kilimasera
JF-Expert Member
- Dec 2, 2009
- 3,068
- 268
MTUHUMIWA wa ujambazi sugu ambaye amekuwa akisakwa kwa muda mrefu na Polisi mkoani Rukwa, amekufa ghafla baada ya kuvuliwa hirizi kubwa aliyokuwa ameivaa mkononi.
Akizungumzia mkasa huo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Isuto Mantage alisema mtuhumiwa huyo, Jelaz Mwananjela (44), alikamatwa na wananchi saa 11 juzi jioni pamoja na mwanawe, Galus Mwananjela (18) na kufikishwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Namanyere, wilayani Nkasi kwa mahojiano.
Baada ya kufikishwa kituoni hapo, Kamanda Mantage alisema, mtuhumiwa huyo alianza kulalamika kuwa wananchi walimnyang'anya hirizi yake aliyokuwa ameifunga kwenye mkono wake wa kushoto.
Kwa mshangao wa wengi wetu, Mwananjela alianza kulalamika kuwa anaweza kufa wakati wowote kama hatarudishiwa hirizi yake na kweli muda mfupi baada ya kutoa kauli hiyo alipoteza fahamu, alisema Kamanda Mantage.
Kwa mujibu wa Kamanda Mantage, Galus ambaye ni mtoto wa marehemu na pia anashikiliwa Polisi, alikiri kuwa baba yake alivaa hirizi hiyo kama kinga yake na ilikuwa inamsaidia asiumie wala kufa kama akipigwa katika matukio ya ujambazi.
Kamanda Mantage, alisema watuhumiwa hao walikamatwa na bunduki moja aina ya Shotgun yenye namba 065678 na risasi mbili, na walikuwa katika maandalizi ya kufanya unyang'anyi katika kijiji cha Ntalamila wilayani Nkasi.
Alisema, watuhumiwa hao walikamatwa baada ya wananchi wema kutoa taarifa za siri kuwa kuna watu wana silaha kijijini hapo, ndipo polisi, viongozi wa kijiji na wananchi wakashirikiana kuwakamata.
Mwananjela alikutwa pia na kisu kikubwa ambacho wananchi walikitumia kukata hirizi hiyo na kuichoma moto.
Kwa mujibu wa Kamanda Mantage, Gulus atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.
Akizungumzia mkasa huo jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Isuto Mantage alisema mtuhumiwa huyo, Jelaz Mwananjela (44), alikamatwa na wananchi saa 11 juzi jioni pamoja na mwanawe, Galus Mwananjela (18) na kufikishwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Namanyere, wilayani Nkasi kwa mahojiano.
Baada ya kufikishwa kituoni hapo, Kamanda Mantage alisema, mtuhumiwa huyo alianza kulalamika kuwa wananchi walimnyang'anya hirizi yake aliyokuwa ameifunga kwenye mkono wake wa kushoto.
Kwa mshangao wa wengi wetu, Mwananjela alianza kulalamika kuwa anaweza kufa wakati wowote kama hatarudishiwa hirizi yake na kweli muda mfupi baada ya kutoa kauli hiyo alipoteza fahamu, alisema Kamanda Mantage.
Kwa mujibu wa Kamanda Mantage, Galus ambaye ni mtoto wa marehemu na pia anashikiliwa Polisi, alikiri kuwa baba yake alivaa hirizi hiyo kama kinga yake na ilikuwa inamsaidia asiumie wala kufa kama akipigwa katika matukio ya ujambazi.
Kamanda Mantage, alisema watuhumiwa hao walikamatwa na bunduki moja aina ya Shotgun yenye namba 065678 na risasi mbili, na walikuwa katika maandalizi ya kufanya unyang'anyi katika kijiji cha Ntalamila wilayani Nkasi.
Alisema, watuhumiwa hao walikamatwa baada ya wananchi wema kutoa taarifa za siri kuwa kuna watu wana silaha kijijini hapo, ndipo polisi, viongozi wa kijiji na wananchi wakashirikiana kuwakamata.
Mwananjela alikutwa pia na kisu kikubwa ambacho wananchi walikitumia kukata hirizi hiyo na kuichoma moto.
Kwa mujibu wa Kamanda Mantage, Gulus atafikishwa mahakamani mara baada ya uchunguzi wa awali kukamilika.