Kyachakiche
JF-Expert Member
- Feb 16, 2009
- 983
- 207
Heshima kwako Kyachekiche.
Mkuu afadhali wewe umemwelewa Mzee wa Kiraracha.wengine wanajaribu kumwona mjinga wakati hata Mtu huru katangaza kugombea ubunge Hai.Mtu wa kumshangaa ni Lipumba asietaka kusoma alama za nyakati.Ukweli ni kwamba CCM iatshinda tena ingawa sipendi hii hali lakini mpaka sasa sijaona juhudi za dhati za vyama vyote vya upinzani kutaka kuongoza dola.
Najua wako baadhi ya wachangiaji wasioamini Mzee wa Kiraracha atakuwa mbunge wa Vunjo lakini mtashanga sana jinsi atakavyopita kwa kishindo huko Vunjo kama hamuamini mulizeni Mheshimiwa Kimaro alivyogaragazwa kwenye uchaguzi wa wenyeviti wa vitongoji hadi akafikia hatua ya kuwarubuni wenyeviti walioshinda.
Kwa macho na masikio ya kawaida unaweza usimuelewe, lakini impact yake utaisikia kampeni zikianza.