Jamani tusikilizane kwa makini

Muuza simu used

JF-Expert Member
Aug 23, 2017
4,393
7,039
Kaeni kwa kutulia, tumeshakubaliana ni hivi mapenzi ni kama vile mmekutana club ama sehemu yeyote ile ya starehe hakuna yeyote anayemshauri mwenzake ni kwa namna gani atumie pesa zake

Sasa hivi mada za nimeachwa mara nimeachika zimekuwa ni nyingi kupita maelezo! Yaani unamshauri mtu aachane na mpenzi wake kesho unakuta wamerudiana mbona mnatutia ubaya tu ndugu zangu

Ni hivi, kama umempenda na hukulazimishwa na mtu yeyote hakuna kuachana tena kama mna matatizo yenu kunyweni maji yakutosha kesho ni siku nyingine tena

Kuanzia leo watu wanaotakiwa kuja kuomba ushauri ni wale waliofunga ndoa tuna wataotoa ushauri ni wale walio kwenye ndoa tu

Sisi wengine tukae pale pembeni tena kwa kutulia tumechoka kusema mpige chini hakufai wakati ukitoka hapa unatutangazia kwa mpenzi wako eti watu JamiiForums wanasema nikuache

Koma
 
umeandika kama vile ni max mello. yaani ww ndio admin wa jf sio.
watu hawapangiwi cha kupost. kama unaona kero usitoe ushauri kwenye mada zao
 
Back
Top Bottom