Jamani tuacheni kiburi, mimi nimechagua kuacha

The golden

JF-Expert Member
Sep 11, 2018
1,381
2,553
Kadri siku zinavyokwenda nazidi kujifunza, moyo wangu unapondeka, unyenyekevu unatawala.
Kwanza kabisa, nimepoteza watu wengi sana wa maana katika maisha yangu, watu niliowapenda na kuwategemea, kwa kiasi fulani walinijengea kiburi.
Nimewaona watu wenye mamlaka na nguvu kubwa wakitoweka ghafla kama upepo, hili nalo limepunguza majivuno yangu. Kuna watu walikuwa na sauti ya kutisha, wangeweza kufanya chochote, kusema chochote, au kumfanya mtu mwingine chochote hawa nao hawapo, na wengine wako gerezani.

Siku zinaenda kasi sana, jana siyo sawa na leo. Leo unaweza kucheka kesho ukaamuka unalia.

Mimi nimechagua haki, upendo, na unyenyekevu. Dunia wala Tanzania si mali yetu, dunia tuliikuta na Tanzania tuliikuta, vyote tutaviacha.
 
πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜‹πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜πŸ˜
 
Kadri siku zinavyokwenda nazidi kujifunza, moyo wangu unapondeka na kuwa mnyenyekevu.
Kwanza kabisa, nimepoteza watu wengi, sana wa maana katika maisha yangu, watu niliowapenda na kuwategemea, kwa kiasi fulani walinijengea kiburi.
Nimewaona watu wenye mamlaka na nguvu kubwa wakitoweka ghafla kama upepo, hili nalo limepunguza majivuno yangu. Kuna watu walikuwa na sauti ya kutisha, wangeweza kufanya chochote, kusema chochote, au kumfanya mtu mwingine chochote hawa nao hawapo, na wengine wako gerezani.

Siku zinaenda kasi sana, jana siyo sawa na leo. Leo unaweza kucheka kesho ukaamuka unalia.

Mimi nimechagua haki, upendo, na unyenyekevu. Dunia wala Tanzania si mali yetu, dunia tuliikuta na Tanzania tuliikuta pia vyote tutaviacha.
Kama hivi

IMG-20211016-WA0004.jpg
 
Kadri siku zinavyokwenda nazidi kujifunza, moyo wangu unapondeka na kuwa mnyenyekevu.
Kwanza kabisa, nimepoteza watu wengi, sana wa maana katika maisha yangu, watu niliowapenda na kuwategemea, kwa kiasi fulani walinijengea kiburi.
Nimewaona watu wenye mamlaka na nguvu kubwa wakitoweka ghafla kama upepo, hili nalo limepunguza majivuno yangu. Kuna watu walikuwa na sauti ya kutisha, wangeweza kufanya chochote, kusema chochote, au kumfanya mtu mwingine chochote hawa nao hawapo, na wengine wako gerezani.

Siku zinaenda kasi sana, jana siyo sawa na leo. Leo unaweza kucheka kesho ukaamuka unalia.

Mimi nimechagua haki, upendo, na unyenyekevu. Dunia wala Tanzania si mali yetu, dunia tuliikuta na Tanzania tuliikuta pia vyote tutaviacha.
Hata malaika mbinguni wanashangilia Mtu mwovu akiamua kuokoka na kuacha njia yake mbaya
 
Kanyaga taratibu hii dunia tunapiata
Malipo ni hapa hapa dunian

Usipolipa wewe wanao watalipia madhambi yako
 
CCM wanaifanya NCHI kama mali yao, Siku zinakuja viongozi wote wanaotenda isivyo HAKI mtalia na kusaga meno. Acheni kubambika watu kesi zisizo za haki
 
Kadri siku zinavyokwenda nazidi kujifunza, moyo wangu unapondeka, unyenyekevu unatawala.
Kwanza kabisa, nimepoteza watu wengi sana wa maana katika maisha yangu, watu niliowapenda na kuwategemea, kwa kiasi fulani walinijengea kiburi.
Nimewaona watu wenye mamlaka na nguvu kubwa wakitoweka ghafla kama upepo, hili nalo limepunguza majivuno yangu. Kuna watu walikuwa na sauti ya kutisha, wangeweza kufanya chochote, kusema chochote, au kumfanya mtu mwingine chochote hawa nao hawapo, na wengine wako gerezani.

Siku zinaenda kasi sana, jana siyo sawa na leo. Leo unaweza kucheka kesho ukaamuka unalia.

Mimi nimechagua haki, upendo, na unyenyekevu. Dunia wala Tanzania si mali yetu, dunia tuliikuta na Tanzania tuliikuta, vyote tutaviacha.
Haa umenikumbusha kuondoka mjini ,unatumia tungo tata mwishowe unasindikizwa kijijini kwenu
 
Back
Top Bottom