Jamani naomba msaada, nimeandaa bwawa nataka nifuge samaki nisaidieni mbegu nzuri ya kufuga

Chuo cha uvuvi au taasisi yoyote ya serikali simshauri. Aende kwa wazalishaji binafsi akachukue. Akipata mbegu ya dume tupu (YY) itafaa zaidi
HDMI ebu dadavua kigodo, namake wengine tunawaogopa watu binafsi kwa sababu wanadanganya sana.
 
HDMI ebu dadavua kigodo, namake wengine tunawaogopa watu binafsi kwa sababu wanadanganya sana.
Kuna wazalishaji binafsi ambao wako vizuri. Mimi natumia sana vifaranga kutoka Bigfish (Kigamboni) au ukiweza Ruvu Fish Farm (Mlandizi)

Tatizo la serikali ni kwenye huduma baada ya kukuuzia. Kama unavojua ni wasanii sana. Ukiwaita site wakushauri hata kwa malipo kidogo wana jeuri sana. Wao wakishakupa control number ukalipia vifaranga jua ndio mmemalizana
 
asante mkuu, nimekuelewa. inaonekana hawa watumishi wanamastress yao ya kazini na wanafanya as usual hawataki kujiongeza.
 
Chuo cha uvuvi au taasisi yoyote ya serikali simshauri. Aende kwa wazalishaji binafsi akachukue. Akipata mbegu ya dume tupu (YY) itafaa zaidi
Ahsante sana kwa ushauri wako nashukuru ndugu yangu
 
Nipo mbeya ndugu yangu, labda kama unafahamu sehemu yoyote huku naomba nielekeze
mimi niko Dar, kwa mikoani sina ideas yeyote labda ufunge safari au wasiliana na Bigfish au Ruvu fish farm kama HDMI alivyoshauri, ili uone kama wanaweza kukusafirishia huko ulipo.
 
mimi niko Dar, kwa mikoani sina ideas yeyote labda ufunge safari au wasiliana na Bigfish au Ruvu fish farm kama HDMI alivyoshauri, ili uone kama wanaweza kukusafirishia huko ulipo.
Ahsante sana kiongozi nashukuru kwa mrejesho!!
 
Nipo mbeya ndugu yangu, labda kama unafahamu sehemu yoyote huku naomba nielekeze
Kama uko mbeya mjini.. Nenda Iyunga kalobe, kuna jamaa anafuga sana samaki na ana hivo vifaranga vya kutosha
Atakushauri vizuri.kwenye Google map ukiangalia hiyo kalobe utaona location inaonekana
 
Kama uko mbeya mjini.. Nenda Iyunga kalobe, kuna jamaa anafuga sana samaki na ana hivo vifaranga vya kutosha
Atakushauri vizuri.kwenye Google map ukiangalia hiyo kalobe utaona location inaonekana
daaaah ahsante sana ndugu yangu nitaenda, mimi nipo hapa iyunga
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom