Jamani nimeibiwa au ndio halisi? Mwenye kufahamu naomba kujuzwa tafadhali!!

Zyamwelele

JF-Expert Member
Aug 5, 2013
405
153
Habarini wakuu!

Nimeenda kununua gesi mtungi wa kg 15 bei nimeambiwa tsh 61,000, wakati nilijiandaa na tsh 54,000.

Sasa wakuu hiyo ndo bei halali iliyotolewa na mamlaka husika au nimeibiwa?

Kama ni bei elekezi imeanza kutumika toka tarehe gani na mwezi upi?

Ilitolewa taarifa kwa umma au imeanza kutumika kimyakimya?

Mwenyekujua tafadhali tufahamishane!
 
Labda unaishi Nyanchenche, kutoa gesi toka Dar hadi huko si mchezo.

Umeliwa lakini.
 
Habarini wakuu!

Nimeenda kununua gesi mtungi wa kg 15 bei nimeambiwa tsh 61,000, wakati nilijiandaa na tsh 54,000.

Sasa wakuu hiyo ndo bei halali iliyotolewa na mamlaka husika au nimeibiwa?

Kama ni bei elekezi imeanza kutumika toka tarehe gani na mwezi upi?

Ilitolewa taarifa kwa umma au imeanza kutumika kimyakimya?

Mwenyekujua tafadhali tufahamishane!
Gesi ya Kg 15 ni Tsh 54,000/- . Itakuwa hao jamaa wamekukaBang. Jenga tabia ya kuomba risiti pia,itakusaidia kutoibiwa mara kwa mara.
 
Gesi ya Kg 15 ni Tsh 54,000/- . Itakuwa hao jamaa wamekukaBang. Jenga tabia ya kuomba risiti pia,itakusaidia kutoibiwa mara kwa mara.

Asanteni kwa taarifa'' nimerudi na nimerudishiwa 7,000 yangu!
Wanajikanyaga kanyaga eti alikuwepo alikua hajui bei. Nikajua ni wezi tu.
 
nimenunua kimara jana kwa shilingi 63,000/= sasa mimi labda ndio nimeibiwa zaidi. kama kuna flat rate watuambie au kama wanauza kimaeneo watuambie.
 
Asanteni kwa taarifa'' nimerudi na nimerudishiwa 7,000 yangu!
Wanajikanyaga kanyaga eti alikuwepo alikua hajui bei. Nikajua ni wezi tu.
Labda alikua hajui bei kweli, angeweza hata kukuuzia kwa sh 24,000/=.. Ungefanyaje?
 
Gesi gani mnayoiongelea hapa. Kwani ya Mtwara imeshaanza kuuzwa!?
 
Umeliwa men!

Nimeanzisha kampuni ya yangu, tunauza kwa sh 53,500 inaitwa MANDLA GAS karibuni wadau.
 
nimenunua kimara jana kwa shilingi 63,000/= sasa mimi labda ndio nimeibiwa zaidi. kama kuna flat rate watuambie au kama wanauza kimaeneo watuambie.

NI kweli kimara wamepandisha...sasa sijui ni kwa sababu ya foleni ya magari?...mwe nchi hii
 
nimenunua kimara jana kwa shilingi 63,000/= sasa mimi labda ndio nimeibiwa zaidi. kama kuna flat rate watuambie au kama wanauza kimaeneo watuambie.

Pole hapo umelizwa kama ilivyotaka kutokea kwangu leo! Mm nimerudi na nimerudishiwa! Mi mwenyenyewe yamenitokea huko mbezi mkuu'. Nenda wakupe risiti.
 
Back
Top Bottom