nilitazama juzi wakati mmoja wao alifunikwa na mchanga halafu waketengeneza sehemu bandia za mwanamke kwa mchanga na rasta akapanda juu na kufanya vitu vyake ninaomba wazingatie maadili ya mtanzania.
Mie hata sijui inafundisha nini ..hivi kumbe imeanza haya mwenye ratiba anisaidie
Maisha Plus yanamfundisha nini kijana Mtanzania?Ndiyo ni biashara tuu lakini kuna ujumbe wowote vizazi vijavyo kufaidika??Achana na mshiko wa 15M/=
..Niliangalia ile ya jana sikuamini nilichokuwa nasikia. Nilikuta mabinti kama wanne wamekaa wanamjadili Liumba eti jamaa kazi yake ilikuwa ni kubadili mademu tu. Mara Ray C kafanya vile sijui nani kafanya nini? NI utumbo mtupu. Nadhani Masoud na wenzake wanatakiwa kuwakanya hawa na mazungumzo yao ukizingatia kuwa TBC 1 inatazamwa na watu wengi so kumjadili mtu kwa mambo usiyokuwa na ushahidi nayo yanaweza kuwaletea balaa!!! Kuna demu yuko kama mwarabu simpendi kabisa kwenye hiyo Maisha plus! yeye ni kuzungumzia watu tu.hiyo ni reality show kama show nyingine i.e BBA n.k so yeyote aliyeko kwenye hicho kijiji ukiona anafanya mambo ya kupotosha jamii ni bor kum-evict pia wakati kipindi kinarushwa watu huwa wanatoa maoni yao so ni bora yeyote anayekuboa mtolee maoni na kueleza kiunagauba kile anachokuboa maana ukisema utafute mafunzo hutayapata au pia unaweza kuyapata kwa kujua tabia za baadhi ya vijana wetu zilivyo na ulimbukeni walionao baadhi ya washiriki.
Maana wengine ni umbea tu hawana ya maana wanayoongea. bora siku imepita.
Ingawa napenda sana kuiangalia ila bado hawajaniburudisha kama maisha plus ya 1.
Maisha plus ni burudani......
Tatizo watanzania wengi wana siasa za ujamaa na kujitegemea
kwa hiyo inabidi kila kitu kitangazwe kisiasa kuwa kina mafundisho..
Hata mashindano ya miss tanzania ni burudani tu
na hayana lingine la zaidi..
But watanzania inabidi wapigwe porojo
ili waelewe...
Sio kila burudani inahitaji mafunzo....
Maisha plus ni kama picnic fulani hivi kwa vijana
waliosalia mtazame kwenye tv.
`Masoud mwenyewe kama hatakimbilia shule haraka miaka michache ijayo hataweza kukabiliana na changamoto za uandishi wa habari waujanja ujanja....poleni mliokua na familia zenu wakati upuuzi huo ukitokea.Sikuamini maskio yangu yule dada wa Kiarabu aliposema Liyumba amezoea kuto*** wanawake na kuwapa Magari mekundu... Yaani jana Mungu alisaidia watoto hawakuwepo Sebuleni ingekuwa balaa... Masoud do something...