Jamani Maisha Plus ++

kimatire

JF-Expert Member
Nov 27, 2008
371
93
Maisha Plus yanamfundisha nini kijana Mtanzania?Ndiyo ni biashara tuu lakini kuna ujumbe wowote vizazi vijavyo kufaidika??Achana na mshiko wa 15M/=
 
Aah, mie siku hizi wala siiangalii najinywea chui wangu taratiiibu muda huo!
 
Mie hata sijui inafundisha nini ..hivi kumbe imeanza haya mwenye ratiba anisaidie
 
Kwa kweli sioni km kuna cha kufundisha pale maana nimeona dalili zote za kutangaza biashara kwa akina DADA. kweli huwezi angalia ukiwa na family
 
nilitazama juzi wakati mmoja wao alifunikwa na mchanga halafu waketengeneza sehemu bandia za mwanamke kwa mchanga na rasta akapanda juu na kufanya vitu vyake ninaomba wazingatie maadili ya mtanzania.
 
nilitazama juzi wakati mmoja wao alifunikwa na mchanga halafu waketengeneza sehemu bandia za mwanamke kwa mchanga na rasta akapanda juu na kufanya vitu vyake ninaomba wazingatie maadili ya mtanzania.


Kifuatacho itakuwa ni mimba bandia ya huyo rasta!!
 
Maisha Plus yanamfundisha nini kijana Mtanzania?Ndiyo ni biashara tuu lakini kuna ujumbe wowote vizazi vijavyo kufaidika??Achana na mshiko wa 15M/=


Huu ni uchafu tu na uozo wa maadili ya Kitanzania maana kama mwenye akili timamu huwezi kuangalia pamoja na familia yako na hata ukiwa peke yako.
 
Hata mimi iliniudhi sana ile clip.... Hasa pale mmoja wao aliposema tengeneza na sambusa... (akiwa na maana ya uke)
 
Maisha plus ni burudani......
Tatizo watanzania wengi wana siasa za ujamaa na kujitegemea
kwa hiyo inabidi kila kitu kitangazwe kisiasa kuwa kina mafundisho..

Hata mashindano ya miss tanzania ni burudani tu
na hayana lingine la zaidi..
But watanzania inabidi wapigwe porojo
ili waelewe...

Sio kila burudani inahitaji mafunzo....

Maisha plus ni kama picnic fulani hivi kwa vijana
waliosalia mtazame kwenye tv.
 
hiyo ni reality show kama show nyingine i.e BBA n.k so yeyote aliyeko kwenye hicho kijiji ukiona anafanya mambo ya kupotosha jamii ni bor kum-evict pia wakati kipindi kinarushwa watu huwa wanatoa maoni yao so ni bora yeyote anayekuboa mtolee maoni na kueleza kiunagauba kile anachokuboa maana ukisema utafute mafunzo hutayapata kwani kama maisha ya kijijini wengi wetu tunayajua yalivyo isipokuwa watoto wa kileo ambao wamezaliwa kwenye familia za kitajiri wameogeshwa na kufuliwa chupi mpaka wamebalehe, yaani hawajui hata kuingia jikoni kupika wao hukaribishwa chakula mezani hawajui hata kutoa vyombo wakimaliza kula, hao ndio inapaswa wajifunze maisha ya kijijini yakoje sanasana tunachojifunza hapa ni kujua tabia za baadhi ya vijana wetu zilivyo na ulimbukeni walionao baadhi ya washiriki kwa muonekano na vitendo vyao mfano ni wanaume wanaosuka, kuvaa hereni, wanaojichubua kwa kutafuta weupe so ukiwaangalia unapata picha ya tabia zao.

Wengine zaidi ya umbea tu na majungu unaona hawana ufahamu wa kuelewa mambo yanavyokwenda katika dunia ya sasa hawana ya maana wanayoongea. bora siku imepita.
Ingawa napenda sana kuiangalia ila bado hawajaniburudisha kama maisha plus ya 1.
 
hiyo ni reality show kama show nyingine i.e BBA n.k so yeyote aliyeko kwenye hicho kijiji ukiona anafanya mambo ya kupotosha jamii ni bor kum-evict pia wakati kipindi kinarushwa watu huwa wanatoa maoni yao so ni bora yeyote anayekuboa mtolee maoni na kueleza kiunagauba kile anachokuboa maana ukisema utafute mafunzo hutayapata au pia unaweza kuyapata kwa kujua tabia za baadhi ya vijana wetu zilivyo na ulimbukeni walionao baadhi ya washiriki.

Maana wengine ni umbea tu hawana ya maana wanayoongea. bora siku imepita.
Ingawa napenda sana kuiangalia ila bado hawajaniburudisha kama maisha plus ya 1.
..Niliangalia ile ya jana sikuamini nilichokuwa nasikia. Nilikuta mabinti kama wanne wamekaa wanamjadili Liumba eti jamaa kazi yake ilikuwa ni kubadili mademu tu. Mara Ray C kafanya vile sijui nani kafanya nini? NI utumbo mtupu. Nadhani Masoud na wenzake wanatakiwa kuwakanya hawa na mazungumzo yao ukizingatia kuwa TBC 1 inatazamwa na watu wengi so kumjadili mtu kwa mambo usiyokuwa na ushahidi nayo yanaweza kuwaletea balaa!!! Kuna demu yuko kama mwarabu simpendi kabisa kwenye hiyo Maisha plus! yeye ni kuzungumzia watu tu.
 
Maisha plus ni burudani......
Tatizo watanzania wengi wana siasa za ujamaa na kujitegemea
kwa hiyo inabidi kila kitu kitangazwe kisiasa kuwa kina mafundisho..

Hata mashindano ya miss tanzania ni burudani tu
na hayana lingine la zaidi..
But watanzania inabidi wapigwe porojo
ili waelewe...

Sio kila burudani inahitaji mafunzo....

Maisha plus ni kama picnic fulani hivi kwa vijana
waliosalia mtazame kwenye tv.

Haingii akilini kabisa kuita hii ni burudani,Gharama, kwa maana ya muda wanaopoteza na output wanayotoa havina ulinganisho kabisa.Pia sisi watazamaji wa tv TBC1 Kiukweli hakuna kinachotuburudisha pale ukiacha kujifunza!!Kama jana mabinti watatu walikuwa wanaongea umbea fulani hivi unawahusu watu nje ya hicho Kijiji,Kimaadili haileti maana hata kidogo ,Kisheria ndo kwanza usiombe kwani mhusika akisimama vizuri watalambwa fidia isiyo kifani.Hebu jamani fikirini mambo yanayotupeleka mbele na siyo kuiga tu kila kunapokucha hata yasiyofaaaa?
 
Muongozaji wa kipindi hicho ni mbumbumbu mzungu wa reli, wanavyowahoji wale vijana hata haieleweki wanataka nini, wanauliza maswali ya kijingajinga , kwakweli sina muda nao ni heri nikanywe Konyagi nimshushe mzaramo mikono kuliko kuangalia huo utoto.
 
Sikuamini maskio yangu yule dada wa Kiarabu aliposema Liyumba amezoea kuto*** wanawake na kuwapa Magari mekundu... Yaani jana Mungu alisaidia watoto hawakuwepo Sebuleni ingekuwa balaa... Masoud do something...
 
Sikuamini maskio yangu yule dada wa Kiarabu aliposema Liyumba amezoea kuto*** wanawake na kuwapa Magari mekundu... Yaani jana Mungu alisaidia watoto hawakuwepo Sebuleni ingekuwa balaa... Masoud do something...
`Masoud mwenyewe kama hatakimbilia shule haraka miaka michache ijayo hataweza kukabiliana na changamoto za uandishi wa habari waujanja ujanja....poleni mliokua na familia zenu wakati upuuzi huo ukitokea.
 
maisha plus labda wanafundishwa wale watoto wakifulia wasihofu hata kijihini wanaweza kukaa wakanunua mashamba na kuanza maisha
 
Nimeona jana Dr. akiwahoji washiriki wote kama wana matatizo yoyote ya afya, cha ajabu kina dada wote wanariporti kuwashwa sehemu za siri.

Mmmmm sijui ugonjwa gani huu kwa wasichana wote!!!!!!!!!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom