KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
Wana wa JF mambo vp?.Kama kichwa cha habari kilivyojieleza ni mkasa ulomkuta shemeji yangu mdogo wake na mke wangu.Kama anavyoeleza;Ni miaka miwili sasa toka niwe katika uhusiano wa kimapenzi na huyu mwenzi wangu bila shida yoyote.Lakini cha kushangaza na kilichonishtua hivi karibuni kama mwezi mmoja uliopita tulivyoonana nilimkuta amechanjwa chale kuanzia kichwani hadi miguuni na hirizi aloivaa kiunoni.Nilipomuuliza mwenzangu kulikoni uko hivi ni nini kilichokusibu,maana toka tumeonana na wewe sijawahi kukupata ukiwa ktk hali hii.Akanijibu ni mambo ya kwenye ukoo wangu yanayohusiana na mambo ya majina niliyoitwa.Sasa kutokana na jibu hilo alilopewa anasema hajaamimi hivyo akanitaka ushauri nami likawa zito hivyo nimelileta mbele yenu tusaidiane.