msaragambo
Senior Member
- Aug 6, 2008
- 127
- 17
Much Respect Mkuu........
Sasa kama Kambona aliwapa heshima wenzie kwa kuwaita "Baba", mbona yeye hakupewa heshima hiyo na kuishia kuitwa "Mwanamke" kinyume na jinsia yake, rejea wimbo huu wa jeshini, taasisi ya umma, na mchakamchaka mashuleni!
"Kambona kaolewa, wapi?, ulaya...... wivu wamkereketa?
Mimi kinachonisikitisha, kama msomi na mfuasi wa historia, ni miaka ambayo Kambona aliishi Uingereza. Mbona hakuandika chochote? Ni kama baada ya kufika Uingereza hakuona umuhimu wa kuweka kumbukumbu zake kuhusu tofauti alizokuwa nazo na Kambarage. Hii kwangu was a great disservice to the country. Sisemi kwamba angeandika mwenyewe, lakini kulikuwa na venues nyingi tu za kutoa maoni yake na vision na kuwaachia Watanzania picha nyingine.Kambona was a thinker in his own right.Ukimsoma vizuri anaonekana kuwa mtu wa kujiamini sana.Alikuwa mkweli na muwazi na siyo muoga,mtu wa kushikiwa akili.Kiongozi mkubwa kama yeye anafikia kuruhusu wananchi wamkosoe hadharani,basi inawezekana pia alikuwa muadilifu(hakukimbia na sanduku la manoti!) na mchapakazi.Sijui ingekuwaje kama jamaa ndiye angeshika mpini badala ya Nyerere?<br>Mwanakijiji;Una hotuba yake aliyoitoa Nigeria,baada ya Nyerere ku support Biafra war?Kama una nondo nyingine za Kambona,tumwagie mkuu sisi kizazi cha Mkapa tufanye comparison na tuliyoyasikia/tuliyodanganywa,hasa ugomvi wake na Nyerere!
A speech a man does not make. Nyerere leo tunamhukumu kwa vitendo vyake na wala si hotuba zake. Kwa hiyo si sahihi kusema kuwa Kambona angekuwa kiongozi muwazi au mwenye kukubali kukosolewa kuliko Nyerere. Simply hatujui kwa sababu Kambona hakuwahi kulishika hilo jukwaa.After reading the speech, I came to conclude that Mr Kambona was very open, welcoming, humble and was even willing and ready to accept criticisms, something that Nyerere didn't like or was not comfortable with. Nyerere either didn't like or was rather sensitive when it comes to the idea of being criticised as a leader. Perhaps Nyerere was uneasy to see Kambona as an up and coming brilliant technocrat who was posing a threat of stealing the show within the party/country.
Huyo mzee zake zimeisha sasa anakabiliana na "Baba" wa kila kiumbe. Ana kazi kubwa kujibu jinsi gani aliwatawala wa Tz. Msitulazimishe kumuabudu huyo mzee...wakati umefika wa Tz kuangalia mbele. Kama kuchelewa yeye "Nyerere " ndio alituchelewesha... huo ubaba mnaompa ni kwenu nyinyi msihusishe kila mtz.
Mimi kinachonisikitisha, kama msomi na mfuasi wa historia, ni miaka ambayo Kambona aliishi Uingereza. Mbona hakuandika chochote? Ni kama baada ya kufika Uingereza hakuona umuhimu wa kuweka kumbukumbu zake kuhusu tofauti alizokuwa nazo na Kambarage. Hii kwangu was a great disservice to the country. Sisemi kwamba angeandika mwenyewe, lakini kulikuwa na venues nyingi tu za kutoa maoni yake na vision na kuwaachia Watanzania picha nyingine.
Nakubaliana nawe mkuu.Ingekuwa jambo jema sana kama Kambona angetuachia walau maandiko fulani kuhusu maono,fikra zake na tofauti zake na Nyerere.Binafsi naona hili limefanya pia ugumu wa upatikanaji wa ukweli hasa juu ya tofauti zake na Nyerere/kisa cha yeye kukimbia Tanzania.Ingekuwa raha sana leo kumsoma Kambona akiieleza Tanganyika/Tanzania aliyoitaka yeye!
Lakini pia hata baada ya kupata haya machache,naona kama Kambona alikuwa makini sana kiuongozi na alikuwa na ushawishi na labda alikuwa anakubalika sana miongoni mwa watanzania.Labda bifu ndipo lilipoanza hapa?
Nimeelimika sana! Now I can see that this guy was not that bad. Mnao mtetea mwalimu muitendee jamii nzima haki by giving credit where its due. This guy should also be apportioned a part of national heros status.
Wakati ule maoni ya Kambona au machapisho yake yasingeweza kupokewa Tanzania, na wala uhuru wa habari haukuwa mkubwa kiasi unachokiona sasa hivi. Nimawazo ya watu wachache/wasomi kama akina Abdulahaman Babu yaliweza kupenya kwenye magazeti kama "Africa" na baadae "Africa Now" na "Africa Events" lakini magazeti hayo yalikuwa ya nawafikia watu(wasomi)wachache sana. Kuna kitabu kiliandikwa na Abdulahamani Babu kinaitwa " African Socialism or Socialist Africa" ilikuwa ni vigumu sana kukipata japokuwa hakikupigwa marufuku. Kwahiyo uhuru wa mawazo tofauti haukuwa mkubwa sana enzi hizo. Wengine tunaishukuru sana mitandao ya kijamii kama hii na kukuwa kwa tekinolojia ya habari ambayo imetuletea uhuru mkubwa wakutoa na kupokea habari na mawazo hatakama kuna wanaotumia vibaya fursa hii. Zamani dola liliweza kudhibiti habari kisawasawa!Mimi kinachonisikitisha, kama msomi na mfuasi wa historia, ni miaka ambayo Kambona aliishi Uingereza. Mbona hakuandika chochote? Ni kama baada ya kufika Uingereza hakuona umuhimu wa kuweka kumbukumbu zake kuhusu tofauti alizokuwa nazo na Kambarage. Hii kwangu was a great disservice to the country. Sisemi kwamba angeandika mwenyewe, lakini kulikuwa na venues nyingi tu za kutoa maoni yake na vision na kuwaachia Watanzania picha nyingine.
Mumpambe mtakavyoweza, kwangu mimi Oscar Kambona ni msaliti kwa Taifa hili, simtofautishi na EL, kiongozi mwenyeuchu na tamaa ya mali na utajiri wa haraka haraka.
Sidhani kuna kumuabudu Nyerere bali ni ile heshima kama muasisi wa Taifa kama aalivyo Karume muasisi kule Zanzibar.Tusiwe tu wa kupinga UKWELI! Tupende tusipende atabakia kama KIONGOZI MAARUFU NA MWENYE MCHANGO MKUBWA SANA AFRIKA HATA KAMA "TANZANIA" MTALAZIMISHA KUMFUTA!!! Uzuri historia imeshaandikwa na hata wanaojaribu "kusahihisha" kwa kumpaka matope na kumchafua hawataenda mbali sana.
Nadhani, kwa wale wanaotaka kupata uelewa ukweli ni vizuri mjongelee historia with an open mind. Kuna extremes mbili ambazo tunakutana nazo sana. Moja ni ile ya kujaribu kumfuta Nyerere kabisa na mchango wake kwani watu wameshaamua kuwa he was the bad guy na wengine wote walikuwa ni wazuri. Upande wa pili wapo ambao wanaamini kuwa viongozi wote waliopingana na Nyerere au waliompinga Nyerere walikuwa sahihi. Hivyo, kwao Fundikira, Kambona, Tumbo, na wengine walikuwa sahihi simply because walitofautiana na Nyerere - haijalishi the substance of those differences.
Lengo moja la kuweka hotuba hii ni kudokeza tu kuwa hadi 1966 - Kambona hakuwa na tofauti kubwa sana ya msingi na Nyerere na wala yeye hakuwa na utata na nafasi ya Nyerere thus kumuita Baba wa Taifa na wale walioangalia clip ile ya JFK watakumbuka jinsi Nyerere alivyomtambulishi na kumshukuru kwa jina (he was the Minister of Foreign Affairs). Lakini vile vile watu wanaposoma historia wasije kujikuta wanaisoma nje ya "historical context". Hivyo, mojawaop ya changamoto za wasomi wetu ni kumuangalia Nyerere and his times in the context of history.
Je, mapinduzi na migogoro ya kisiasa katika nchi zilizoizunguka Tanzania na Afrika kwa jumla wakati ule ilitoka kwa watu walio mbali na watawala (watu baki)? Ghana, Nigeria vile vile Malawi, Congo, Kenya na Uganda ilikuwa ni migogoro ya watu ambao hawakuwa karibu na watawala? Je viongozi wa Afrika walikuwa salama kiasi gani kutoka kwa watu wa karibu yao? Je mataifa ya kigeni (hasa colonial and world power) walitumia nafasi gani kuwatambua na kuwaencorage watu wa karibu na watawala kuwa "mbadala"? Kesi za Misri ni mfano mmojawapo.
So, ni vizuri kumuangala Nyerer na Kambona na mambo yaliyotokea kati yao katika mwanga wa kihistoria. Vinginevyo, tunaweza kujikuta tunalazimisha historia isomeke namna moja - licha ya ushahidi wa kihistoria. Binafsi naamini kulikuwa na kitu zaidi ya tofauti za Azimio la Arusha kwani tunaona hata wale wanaosema Kambona hakutaka chama kimoja wanasahau kuwa uamuzi wa kwenda chama kimoja ulianzia 1963 na hoja zake zilianza mapema kabla ya uhuru - sijaona Kambona aki encourage upinzani mahali popote hadi pale alipojikuta yuko nje ya madaraka au madaraka yake yanatishiwa.
Nitafurahi kupata hotuba nyingine nyingi za Kambona au kiongozi mwingine yeyote wa zama za Nyerere ili tuweze kujenga historia nzuri na sahihi ya taifa letu.