Kwa namna alivyonogewa na hicho cheo, sijui kama ataupokea huu ushauri wako kwa mikono miwili! Nadhani atachagua tu kufa na tai yake shingoni. 😇
 
Kutembea na escort ya king'ora ndani ya kiyoyozi kuna raha yake, asikwambie mtu. Mzee atakaa mpaka dakika ya mwisho kuomba Majaaliwa (kama jina lake) ya Mungu.
 
Baada ya Mh. Rais Samia kumteua Bw. Mpango aliyekuwa waziri wa fedha katika serikali ya Magufuli ni vema ukaonyesha mfano kwa wewe na Baraza zima la mawaziri mkajiuzulu ili kumpa Rais Samia wigo mpana zaidi wa kuunda serikali yake. Sasa hivi mnamlazimisha Mh. Rais kuziba kiraka cha Mpango katika wizara ya fedha tu na ninyi kubaki katika nafasi zenu.

Kujiuzulu kwako haina maana hawezi kukuteua tena bali ni kulinda heshima yako na ukiteuliwa tena itakupa wewe uhalali wa kufanya kazi zako kwa uhuru zaidi. Kuendelea kung'ang'ania hiyo nafasi kunaweza kusababisha ukaondolewa kwa fedheha.
Hapo patamu maana alishasahau bei umeme, maji, petrol, chakula, mavazi n.k shida anaziona kwenye tv pekee
 
Tufuate Katiba. Si vizuri kwa nafasi zote za juu kuwa na Watu wapya. Nimesikia Rais Samia SH akisifiwa leo alivyo tuongoza vizuri kipindi cha Msiba. Hivi hizi sifa ni za Mh Rais peke yake au ni team mzima. Mh Rais na Makamu wake kama wanafikiri ni afya kwa kumtoa PM na kuvunja Baraza la Mawaziri na Wafanye hivyo. Ila ingekuwa vizuri wakajaza nafasi kwa Umakini ya Wizara ya Fedha. Na wakaendelea na Baraza lililopo halafu wakawapa matarajio yao. Atakaye shindwa kutumbua kuhusike.

Nchi hii imetikiswa vya kutosha na msiba wa Hayati JPM tusiitikise tena kwa taama za watu kutafuta vyeo.

Mbatia anataka ubunge wa viti maalumu kwa hiyo naye kasema asikike.
 
Majaliwa amekaa kishari sana utafikiri amepewa hati miliki ya kuwa waziri mkuu milele wakati cha maana anachokifanya hata hakionekani
 
Mnampotosha huyu mama, mnatafutia vita huyu mama CCM ni hile hile na watu ni wale wale au mnataka akalete mawaziri Zanzibar kwao?

yeye ni Vp Hilo balaza la mawaziri wakati linaundwa si alikuepo kwenye huo utawala
Hujawajua hawa watu wanataka nini? Wanajalibu kubahatisha kama mama atapovunja baraza la mawaziri labda mama anaweza kuwakubuka kwenye teuzi
 
Kabisa ili mama aongoze nchi bila kufunikwa na kivuli cha Magufuli, inabidi avunje hilo baraza haraka. Ma hata hao mawaziri hilo wanalijua, lakini wanalazimisha kuwepo ili kumtisha huyo mama asiwaguse. Na kwenye kuunda baraza lake ahakishe Majaliwa, Kabudi, Mwigulu na Jafo wasiwepo. Wale wate waliokuwa wanajipendekeza wazi wazi kwa Magufuli awapige chini haraka maana ndio watamkwamisha. Hao waliokuwa mawaziri wa wizara nyingine, awageuze kuwa manaibu mawaziri.
ACHA WIVU NA CHUKI UTAKUFA MASIKINI
 
Mhe:Rais Mama yetu Samia Suluhu Hassan chondechonde vunja baraza lote la mawaziri. Teua wachapa kazi na Waape kiapo cha utii mbele yako. Pia nakupongeza kwa uteuzi wa Dr. Philip Isdory Mpango kuwa Makamu wa Rais. Pia nakupongeza kwa kuanza vizuri na ATCL, TPA na BOT/HAZINA.

Tembea zaidi TAMISEMI, TRA, LOAN BOARD (HESLB), Mpe msimamo Speaker wa Bunge Job Ndugai wito wa kuwaondoa Wabunge hewa19, Fanya Special Auditing ya Miradi mikubwa ya JPM hata Ubungo Interchange, Busisi Bridge, Nyerere Hydro Power Project, na mwisho toa Ajira mpya.

Mungu akulinde na akuongoze Mama. Kila la Kheri.
Naona Sasa wafanya kazi wanaanza kupangia boss cha kufanya au mnataka avunje baraza nanyi awakumbuke kwenye teuzi?
 
Baada ya Mh. Rais Samia kumteua Bw. Mpango aliyekuwa waziri wa fedha katika serikali ya Magufuli ni vema ukaonyesha mfano kwa wewe na Baraza zima la mawaziri mkajiuzulu ili kumpa Rais Samia wigo mpana zaidi wa kuunda serikali yake. Sasa hivi mnamlazimisha Mh. Rais kuziba kiraka cha Mpango katika wizara ya fedha tu na ninyi kubaki katika nafasi zenu.

Kujiuzulu kwako haina maana hawezi kukuteua tena bali ni kulinda heshima yako na ukiteuliwa tena itakupa wewe uhalali wa kufanya kazi zako kwa uhuru zaidi. Kuendelea kung'ang'ania hiyo nafasi kunaweza kusababisha ukaondolewa kwa fedheha.
pambana atakukumbuka kwenye teuzi!
 
Wakati unampigia kura magufuli,ni wakati huo huo ulimchagua na Makamu wake.
basi sawa Kama mambo yapo vile PM Hana ulazima wa kujiuzulu,tulishajua mnachotaka baraza livunje ili nanyi awakumbuke kwenye teuzi
Si ndio hicho mnachotaka?
 
Back
Top Bottom