Jamani ukipenda Ua basi penda na boga lake

Kuwapenda ndugu wa mwenzio haina maana ufurahie wao kuhamia kwako(kuja kuja kila mara).Hiyo inabadilisha maana nzima ya ndoa aliyokua nayo anaeingia...familia ipo hata yake kaicha ili aje kuwa na mumewe na sio familia ya mumewe!Kama mama wa watu kajichokea badala ya kwenda kupumzika analazimika kukaa na wageni ambao unaweza kuta hata story nae hawana!Matumizi na maisha yanabadilika kwa muda maana kila anachofanya inabidi afikirie wageni!Wengine hua wanakuja na maneno basi tabu tupu...ukiwakuta wanaongea hao wananyamaza na kujifanya kukuchekea kinafiki!Kubadilisha mambo yanavyoenda nyumbani maana unaweza kuta mama kaacha maagizo ya lunch iwe wali maharage akirudi anaambiwa nyama jioni ilipikwa mchana kwasababu shangazi hapendi maharage...unadhani kama mambo ya aina hii yanaendelea dada wa watu ataacha kua alivyo?!Kuna watu hata ukiwachekea wanakwangalia tu!!
Muhimu huyo mume amuulize mwenzake nini tatizo...huwezi jua labda asipokuwepo ndugu wanambeza mke.

Alafu jamani nyie wanaume hata kama ndugu zenu wanawategemea mnashindwa nini kuwasaidia wakiwa mbali?!Epukeni matatizo yasiyo ya lazima kwakuwafikishia mahitaji yao walipo badala ya kuishi au kuwpo kwenu muda mwingi.Hao ndugu nao wajue kusalimia unakaa siku mbili unaondoka na sio kila mwezi unakuja!Simu zipo salimianeni kwenye simu maisha yaendelee!
 
Yaani ukoo mzima uhamie kwangu hiyo hapana awasaidie wakiwa huko huko kwao sio kuja kujazana nyumbani kwangu ukoo wote nitawanunia kwa sana tu (joke) bana ha ha haha

hatuzungumzii ukoo hapa,
lets say, unaishi na wifi zako 2,
na shemeji yako 1, hapo vipi?
 
Kuwapenda ndugu wa mwenzio haina maana ufurahie wao kuhamia kwako(kuja kuja kila mara).Hiyo inabadilisha maana nzima ya ndoa aliyokua nayo anaeingia...familia ipo hata yake kaicha ili aje kuwa na mumewe na sio familia ya mumewe!Kama mama wa watu kajichokea badala ya kwenda kupumzika analazimika kukaa na wageni ambao unaweza kuta hata story nae hawana!Matumizi na maisha yanabadilika kwa muda maana kila anachofanya inabidi afikirie wageni!Wengine hua wanakuja na maneno basi tabu tupu...ukiwakuta wanaongea hao wananyamaza na kujifanya kukuchekea kinafiki!Kubadilisha mambo yanavyoenda nyumbani maana unaweza kuta mama kaacha maagizo ya lunch iwe wali maharage akirudi anaambiwa nyama jioni ilipikwa mchana kwasababu shangazi hapendi maharage...unadhani kama mambo ya aina hii yanaendelea dada wa watu ataacha kua alivyo?!Kuna watu hata ukiwachekea wanakwangalia tu!!
Muhimu huyo mume amuulize mwenzake nini tatizo...huwezi jua labda asipokuwepo ndugu wanambeza mke.

Alafu jamani nyie wanaume hata kama ndugu zenu wanawategemea mnashindwa nini kuwasaidia wakiwa mbali?!Epukeni matatizo yasiyo ya lazima kwakuwafikishia mahitaji yao walipo badala ya kuishi au kuwpo kwenu muda mwingi.Hao ndugu nao wajue kusalimia unakaa siku mbili unaondoka na sio kila mwezi unakuja!Simu zipo salimianeni kwenye simu maisha yaendelee!



mbona wakati mwingine Lizzy,
waweza kuta mume anakaa na shemeji zake wengi tu,
lakini hakuna mikwaruzo wala migongano yeyote!
 
Lazima kutakuwa na tatizo si hiv hiv mtu anaweza kuchukia watu bana.
Pia mi nadhan kwa ndugu wa kuja na kuondoka, au kaja kusalimia toka kijijin kwa muda na ataondoka huyo hana shida sana, na hata kama anamatatizo ni rahis tu wala hakupi presha kabisaaa mana si unajua ni mpitaji?

TATIZO KUBWA
Ni baadhi ya wale ndugu wa mume ambao akifika hapo nyumban anataka kujifanya yeye ndo haswaaaa kila kitu anajua na kujifanya anapanga taratibu za ndani kwa khaaa!! Wa hiv ntamkomesha akija anga zangu
Eti unashida nyingine za kawaida kabisa unaweza mwambia shemej/wifi unasubiri mpaka ndugu yako mhhh!

Ila nyie wababa mjue wakat mwingine wake zenu si kwamba hawawapend ndugu zenu ila ndugu wanachangia sana, tena wanawake wengine kukwambia kila kitu anachofanya nduguyo anaona kama utaona kama hawepend ndugu zako au kuwagombanisha bora tu anyamaze, vikizid ndo hayo sasa.
 
mbona wakati mwingine Lizzy,
waweza kuta mume anakaa na shemeji zake wengi tu,
lakini hakuna mikwaruzo wala migongano yeyote!

Ndo maana inasemekana watu hatufanani!Kwasababu hao wanaweza haina maana wote wataweza...kuna watu kuishi nao haitofautiani na adhabu!!Vyovyote vile sisuport sana ndugu kuhamia/kuishi kwa ndugu aliyeoa/olewa wakati wanaweza kukaa kwao na wakapata kila kitu!!!
 
Kwahiyo SMU,
unataka kuniambia hizi sababu zinaweza kumfanya mama,
ajifungie chumbani na kuzanza kununa nuna eeee?

Yes...mara nyingi anakuwa kwenye dilema...hajui afanye nini hasa! Kukwambia moja kwa moja kuwa uwepo wa ndugu zako unamkwaza na angependa waondoke/uwaondoe anashindwa! Wengine anaweza kwenda mbali zaidi kwa kutengeza 'zengwe' la kukufanya uwachukie hao wageni.
 
mbona wakati mwingine Lizzy,
waweza kuta mume anakaa na shemeji zake wengi tu,
lakini hakuna mikwaruzo wala migongano yeyote!

Sababu ndugu wa mke mara nyingi hawajikwezi sijui nisemaje yaani hawa nguvu sana labda sababu dada ndo kaolewa.

Sasa hawa wa mume (baadhi) wanapenda sana sijui hata nitumie neno gani, sijui mashindano, sijui kaka yao ndo kichwa nyumba aahh hata sijui
 
or the vice versa is true!!!!!!

Kuna jamaa mmoja alisikika akilalamika mbele ya wenzake;

Nanukuu,

''Mke wangu toka tumefunga ndoa amebadilika na kuwa mtu wa kununa na kujifungia ndani kila wakati hasa pale ndugu zangu wanapokuja kunisalimia kwangu. Ukizingatia kuwa mimi ndo kaka mkubwa katika familia yetu na wazazi wetu wote (Baba na Mama) wameshafariki, kwahiyo nimebaki kuwa msaada mkubwa kwao."

Mwisho wa kunukuu.

SWALI: Hivi ni kwa nini kwenye ndoa nyingi akina mama huwa wanagombana au kushindwa kukubaliana na uwepo wa ndugu wa mume nyumbani tofauti na akina baba? Ikitokea tu ndugu wa mume wamekuja nyumbani, basi mama hubadilika tabia, yaani ule uwajibikaji wa kila siku unapotea ghafla na kutwa nzima ananuna nuna tu!tafadhali naomba nisisitize, sio akina mama wote
(nimesema kesi nyingi hapa utakuta ni akina Mama Vs ndugu wa mume na sio Baba Vs ndugu wa mke!!!!)!!!!!!!!!!!!!


Samahani dada zangu, siwapondi ila naelezea hisia zangu!!!!!


Hapa naomba tusichanganye mada, knachozungumziwa na mtoa mada ni ndg zake wanapokuja kumsalimia, na si kuhamia kwake ukoo mzima!! someni vizuri jamani hapo kwenye red
 
hatuzungumzii ukoo hapa,
lets say, unaishi na wifi zako 2,
na shemeji yako 1, hapo vipi?

Wachache hao kaka? Na hao vijana wanasoma au wanafanya kazi? Nae mkeo umempa uhuru wa kuleta wadogo zake watatu wanaomtegemea? Kwa hesabu ya haraka haraka, hilo 'bungalow' lenu lina vyumba vingapi? Na watoto mnao au bado mpo mpo? Mara nyingi mnajikuta hata nyie mna hofu ya kuanzisha familia kwa kigezo kuwa mnataka muwasogeze hao wadogo zenu, mkistuka saa kumi na mbili jioni. Yale yale ya kuwa na miaka 50, na watoto wana miaka 10 - 14!
 
Hao ndugu wanatafuta nini kwa kaka yao hawajaolewa hao wakaishi na waume zao nazungumzia mawifi

Nitarudi ngoja kwanza nikumbuke mawifi zangu na mashemeji.

Ha ha ha ha Bacha bana leo yamekukuta yapi tena mkeo kanunia Dada zako (Joke)
am missing so much!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
hatuzungumzii ukoo hapa,
lets say, unaishi na wifi zako 2,
na shemeji yako 1, hapo vipi?

Mkubwa wifi 2 + shem 1

Haya ongeza hivi na mkeo naye wadogo zake 2 + kaka yake mmoja

Hapo kutakuwa na maendeleo ndani ya nyumba kweli.

Namuunga mkono DA katika hili hapa kujazana nyumbani kwetu bana kama msaada watapata wakiwa huko waliko sio kuja kuhamia nyumbani kwetu na mke wangu
 
Alafu jamani nyie wanaume hata kama ndugu zenu wanawategemea mnashindwa nini kuwasaidia wakiwa mbali?!Epukeni matatizo yasiyo ya lazima kwakuwafikishia mahitaji yao walipo badala ya kuishi au kuwpo kwenu muda mwingi.Hao ndugu nao wajue kusalimia unakaa siku mbili unaondoka na sio kila mwezi unakuja!Simu zipo salimianeni kwenye simu maisha yaendelee!
wewe Lizzy!!!this dont sound good umejiandaa kwa bifu
 
mbona wakati mwingine Lizzy,
waweza kuta mume anakaa na shemeji zake wengi tu,
lakini hakuna mikwaruzo wala migongano yeyote!

Hapa naomba tusichanganye mada, knachozungumziwa na mtoa mada ni ndg zake wanapokuja kumsalimia, na si kuhamia kwake ukoo mzima!! someni vizuri jamani hapo kwenye red

Wewe uliyeelewa msome mtoa mada hapo juu halafu leta mchango wako
 
Mkubwa wifi 2 + shem 1

Haya ongeza hivi na mkeo naye wadogo zake 2 + kaka yake mmoja

Hapo kutakuwa na maendeleo ndani ya nyumba kweli.

Namuunga mkono DA katika hili hapa kujazana nyumbani kwetu bana kama msaada watapata wakiwa huko waliko sio kuja kuhamia nyumbani kwetu na mke wangu

Mlimazunzu angalia usije suswa na ukoo mzima!!!!!!!
 
Wachache hao kaka? Na hao vijana wanasoma au wanafanya kazi? Nae mkeo umempa uhuru wa kuleta wadogo zake watatu wanaomtegemea? Kwa hesabu ya haraka haraka, hilo 'bungalow' lenu lina vyumba vingapi? Na watoto mnao au bado mpo mpo? Mara nyingi mnajikuta hata nyie mna hofu ya kuanzisha familia kwa kigezo kuwa mnataka muwasogeze hao wadogo zenu, mkistuka saa kumi na mbili jioni. Yale yale ya kuwa na miaka 50, na watoto wana miaka 10 - 14!

oraiti Dina,sasa unamwambiaje huyo bwana
awafukuze hao ndugu au,
kwani yawezekana wapo pale kwa mahitaji mbalimbali,
shule, ugonjwa n.k.
 
Back
Top Bottom