Diason David
JF-Expert Member
- Aug 2, 2018
- 7,562
- 7,348
Ccc NAKWEDEPumbavu zake huyo DC!
Hata kama ni pesa zake lakini najisikia kumpangia matumizi.
Yaani kuna wahitaji kibao, halafu anampa jambazi
mxeweeeu DC
Nipooo
Kuna mchizi alikimbia alimpa mimba denti,ni wa huku kimbiji.
Ngoja nimwambie akajisalimishe anaweza kupewa na mke ili aache kuwafuata wanafunzi.
Ndivyo hivyo!Sasa ina maana kaachiwa huru?
Jambazi sugu aitwaye Ali Mtemi amejisalimisha katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya baada ya kukoswa koswa kuuwawa na Askari wa doria mara nne katika Wilaya ya Kigamboni huku baadhi ya wengine katika kikundi chake wakiuwawa na kukamatwa.
Polisi wamekuwa wakimsaka kwa muda mrefu ambapo amekuwa akijificha katika mikoa mbalimbali lakini hatimaye ameamua kujitokeza na kwenda kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni ili kuomba msamaha kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigamboni.
Ujasiri wake wa kujisalimisha umepongezwa na Kamati ya Ulinzi ya Ulinzi na Usalama, ambapo Mkuu wa Wilaya amemuahidi kumsaidia shilingi 1,000,0000 kama mtaji wa biashara baada ya kuahidi ameachana na ujambazi mbele ya wazazi wake na mjomba wake.
Mkuu wa Wilaya amemuomba akawe ni kioo kwa vijana wengine ambao bado wanafanya vitendo vya wizi na ujambazi katika Wilaya ya Kigamboni.
NB: Kumbe hata majambazi wanaogopa kifo!
Video ya jambazi sugu akijisalimisha kwa Mkuu wa Wilaya.
Mkuu wa Wilaya amemuahidi kumsaidia shilingi 1,000,0000 kama mtaji wa biashara baada ya kuahidi ameachana na ujambazi
Nadhani hafikishwi mahakamani na sidhani kama ni kiki za Uchaguzi kwa sababu tunaambiwa ''CCM hawana haja ya kufanya kiki ili wachaguliwe kwa sababu wanaiba kura''!Mahakamani anapelekwa lini?au kiki za uchaguzi maana CCM mna vijimambo.
Sasa tutaaminije hawaibi kama hakuna maigizo na sanaa kama hizi?Nadhani hafikishwi mahakamani na sidhani kama ni kiki za Uchaguzi kwa sababu tunaambiwa ''CCM hawana haja ya kufanya kiki ili wachaguliwe kwa sababu wanaiba kura''!
Huwezi kusema wanafanya kiki kwa sababu ya chaguzi halafu hapo hapo unasema huwa wanaiba kura!
Wazee wa kupingaaaInsanity! Sasa kama kajisalimisha si apelekwe rumande kusubiri kesi? Kosa halina expiry date, hadi ulilipe. Sasa na milioni 1 juu? Na hivyo vyombo vya habari vilijuaje ataenda kujisalimisha siku hiyo?
Maigizo mengine ya kitoto sana.