MGODOLO
JF-Expert Member
- Oct 23, 2020
- 209
- 172
Habari zenu ndugu zangu,
Kwanza niombe radhi kwenu, ni hali ya maisha kuwa ngumu jamani. Leo nimeona bora nije kwa ndugu zangu humu huenda nikapata msaada ili nipate ridhiki ya kukizi maisha.
Naitwa Rashidi, nipo jijini Arusha, jamani mwanaume mwenzenu nimekwama kiajira. Nimemaliza mji wote wa Arusha huu, ni mwezi wa saba sasa sina kazi ya kujishikiza zaidi ya zile unapiga leo, unapata buku mbili unaikimbiza kwa watoto. Halafu bora hiyo buku mbili uipate kila siku iwe afadhali, hapana.
Ndugu zangu, taaluma yangu ni udereva, nimetafuta hii nafasi nimekosa. Baadhi ya sehemu wanataka pesa, nami hata ya kula na watoto sina.
Kwa wewe ndugu yangu kama unayo nafasi ya udereva gari lolote, hususan ya mizigo nipo tayari kuja mkoa wowote, leseni yangu ni Class C, na ina vyeti vyake.
Jamani wanaume wenzangu, tusaidiane, mwanaume mwenzenu nimeshikika.
Waswahili wanasema mficha uchi hazai, mimi leo nimeuonesha nizae. Nisaidie ndugu zangu, ikipatikana tofauti na udereva pia nitafanya ili familia ipate kula.
Asanteni sana. nitamshukuru mwenye kunisaidia na mwenye kunipa mawazo mazuri ya kimaisha.
Namba yangu kwa alie na uhakika wa ajira +255755360768. Msaada wenu ndugu zangu.
Kwanza niombe radhi kwenu, ni hali ya maisha kuwa ngumu jamani. Leo nimeona bora nije kwa ndugu zangu humu huenda nikapata msaada ili nipate ridhiki ya kukizi maisha.
Naitwa Rashidi, nipo jijini Arusha, jamani mwanaume mwenzenu nimekwama kiajira. Nimemaliza mji wote wa Arusha huu, ni mwezi wa saba sasa sina kazi ya kujishikiza zaidi ya zile unapiga leo, unapata buku mbili unaikimbiza kwa watoto. Halafu bora hiyo buku mbili uipate kila siku iwe afadhali, hapana.
Ndugu zangu, taaluma yangu ni udereva, nimetafuta hii nafasi nimekosa. Baadhi ya sehemu wanataka pesa, nami hata ya kula na watoto sina.
Kwa wewe ndugu yangu kama unayo nafasi ya udereva gari lolote, hususan ya mizigo nipo tayari kuja mkoa wowote, leseni yangu ni Class C, na ina vyeti vyake.
Jamani wanaume wenzangu, tusaidiane, mwanaume mwenzenu nimeshikika.
Waswahili wanasema mficha uchi hazai, mimi leo nimeuonesha nizae. Nisaidie ndugu zangu, ikipatikana tofauti na udereva pia nitafanya ili familia ipate kula.
Asanteni sana. nitamshukuru mwenye kunisaidia na mwenye kunipa mawazo mazuri ya kimaisha.
Namba yangu kwa alie na uhakika wa ajira +255755360768. Msaada wenu ndugu zangu.