Jamani Kamshahara kangu!!!!!!

Umesahau moja, mchango kwa ajili ya kuiendeleza jf. Kazi ipo mkuu Mchango wa mwenye nyumba piga chini, kuhusu sisiemu no koment, harusi hizi siku kawaida harusi si lazima manake mambo ni mengi, send off ni kama nilivyoeleza kwa harusi!
 
hakuna mtumishi wa serikali anaeishi kwa mshahara wake tu, hivyo kama wewe ni mtumishi kweli wa serikali basi ni mzoefu mnajua mnapataje pesa zetu za kodi kiulani na maisha ya nasongambele, nyumba mnajenga magari mnanunua na kubadili
 
Pata uzoefu wa kazi kwa miaka kadhaa, then tafuta kazi inayokufaa. TGS D kwa serikalini ni mshahara wa kuanzia kwa mwajiriwa. Fani ziko nying kaka, kuna makampuni mengi yanahitaji damu changa kama yako katika utendaji kazi (sector ya banking, makampuni ya simu, mashirika mbalimbali).........achana na serikalini, after all huwezi kujifunza kazi ukiwa serikalini, watu wamekalia majungu na hawataki kuachia viti. Serikalini utaingia baada ya kupata uzoefu katika sector binafsi au mashirika mengine.....

Hayo ni maoni yangu kwako
 
duuh pole mkuu na hii michango ya harusi kama hujaoa bado kuipiga chini ni very risky...
Yaani hapa ndio pagumu ndugu yangu siwezi kuipiga chini kama ulivyosema ni very risk!
 
Jamani naombeni japo mnipe ka elimu kidogo kuhusiana na bajeti ili niweze kusavaivu katika sikukuu hizi zijazo za mwezi wa Desemba. Kamshahara kenyewe ni TGS.D na kabla ya tarehe 20 Desemba kuna mambo yafuatayo natakiwa nikamilishe.
1. Kuna kadi sita za harusi.............kiwango kwa kuwa nipo single kila moja elfu 20.
2. Kuna kadi ya mchango wa birthday ya mtoto wa mwenye nyumba mwisho tarehe 10 Desemba.
3. Kuna fomu ya mchango wa ujenzi wa ofisi ya CCM............hii nimepewa na bosi wangu, inabidi nichangie ili kuongeza imani mbele ya bosi, nisije nikakosa safari za kiofisi.
4. Kadi mbili za send-off.
Hapo ili kukamilisha hayo mambo yote hapo kamshahara kote kameisha.............wenye uzoefu huwa mnasavaivu vipi katika hali kama hii??

1) tema harusi zote
2)mwombe mwenye nyumba akukope elfu tano au kumi mwambie umepata matatizo utamrudishia tu, automatically wazo la mchango toka kwako litakufa!
3)kesho asubuhi kumbuka kubeba kadi yako ya CHADEMA, wakati unaenda kunywa chai hakikisha unaiacha mezani, unakua ka umeisahau flani hivi, hakikisha unatumia kila njia hadi bosi wako aione na ajue kuwa ni yako--automatically atakuwa keshakufuta katika hesabu za wataotoa mchango
 
Pata uzoefu wa kazi kwa miaka kadhaa, then tafuta kazi inayokufaa. TGS D kwa serikalini ni mshahara wa kuanzia kwa mwajiriwa. Fani ziko nying kaka, kuna makampuni mengi yanahitaji damu changa kama yako katika utendaji kazi (sector ya banking, makampuni ya simu, mashirika mbalimbali).........achana na serikalini, after all huwezi kujifunza kazi ukiwa serikalini, watu wamekalia majungu na hawataki kuachia viti. Serikalini utaingia baada ya kupata uzoefu katika sector binafsi au mashirika mengine.....

Hayo ni maoni yangu kwako

Jamaa anataka jinsi ya kusavaivu mwezi huu wa 12, sasa akiacha kazi mwezi atakuwa hajasovu hayo mambo aliyoyaainisha, hilo la kuacha kazi nadhani lije baadae baada ya kumaliza matatizo yake ya mwezi huu.

Mimi nakushauri uombe mkopo wa sikukuu ya xmass kama hapo kwenu mna utamaduni wa kupewa mikopo vipindi vya sikukuu. Then angalia priority ya hiyo michango yako. Hiyo ya harusi siyo uchangie kiasi chote, unaweza wapa book tano tano, kwani si lazima uende ukaudhurie.

All the best!
 
1) tema harusi zote
2)mwombe mwenye nyumba akukope elfu tano au kumi mwambie umepata matatizo utamrudishia tu, automatically wazo la mchango toka kwako litakufa!
3)kesho asubuhi kumbuka kubeba kadi yako ya CHADEMA, wakati unaenda kunywa chai hakikisha unaiacha mezani, unakua ka umeisahau flani hivi, hakikisha unatumia kila njia hadi bosi wako aione na ajue kuwa ni yako--automatically atakuwa keshakufuta katika hesabu za wataotoa mchango
Hii mbinu nzuri sana.......hasa hiyo ya kuipiga chini michango ya ccm, nimeipenda!!!
Jamaa anataka jinsi ya kusavaivu mwezi huu wa 12, sasa akiacha kazi mwezi atakuwa hajasovu hayo mambo aliyoyaainisha, hilo la kuacha kazi nadhani lije baadae baada ya kumaliza matatizo yake ya mwezi huu.

Mimi nakushauri uombe mkopo wa sikukuu ya xmass kama hapo kwenu mna utamaduni wa kupewa mikopo vipindi vya sikukuu. Then angalia priority ya hiyo michango yako. Hiyo ya harusi siyo uchangie kiasi chote, unaweza wapa book tano tano, kwani si lazima uende ukaudhurie.

All the best!
Asante sana Ejogo........
 
jamani naombeni japo mnipe ka elimu kidogo kuhusiana na bajeti ili niweze kusavaivu katika sikukuu hizi zijazo za mwezi wa desemba. Kamshahara kenyewe ni tgs.d na kabla ya tarehe 20 desemba kuna mambo yafuatayo natakiwa nikamilishe.
1. Kuna kadi sita za harusi.............kiwango kwa kuwa nipo single kila moja elfu 20.
2. Kuna kadi ya mchango wa birthday ya mtoto wa mwenye nyumba mwisho tarehe 10 desemba.
3. Kuna fomu ya mchango wa ujenzi wa ofisi ya ccm............hii nimepewa na bosi wangu, inabidi nichangie ili kuongeza imani mbele ya bosi, nisije nikakosa safari za kiofisi.
4. Kadi mbili za send-off.
Hapo ili kukamilisha hayo mambo yote hapo kamshahara kote kameisha.............wenye uzoefu huwa mnasavaivu vipi katika hali kama hii??

usiige kunya kwa tembo utapasuka msamba mshahara kazi yake siyo kufadhili vitu ambavyo havina vipa umbele, hiyo michango yote ni kifisadi tu think twice hiyo siyo status yako.
 
Si ujifanye mgonjwa halafu uombe likizo uende zako kijijini!! ila kama hujaoa waweza rudi na ka binti ka darasa la saba huko!!!!! wakikukabidhi hako kalete kwangu kawe HG
 
Watumishi wote serikalini wezi,wanaishi kwa rushwa,visafari vya uongo na kweli,tender hewa,allowance za kazi hewa za masaa 1 inaandikwa 4

Umesahau kuna allowance za kongamano, semina, warsha na workshop!
 
Duh! Mchango wa birthday upotezee. Nenda kwa bosi wako kwa lengo la kuomba ushauri kama ulivyokuja hapa, mwambie kama vipi akukopeshe.
Kama hiyo haifai tafuta ugonjwa ulazwe hospital. Watu watakuwa wanakuletea hela za pole. Make sure hautok hosp hadi harusi, birthday na huo mchango wa sisim ushapita.
duh wewe mjanja sana , ndo mana kwny thread yako ya mtoto chatala umekataa nisikuzalishe mnyarwanda
 
Duh! Mchango wa birthday upotezee. Nenda kwa bosi wako kwa lengo la kuomba ushauri kama ulivyokuja hapa, mwambie kama vipi akukopeshe.
Kama hiyo haifai tafuta ugonjwa ulazwe hospital. Watu watakuwa wanakuletea hela za pole. Make sure hautok hosp hadi harusi, birthday na huo mchango wa sisim ushapita.
mmmh,jamani idea nyengine zinachekesha,ulazwe hospitali ku avoid michango mmmh
 
Duh! Mchango wa birthday upotezee. Nenda kwa bosi wako kwa lengo la kuomba ushauri kama ulivyokuja hapa, mwambie kama vipi akukopeshe.
Kama hiyo haifai tafuta ugonjwa ulazwe hospital. Watu watakuwa wanakuletea hela za pole. Make sure hautok hosp hadi harusi, birthday na huo mchango wa sisim ushapita.

tena azuge hawezi hata kuongea akiwa hospitalini
 
oppps kijasho chembamba kimenitoka
Hiyo michango mingine cancel bana hakuna anyejua unaishije sana sana awatakupa presha tu ya maisha
Hiyo ya jengo la CCM piga chini serikali ina hela zetu watoe huko
PAYE kubwa namna hii hela inaenda wapi.
Hiyo ya Birthday achana nayo mwenye nyumba anunue biscuit na soda aite watoto wafurahi pamoja
 
si ujifanye mgonjwa halafu uombe likizo uende zako kijijini!! Ila kama hujaoa waweza rudi na ka binti ka darasa la saba huko!!!!! Wakikukabidhi hako kalete kwangu kawe hg
una mataaizo sana ndugu yangu, hapo hujamshauri, bora mimi niyekaa kimyaa
 
Si ujifanye mgonjwa halafu uombe likizo uende zako kijijini!! ila kama hujaoa waweza rudi na ka binti ka darasa la saba huko!!!!! wakikukabidhi hako kalete kwangu kawe HG
Ahahahahaaaaaah huu ushauri mwingine bwana!!!
 
Umesahau moja, mchango kwa ajili ya kuiendeleza jf. Kazi ipo mkuu Mchango wa mwenye nyumba piga chini, kuhusu sisiemu no koment, harusi hizi siku kawaida harusi si lazima manake mambo ni mengi, send off ni kama nilivyoeleza kwa harusi!
Huu wa kuiendeleza JF upo kwenye bajeti.......tatizo ni hii ya harusi, birthday, send-off na huo wa kuwachangia CCM.
 
Duh! Mchango wa birthday upotezee. Nenda kwa bosi wako kwa lengo la kuomba ushauri kama ulivyokuja hapa, mwambie kama vipi akukopeshe.
Kama hiyo haifai tafuta ugonjwa ulazwe hospital. Watu watakuwa wanakuletea hela za pole. Make sure hautok hosp hadi harusi, birthday na huo mchango wa sisim ushapita.


Ama kweli, ushauri wa bure
 
Uko safi wewe nenda kanisani katoe fungu la 10 uondoke zako na usilete tena hii mada hapa
 
Katavi,

Hujui cha kufanya? Wenzio akina Rostam wanaiba ati...! Na wewe iba kama wao...!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom