia ndio itakayomsafisha Mbowe.
Katika maisha unapokuwa unarushiwa tuhuma za uzushi hadharani hata kwa mayowe na kujiliza kwa machozi ya kukamua, busara ni kuwanyamazia.

Ni wazi kuwa wasiokupenda hawatasikiliza kujitetea kwako. Lakini la msingi zaidi ni kuwa wanaokuamini hawatasikiliza huo uzushi wao, na ndio watasimama kukutetea.

Hali hii itawafanya wazushi na wapambe wao kama MAFARISAYO, waanze 'kutafuta na kuombana' ushahidi/vielelezo kama ilivyo sasa.
Kwa vile uongo huwa hauna uwezo wa kukimbia kwenda mbali, huo ndio utakuwa mwisho mwema wa takataka hizo. Amen.
 
CHADEMA ni kundi la wapigaji. Hawahitaji siasa kuwasaidia wananchi ni biashara. Wana viongozi wenye Busara ndogo. Ktk jamii zote, wizi ni kosa lisilokubalika, lakini eti Mkiti wa CAHDEMA akiambiwa kaiba, busara ni kunyamaza halafu, anajibiwa na wanaomuunga mkono. Uzuri mwaka huu kuna kila dalili wanapigwa chini!

Sio kwa kura, bali matumizi mabaya ya madaraka. Tunaoikubali cdm tupo wa kutosha, na hatudanganyiki. Ile 1.5t mpaka leo bado inatuuma.
 
"Alipowauliza wakasema Mbatia amezoea kudekadeka sana. Ulisikia nalalamika popote?"
๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿค—๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚
 
Injinia Mbatia ule mpango wako wa kutengeneza barabara jimbo lako lote la vunjo umeishia wapi? Nakumbuka ulichangisha wapiga kura wako na zikapatikana bilioni za kutosha ila hadi leo kimya. Tuliishia kuona mapicha ya magreda na maaskofu tu huku mitandaoni.

Zile bilioni saba na ushee za kujenga barabara vunjo ziko wapi?
 
Back
Top Bottom