Jamani tunakwenda wapi?

Nyumisi

JF-Expert Member
Nov 10, 2010
13,405
19,067
Mimi ni mwanajamii mpya na hii ndo post yangu ya kwanza.
Mimi nasikitishwa na tatizo la kikatiba lililopo ambayo inampa rais madaraka kupita kiasi, kiasi kwamba nchi inakuwa kama kampuni binafsi ya mtu. Yaani atateua kila mtu amtakaye bila kuingiliwa na mtu yoyote. Mpaka watendaji wa tume ya uchaguzi anateua yeye kiasi kwamba wapinzani wanalalamikia uhuru wa tume kuweza kufanya haki katika chaguzi.
Matokeo yake ndo tunaona madudu ya ufisadi kila kona na tunaona watu wenye kashfa nzito nzito wanajitokeza hadharani kuomba uongozi bila aibu.
Kwa hiyo nashauri watanzania tubadilike kudai mambo ambayo yatatusaidia kama nchi na vizazi vijavyo kuliko hivi sasa ambapo utakuta kashfa nyingi za ubadhirifu wa mabilioni ya pesa za umma zinaibuliwa, kama EPA, richmond lakini watanzania tunakaa kimya tu utafikiri hakuna kitu kilichotokea. Let us be serious, tusiwe watumwa kwa kisingizio cha amani.
 
mimi ni mwanajamii mpya na hii ndo post yangu ya kwanza.
Mimi nasikitishwa na tatizo la kikatiba lililopo ambayo inampa rais madaraka kupita kiasi, kiasi kwamba nchi inakuwa kama kampuni binafsi ya mtu. Yaani atateua kila mtu amtakaye bila kuingiliwa na mtu yoyote. Mpaka watendaji wa tume ya uchaguzi anateua yeye kiasi kwamba wapinzani wanalalamikia uhuru wa tume kuweza kufanya haki katika chaguzi.
Matokeo yake ndo tunaona madudu ya ufisadi kila kona na tunaona watu wenye kashfa nzito nzito wanajitokeza hadharani kuomba uongozi bila aibu.
Kwa hiyo nashauri watanzania tubadilike kudai mambo ambayo yatatusaidia kama nchi na vizazi vijavyo kuliko hivi sasa ambapo utakuta kashfa nyingi za ubadhirifu wa mabilioni ya pesa za umma zinaibuliwa, kama epa, richmond lakini watanzania tunakaa kimya tu utafikiri hakuna kitu kilichotokea. Let us be serious, tusiwe watumwa kwa kisingizio cha amani.
at least new comer unakuja na mawzo mapya badala ya umbea mtupu, sasa unashuri tufanya nini mr newcomer?
 
Mimi ni mwanajamii mpya na hii ndo post yangu ya kwanza.
Mimi nasikitishwa na tatizo la kikatiba lililopo ambayo inampa rais madaraka kupita kiasi, kiasi kwamba nchi inakuwa kama kampuni binafsi ya mtu. Yaani atateua kila mtu amtakaye bila kuingiliwa na mtu yoyote. Mpaka watendaji wa tume ya uchaguzi anateua yeye kiasi kwamba wapinzani wanalalamikia uhuru wa tume kuweza kufanya haki katika chaguzi.
Matokeo yake ndo tunaona madudu ya ufisadi kila kona na tunaona watu wenye kashfa nzito nzito wanajitokeza hadharani kuomba uongozi bila aibu.
Kwa hiyo nashauri watanzania tubadilike kudai mambo ambayo yatatusaidia kama nchi na vizazi vijavyo kuliko hivi sasa ambapo utakuta kashfa nyingi za ubadhirifu wa mabilioni ya pesa za umma zinaibuliwa, kama EPA, richmond lakini watanzania tunakaa kimya tu utafikiri hakuna kitu kilichotokea. Let us be serious, tusiwe watumwa kwa kisingizio cha amani.

Kwenye hiyo RED ndio kimbilio la CCM na kutisha watu wa vijijini.
 
Nani wa kumfunga paka kengele?
I mean nnani wa kuanzisha hayo madai? yadaiwe kwa njia gani?
 
Nani wa kumfunga paka kengele?
I mean nnani wa kuanzisha hayo madai? yadaiwe kwa njia gani?

Cha msingi mimi naona ni elimu ya ulaia kwa watanzania wote, namshukuru mungu kwa sasa asubuhi inakaribia, lakini bado tuna kazi kubwa ya kuwafanya watanzania wote kujitambua ni akina nani, tumetoka wapi, tuko wapi, tunaelekea wapi, tulitakiwa kwenda wapi, kwa nini tuko kama tulivyo, tatizo ni nini, chanzo ni akina nani, na wana nia gani (sasa na baadae), nini hatima yetu na vizazi vyetu.

Tatizo kubwa wengi wetu bado ni wanafiki, hivyo tuache unafiki na twende mkoa kwa mkoa, wilaya kwa wilaya, tarafa kwa tarafa, kata kwa kata, kijiji kwa kijiji, kitongoji kwa kitongoji, mtaa kwa mtaa, nyumba kwa nyumba, chumba kwa chumba, kitanda kwa kitanda na mwisho kabisa one by one tuwaelimishe watanzania wote, kwani wakenya au taifa lingine lolote haliwezi kuja kutututea sisi wenyewe, bali tunatakiwa sisi kujitambua na kusimama kama watanzania kuikomboa nchi yetu mikononi mwa watu wabaya (CCM).

TWENDENI SOTE
 
Back
Top Bottom