Jamani kuna nini kwani kinaendelea Tanzania kwa sasa?

Nchi iko salama tu hakuna shida ila Tanzania tunapenda maneno sana ya umbeya na udaku.

Nchi haina shida kabisa ila Dr Magufuli ana vita na wengi ktk system kimaslahi baada ya kubana njia zote za ufisadi.

Kwahiyo kuna mbinu nyingi zinatumika kudhoofisha utawala wake toka kwa mafisadi.


Mkuu:
Bashite nae fisadi?
 
Watanzania ach tulie tu kwa ujinga wetu. Miaka yote tunalia maji umeme mashamba wanauziwa akina fulani madini yanaibwa tembo na faru wameisha twiga wanaibwa mchana. Yoote haya na mengine tunayalilia kila siku lkn ukifika ule wakati mkipewa pilau baai akili yote inahamia kwenye beseni. Tunasahau yote tunasema tunapenda kusoma namba. Acha tu tuchanganyikiwe kwakweli
Number nazani zinasomeka vizuri sana
 
Nchi iko salama tu hakuna shida ila Tanzania tunapenda maneno sana ya umbeya na udaku.

Nchi haina shida kabisa ila Dr Magufuli ana vita na wengi ktk system kimaslahi baada ya kubana njia zote za ufisadi.

Kwahiyo kuna mbinu nyingi zinatumika kudhoofisha utawala wake toka kwa mafisadi.
Duh hivi unajielewa kweli wew?
 
Bashite bashite bashite kasababisha yote haya. Mange pia anasababish Bashite asitumbuliwe, angeacha kumpelekesha Magu pengn angeshamtumbua zaman lkn saivi wanaonyeshana ubabe tu halafu nyasi ndo zinaumia
 
Duh hivi unajielewa kweli wew?
Nchi iko salama kabisa hakuna shida,na wanaiona nchi ina shida ni wenye uchu wa Mali za nchi hii ambao kwa sasa hawana nafasi ya kuzipata kama ilivyokuwa awali.

Usituletee ngonjera hapa kuwa kuna shida ndani ya Tanzania wakati wewe ni mmoja wa unaopinga kazi nzuri za Rais wa nchi anazozifanya.

Nchi iko salama na wanainchi wako salama wala sijaona hicho unachoshangaa.
 
Nchi iko salama kabisa hii ya Tanzania, ila kama propaganda zinaenezwa kuwa Tanzania sio salama ukimuuliza kwanini sio salama hajui.

Nijuavyo Mimi Tanzania Tuko salama kabisa wala hakuna shida.

Huo uhalifu unaotokea ni kama uhalifu mwingine wowote ule na utashughulikiwa kama uhalifu mwingine unavyoshughulikia.

Hatuna jambo jipya ila kuna watu wanataka tuamini nchi haiko salama kitu ambacho si kweli.

Kama kutekwa watu haijaanza Leo,watu kupotea hakujaanza leo,kuuwawa watu na majambazi hakujaanza Leo,kuibiwa watu hakujaanza leo.

Ni matukio ambayo yapo na ni kiwango cha chini sana ambacho hakiwezi kuathiri amani ya nchi kiasi cha kusema nchi haiko salama.
Hakuna nchi iliyo salama wewe! Achana na kudumaza akili yako huku ukifumba macho eti nchi iko salama!
 
Mkuu:
Usiwe mvivu wa kufikiri, jaribu kutumia fikra zako kidogo sana ktk duru za siasa zinazo endelea kwa sasa hapa nchini na hatimae utamjua huyo Bashite.
Hatumjui Bashite
 
Mkuu:
Ha Ha Haaaaaaaaaaaaaa!
Hatumjui Bashiteeeeeeeee
Hata Bungeni nimemsikia Mh Mdee na Mh Sugu wanalitaja hili jina ndiyo najiuliza ni nani huyu.

Maana inaonekana ni MTU maarufu sana huyu.Lakini ni nani hasa na Anafanya nini?
 
Ukiamka unasikia sijui Gwajima hujakaa sawa sijui Makonda na vyeti feki hujajipumzisha mara unasikia tena sijui Halima Mdee na Spika Ndugai ukiangaza angaza tena unasikia sijui mchanga wa dhahabu na mtu bado hujapumzika na unayatafakari hayo mara ghafla tena unasikia sijui akina roma wamefanywa nini.

In short Mimi Mtanzania mwenzenu nimechanganyikiwa na haya ya nadhani nahitaji counseling ya kutosha kwani naanza kwa mbali kuichukia Tanzania na huko tuendako kama hali hii haitaisha au kumalizwa nadhani itabidi tu nimkabidhi rasmi roho yangu Israeli aondoke nayo tu Mbinguni kwa Baba Mungu.

Ndugu zanguni na wana JF wenzangu Tanzania yetu imekumbwa na nini sasa? Mwenye hii hofu na wasiwasi ni Mimi peke yangu tu au?

Ewe Mwenyezi Mungu tusaidie!
Nani kakwambia kuwa anayehusika kutoa roho za watu anaitwa Israel?
 
Kwani unatokea nchi gani?OK karbu ila kinachoendelea tunaogopa kusema ukweli ata watakaojibu watakuambia uongo au ya juu juu
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom