Juzi nilikua nafatilia Bunge la bajeti, kilicho nishangaza mimi kama mswahili ni namna gani Wabunge na Mawiziri wanavyo halibu Lugha.Waziri ama Mbunge akihalibu kingeleza watu wanan'gaka,lakn la juzi kimya: Waziri-"Maziwa yaliopo hayatoshelezi mahitaji ya mashule". Mbuge- "madawa katika mahospitali".Wale ndio tunawategemea wasimamia lugha na kuipigania halafu wao kwa kujua ama kutokujua wanahalimbu nembo yetu ya taifa.Halafu kunafaida gani kuweka neno la kiingeleza wakati la kiswahili lipo au ndio usomi,lakini wanaokusikiliza wanakuelewa wote ama ndio utumwa wa lugha.Hebu tujitathimini kama ni kingereza tuongee kiingeleza na panapo takiwa lugha ya kiswahili tuiongee kwa ufasaha.