Jamani mbona wahamihaji haramu ni wengi Sana Tz??

Mayolela

JF-Expert Member
Sep 21, 2009
384
6
Jamani,naomba wana JF tulijadili hili kwani kwangu imekuwa kero sana,yaani hata kazi za kuoika chai,karani,kufagia wapewe wahamihaji harum ,ambao wengi sana wanatokea Kenya.Naomba Idara ya Uhamihaji ifanye kazi ipasavyo,ndio hao sasa wanaongaika sana hili wapate hati ya kupigia kura kama raia ,jamani kweli tutafika- hata wazungu wengine wankuja kufanya kazi za ukarani tu hapa bongo,na permit zinatolewa kwa zaidi ya miaka miwili,nadhani sheria sio zaidi ya miaka miwili,utakuta mhamihaji kakaa hapa mpaka kanunua shamba sehemu.
Tunaomba Idara husika itupie macho hili.Haswa kwenye hizi kampuni za kigeni hapa d,salaam.

naomba tuoa hoja.(ili cctv isijeninasa,maana ndio haohao)>
 
Wizara ya mambo ya ndani na wizara ya kazi zimelala usingizi wa pono.
 
Tusilaumu wizara ya mambo ya ndani peke yake. Ukimsikia rais wa Tanzania anasema hadharani kuwa Watanzania ni wezi na ndiyo sababu "wawekezaji" hawawaajiri, hii inawafunguliwa milango 'wawekezaji" kuleta kila Tom, Dick, and Harry na kuwapa kazi Tanzania kwa sababu wanajua hawataguswa. Chagueni serikali/viongozi makini.
 
Nakumbuka kesi moja miaka michache ya nyuma nadhani kampuni ya Kioo ambayo ni Wahindi. Jamaa waliwaleta wahindi wenzao na kuwaingiza nchini kiharamu na wakapata ajira pale za nafasi za juu pamoja na kuwa walikuwa hawajui kiingereza wala kiswahili na wakawa wanawanyanyasa sana wazawa. Baadhi ya Wafanyakazi wazawa wakaenda kuwachomea Uhamiaji jamaa walienda pale na kupata bulungutu lao na wale wahindi wakaendelea kupeta pamoja na kuwa walikuwa nchini kiharamu.

Wakongo, Wanyarwanda, Warundi, Waethiopia, Wasomali, Wahindi wa India, Bangladesh, Pakistan, Wachina na hata wazungu wanaoishi nchini kiharamu wanazidi kuongezeka kila siku na Wizara ya mambo ya ndani haiwachukulii hatua zozote kuhusu uvunjaji wao wa sheria za nchi.
 
Wewe Omega hapo juu kweli umenena nyie wenyewe mnaotoa comment hapa msikute mpo illegal kwenye nchi za watu. Hao illegal immigrant in Tanzania nao wanatafuta maisha kama nyie mnavyotafuta maisha huko majuu.Hebu acheni kuwasema kama vp rudini home muwafukuze.
 
NCHI CORRUPT.... Aaah wacha niende zangu Leaders J'mosi kuzindua mradi wakupambana na Malaria... ZINDUKA...
 
Watanzania wengi hawapendi purukushani katika nchi za watu. 99.9% ya Watanzania ninaowafahamu makaratasi yao yako bomba na wanaingia na kutoka bila wasiwasi wowote ule na wale ambao hawajapata makaratasi wanafuata njia halali ili kuhakikisha wanayapata makaratasi hao.
 
Watanzania wengi hawapendi purukushani katika nchi za watu. 99.9% ya Watanzania ninaowafahamu makaratasi yao yako bomba na wanaingia na kutoka bila wasiwasi wowote ule na wale ambao hawajapata makaratasi wanafuata njia halali ili kuhakikisha wanayapata makaratasi hao.

Hmmmm....sijui wewe uko wapi mwenzangu....lakini huku tuliko sisi wengine ni viroja mtindo mmoja kuanzia watu kutokuwa na namba, kutumia majina na utaifa tofauti (eg. South African), etc.
 
Kujadili waTz waliopo nje wanaoishi bila kufuata sheria thats has nothing to do with topic in hand.
 
In actual sense matatizo mengi yaliyopo Tz yanasababishwa na state of anarchy. Kukosekana kwa dola imara yenye nia ya dhati ya kuindeleza nchi ndio msingi wa matatizo yote haya na yajayo.
 
Watanzania wengi hawapendi purukushani katika nchi za watu. 99.9% ya Watanzania ninaowafahamu makaratasi yao yako bomba na wanaingia na kutoka bila wasiwasi wowote ule na wale ambao hawajapata makaratasi wanafuata njia halali ili kuhakikisha wanayapata makaratasi hao.

Hakuna lolote wala hawapati ukazi kihalali kuna watu wanajilipua kwa kujifanya wakimbizi ili wapate makaratasi. Wengine wanafunga ndoa za biashara na ni risk kweli kweli hadi wengine walikufa huko Detroit kwa kufunga ndoa za makaratasi na watu tofauti halafu wakapigwa risasi wote mtu na mchumba wake. Watu wanataabika majuu kuchonga namba au kutumia namba ya mtu. Waliopo marekani sasa hivi wanaomba tu obama awasaidie ili wapate hayo makaratasi.Kama huna makaratasi unasafa kweli kweli. Wapo wanaopata makaratasi kihalali bali ni wachache. Ila majority waliopo huko ni wale wanaoverstay baada ya hapo ni wanahaha kweli kweli kutafuta hayo makaratasi.
 
Kujadili waTz waliopo nje wanaoishi bila kufuata sheria thats has nothing to do with topic in hand.

Unaonekana kuogopa mada ya waTZ wanaoishi nje illegally, Kwani shida iko wapi? Kama unataka kutendewa justice na wewe lazima utende justice.
 
No, lakini watu wa Tea Party wakitaka hawa wahamiaji haramu watimuliwe nyinyi ma liberals mnaanza kulia lia ubaguzi
Achana na Tea Party. At least Marekani wana sheria zinazofanya kazi. Ukikamatwa unabangaiza illegally unapandishwa kizimbani then kwenye pipa, hadi kwenu. Lakini Tz, umesoma kile kisa cha Mwarabu wa Movenpick? Yupo illegally na wafanyikazi wazalendo wamelalamika lakini jamaa kapitisha mshiko polisi wanabaki wanawapigia simu wazalendo wafute malalamiko yao. That is Bongo and that is wrong.
 
Unaonekana kuogopa mada ya waTZ wanaoishi nje illegally, Kwani shida iko wapi? Kama unataka kutendewa justice na wewe lazima utende justice.
Kama unataka kuanzisha mada ya Watanzania wanaoishi nje illegally, fanya hivyo. Hapa tunazungumzia wahamiaji haramu wanavyozidi kuongezeka Bongo. The two may be related lakini kuiingiza hapa ni kupotosha lengo.
 
Hakuna lolote wala hawapati ukazi kihalali kuna watu wanajilipua kwa kujifanya wakimbizi ili wapate makaratasi. Wengine wanafunga ndoa za biashara na ni risk kweli kweli hadi wengine walikufa huko Detroit kwa kufunga ndoa za makaratasi na watu tofauti halafu wakapigwa risasi wote mtu na mchumba wake. Watu wanataabika majuu kuchonga namba au kutumia namba ya mtu. Waliopo marekani sasa hivi wanaomba tu obama awasaidie ili wapate hayo makaratasi.Kama huna makaratasi unasafa kweli kweli. Wapo wanaopata makaratasi kihalali bali ni wachache. Ila majority waliopo huko ni wale wanaoverstay baada ya hapo ni wanahaha kweli kweli kutafuta hayo makaratasi.

Wewe kama unataka kubisha bisha, mimi nakwambia ninayoyajua siyo kila Mtanzania aliye majuu anataabika kupata makaratasi. Na wengi ninaowafahamu mimi wala hawakujilipua kama unavyodhania. Kama mtu madarasa yake yamepanda na una ajira ya maana basi inakuwa rahisi ukilinganisha na yule ambaye asiye na madarasa mengi.

Ninaowafahamu mimi wengi wamefuata njia halali za kuomba makaratasi kama Watanzania bila kujilipua au kutangaza Utaifa wasiokuwa nao. Miaka hiyo ya nyuma ajira zilikuwa belele na hao Wabongo wengi fani walizosomea zilikuwa zinatakiwa sana na waajiri wengi.
 
Back
Top Bottom