MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,974
Jambazi sugu aitwaye Ali Mtemi amejisalimisha katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya baada ya kukoswa koswa kuuwawa na Askari wa doria mara nne katika Wilaya ya Kigamboni huku baadhi ya wengine katika kikundi chake wakiuwawa na kukamatwa.
Polisi wamekuwa wakimsaka kwa muda mrefu ambapo amekuwa akijificha katika mikoa mbalimbali lakini hatimaye ameamua kujitokeza na kwenda kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni ili kuomba msamaha kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigamboni.
Ujasiri wake wa kujisalimisha umepongezwa na Kamati ya Ulinzi ya Ulinzi na Usalama, ambapo Mkuu wa Wilaya amemuahidi kumsaidia shilingi 1,000,0000 kama mtaji wa biashara baada ya kuahidi ameachana na ujambazi mbele ya wazazi wake na mjomba wake.
Mkuu wa Wilaya amemuomba akawe ni kioo kwa vijana wengine ambao bado wanafanya vitendo vya wizi na ujambazi katika Wilaya ya Kigamboni.
NB: Kumbe hata majambazi wanaogopa kifo!
Polisi wamekuwa wakimsaka kwa muda mrefu ambapo amekuwa akijificha katika mikoa mbalimbali lakini hatimaye ameamua kujitokeza na kwenda kwenye ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kigamboni ili kuomba msamaha kwenye Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Kigamboni.
Ujasiri wake wa kujisalimisha umepongezwa na Kamati ya Ulinzi ya Ulinzi na Usalama, ambapo Mkuu wa Wilaya amemuahidi kumsaidia shilingi 1,000,0000 kama mtaji wa biashara baada ya kuahidi ameachana na ujambazi mbele ya wazazi wake na mjomba wake.
Mkuu wa Wilaya amemuomba akawe ni kioo kwa vijana wengine ambao bado wanafanya vitendo vya wizi na ujambazi katika Wilaya ya Kigamboni.
NB: Kumbe hata majambazi wanaogopa kifo!
Video ya jambazi sugu akijisalimisha kwa Mkuu wa Wilaya.