Jamani nilipitiwa tu na majukumu.
Bado siamini kilichotokea. Huyu jamaa nilishawahi kufanya naye biashara kama mwaka umepita. Kama miezi mitatu imepita alikuja kaka yangu akaona ile mifugo niliyoagiza kwa huyu jamaa akatamani naye aifuge hivyo akaniomba nimwagizie halafu nimtumie maana yeye anaishi Lindi
Nikaongea na huyu mjasiriamali akanihakikishia mzigo anao ndipo tukakubaliana nimtumie pesa kama laki 3 hivi ili autume. Baada ya kutuma hela jamaa akaanza sababu mara amekosa basi na hatimaye anauguza hadi leo nikimpigia simu hapokei wala hajibu SMS zangu.
Namtahadharisha kuwa dhuluma siyo nzuri kwenye maisha na atambue kuwa yatakuja kumtokea pabaya maana ameweza kunifanyia hivi mimi ambaye sitaweza kumfanya kitu ila atakuja kumfanyia mtu ambaye anapenda revenge. Mimi naamini zaidi kwenye KARMA
Asanteni
Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
Laki tatu ni pesa ndefu we mama, unaweza kwenda Kimboka kuokoteza mwezi mzima na chenji ikarudijamaa kajidhalilisha laki tatu.... duh
Laki tatu ni pesa ndefu we mama, unaweza kwenda Kimboka kuokoteza mwezi mzima na chenji ikarudi
Miezi mitatu tu tayari umekuja kumtangaza hapa je ingekwa miezi sita si ungefika hadi aljazeera?
Kweli kufanya biashara na masikini yataka moyo!
Haya mtaji hapa huyo mtu wako
Asante FairPlayer!
Jina limeshatajwa mara mbili sema husomi uzi vizuri! Nadhani siyo vyema kufurahia mwenzako akipatwa na matatizo.
Tapeli wangu ni Kitomari2 wa Tengeru
Karibuni mchangie
Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums