Jamani hii CAPITAL TV mbona mimi sioni kama ina vipindi vya maana sana..

Mrimi

JF-Expert Member
Jul 18, 2011
1,691
633
Binafsi mimi ni mpenzi mkubwa wa TV zilizo chini ya IPP.Lakini pamoja na hivyo,hii Capital TV kiukweli(kwa mtazamo wangu) sijaona kama imejipanga kukidhi matarajio ya watazamaji wake.

Binafsi nilitarajia iwe TV maalum yenye vipindi vya kuonesha:
- Documentaries motomoto
- International News and Events mbali mbali,polical,sciantific,na matukio yenye kuvuta hisia za watazamaji
- Sports-Live event,news updates.
- Entertainments mbalimbali kama Movies kali,music za uhakika nk.

Lakini hii imekuwa tafauti kabisa na matarajia yangu.Sifurahishwi na kuoneshwa marudio ya mechi ya finali za kombe la dunia 1998 mpaka leo,tena mechi moja tu.Au marudio ya ligi ya South America ya miaka ya 90.Siamini kama IPP wanashindwa kurusha hata mechi moja ya Serie A kwa wiki.Basi wangekuwa hata wanatuonesha replay ya ligi mbali mbali angalau basi kwa wakati unaofaa.

Haiwezekani tukiingia youtube tunaangalia documentaries za uhakika,halafu kituo kikubwa cha TV kama hiki kiwe kinatuonesha documentary moja hiyo hiyo kila siku.Haiwezekani kuwa tunaoneshwa tv series za kikorea na philipines tu kila siku.Ukiangalia movies ndio kichekesho,movies za kizamani tuu,movie za hihindi ndio usiseme,movie moja inarudiwa rudiwa mpaka basi..

Siami kama wanashindwa kuwa na vipindi vingi vya midala kama ilivyo kwa CH.10(Jen.on Monday,Je Tutafika),StarTV(Jecho letu ndani ya habari) nk. nk. nk. Mimi ninaamini hii ni tv pekee ambayo ikiwekwa vizuri inaweza ikaleta mtazamo mpya miongoni mwa vituo vya TV hapa nchini.Binafsi siamini kama mnashindwa kufanya hivyo,bali hamna nia ya kutupatia kitu kipya.

Mpaka sasa sina hakika kama walishawahi kufanya utafiti wakajua TV hii inatazamwa na watazamaji wa wangapi,wa rika lipi au jinsia ipi.Kiukweli ktk hili,Capital TV mnahitaji kujitazama upya.
 
Binafsi mimi ni mpenzi mkubwa wa TV zilizo chini ya IPP.Lakini pamoja na hivyo,hii Capital TV kiukweli(kwa mtazamo wangu) sijaona kama imejipanga kukidhi matarajio ya watazamaji wake.

Binafsi nilitarajia iwe TV maalum yenye vipindi vya kuonesha:
- Documentaries motomoto
- International News and Events mbali mbali,polical,sciantific,na matukio yenye kuvuta hisia za watazamaji
- Sports-Live event,news updates.
- Entertainments mbalimbali kama Movies kali,music za uhakika nk.

Lakini hii imekuwa tafauti kabisa na matarajia yangu.Sifurahishwi na kuoneshwa marudio ya mechi ya finali za kombe la dunia 1998 mpaka leo,tena mechi moja tu.Au marudio ya ligi ya South America ya miaka ya 90.Siamini kama IPP wanashindwa kurusha hata mechi moja ya Serie A kwa wiki.Basi wangekuwa hata wanatuonesha replay ya ligi mbali mbali angalau basi kwa wakati unaofaa.

Haiwezekani tukiingia youtube tunaangalia documentaries za uhakika,halafu kituo kikubwa cha TV kama hiki kiwe kinatuonesha documentary moja hiyo hiyo kila siku.Haiwezekani kuwa tunaoneshwa tv series za kikorea na philipines tu kila siku.Ukiangalia movies ndio kichekesho,movies za kizamani tuu,movie za hihindi ndio usiseme,movie moja inarudiwa rudiwa mpaka basi..

Siami kama wanashindwa kuwa na vipindi vingi vya midala kama ilivyo kwa CH.10(Jen.on Monday,Je Tutafika),StarTV(Jecho letu ndani ya habari) nk. nk. nk. Mimi ninaamini hii ni tv pekee ambayo ikiwekwa vizuri inaweza ikaleta mtazamo mpya miongoni mwa vituo vya TV hapa nchini.Binafsi siamini kama mnashindwa kufanya hivyo,bali hamna nia ya kutupatia kitu kipya.

Mpaka sasa sina hakika kama walishawahi kufanya utafiti wakajua TV hii inatazamwa na watazamaji wa wangapi,wa rika lipi au jinsia ipi.Kiukweli ktk hili,Capital TV mnahitaji kujitazama upya.
Mimi nilikuwa naipenda kipindi kile inaanza ikiwa na Jina la "Pulse" Mapouka kwa kwenda mbele ila sasa Ptuuuu!!!
 
Dah yani hiyo channel ni special kwa kurudia vipindi vilivyopita kuna movie niliônaga enzi za pulse na bado wakazirudia kama mara kumi hivi. Nashangaa kwanini wanashindwa kuonyesha movies not latest but atleast the best 1,documentary za ukweli na vipindi vingine vya maana sio hivyi wanavyoonyesha sasa.
 
Dah yani hiyo channel ni special kwa kurudia vipindi vilivyopita kuna movie niliônaga enzi za pulse na bado wakazirudia kama mara kumi hivi. Nashangaa kwanini wanashindwa kuonyesha movies not latest but atleast the best 1,documentary za ukweli na vipindi vingine vya maana sio hivyi wanavyoonyesha sasa.

hawana jipya ha kaka!
 
Hakuna bidhaa inayokosa mnunuzi!

Sio kwa sababu wewe hupendi MUHOGO basi unajua na wengine wanauchukia! Fikiri kwanza kabla ya kuandika!
 
Kwa sababu TV Stations zipo nyingi wanakupunguzia tabu ya kuchagua uangalie TV Station ipi.
 
Hebu wana jf tuangalie jambo hili in a positive way: soko la vipindi vya televisheni hapa nchini ni kubwa na watanzani tumekalia kutengeneza komedi zisizo na kichwa wala miguu- jiulize video ya saa moja na nusu inaonyesha wanaume wakimshangaa dada mwenye ------ makubwa utaiuza kwenye kituo gani cha tv?
 
Hv kua unaonesha muvi kama ilivyo kwa hbo inahitaji uwe na licence ya kufanya ivyo? Assume capital wafanye hvyo... Wadau tupo weng,
 
Hakuna bidhaa inayokosa mnunuzi!

Sio kwa sababu wewe hupendi MUHOGO basi unajua na wengine wanauchukia! Fikiri kwanza kabla ya kuandika!

Mkuu umenichekesha sana..

Kwa hiyo ndio kusema ukioneshwa marudio ya mechi ya ligi ya south america ya mwaka 78,ukioneshwa toyota wildlife documentary moja miaka nenda rudi ndio wewe unaufurahia huo muhogo?!Kwako wewe ukiendelea kuoneshwa movie moja ya Mithun kila siku miaka yote,hakuna shida.Kwa hiyo hatuhitaji mabadiliko ya vipindi ili tupate kuona updated programs.

Anyway,mzee wa kufiria kwa hiyo kwako hakuna shida ikiwa tutaendelea kufanya jambo moja kwa namna moja hiyo hiyo miaka nenda rudi mradi tu wewe unaufurahia muhogo,siyo?

Yap.Wewe kweli ni great thinker.Bravo mkuu.
 
Dah yani hiyo channel ni special kwa kurudia vipindi vilivyopita kuna movie niliônaga enzi za pulse na bado wakazirudia kama mara kumi hivi. Nashangaa kwanini wanashindwa kuonyesha movies not latest but atleast the best 1,documentary za ukweli na vipindi vingine vya maana sio hivyi wanavyoonyesha sasa.

Jamaa nadhani ubunifu wao ndipo ulipofikia uko.Siamini kama kweli wanashindwa kutuonesha vipindi vyenye mvuto,ni basi tu hawana nia ya kufanya hivyo.Kiukweli sina hakika kama walishawahi kufanya utafiti ili kujua ni kwa kiasi gani hii TV inatazamwa.
 
Ungejua wenzio hawana time na madokyumentali sijui mpira wala usingeandika..Watazaji wengi ni watoto na wanawake na wanapendelea hayo maseries ya kikorea na mexico
 
Hv kua unaonesha muvi kama ilivyo kwa hbo inahitaji uwe na licence ya kufanya ivyo? Assume capital wafanye hvyo... Wadau tupo weng,

Wadau tupo wengi sana mkuu.Kama ITV inaweza kuonesha 24 na Prison Break wanashindwaje kuonesha Game of Thrones,Legend of The Seaker au Merlin.

Au kama wanaweza kuonesha classic movies,wanashindwaje kuonesha movies nzuri japo za miaka miwili iliyopita?Lakini pia mbona wakati walipoanza walikuwa wanaonesha movies tena kali tu?

Kama wanaweza kutuonesha mechi zilizochezwa miaka 20 iliyopita wanashindwa nini kutuonesha hata replay ya games nzuri za hivi karibuni?

Kama wanaweza kuonesha documentaries za uongo na kweli kupitia DW,wanashindwa nini kuonesha documentaries kupitia Discovery au NatGeo channels au NASA?

Kama wanaweza kuonesha Week Agenda,wanashindwa nini kuanda vipindi vya mijadala na uchambuzi wa mambo mbalimbali hata ya ndani ya nchi?

Yapo mengi sana ya kusema.
 
Ungejua wenzio hawana time na madokyumentali sijui mpira wala usingeandika..Watazaji wengi ni watoto na wanawake na wanapendelea hayo maseries ya kikorea na mexico

Inaweza kuwa kweli mkuu,ila hata kama ni series basi zingekuwa ktk varieties tofauti tofauti.Lakini pia siamini kama watazamaji wake wengi ni watoto na akina mama,maana hata hizo series zao ninaoneshwa kuanzia saa moja jioni na saa tano usiku.Je,mchana wanatazama akina nani?

Mimi nadhani,jamaa wanatakiwa kujua mahitaji ya watazamaji wao.Mbona kwenye EATV wametambua watazamaji wao wengi ni vijana na wamejipanga vizuri kutoa huduma stahiki.Sasa hii Capital wanawalenga watazamaji gani,na wanajuaje kama wanawaridhisha watazamaji wao?
 
Mkuu umenichekesha sana..

Kwa hiyo ndio kusema ukioneshwa marudio ya mechi ya ligi ya south america ya mwaka 78,ukioneshwa toyota wildlife documentary moja miaka nenda rudi ndio wewe unaufurahia huo muhogo?!Kwako wewe ukiendelea kuoneshwa movie moja ya Mithun kila siku miaka yote,hakuna shida.Kwa hiyo hatuhitaji mabadiliko ya vipindi ili tupate kuona updated programs.

Anyway,mzee wa kufiria kwa hiyo kwako hakuna shida ikiwa tutaendelea kufanya jambo moja kwa namna moja hiyo hiyo miaka nenda rudi mradi tu wewe unaufurahia muhogo,siyo?

Yap.Wewe kweli ni great thinker.Bravo mkuu.

Huu hapa chini ni mtazamo wako
hii Capital TV kiukweli(kwa mtazamo wangu) sijaona kama imejipanga kukidhi matarajio ya watazamaji wake.

Hapa chini ukaendelea..
Lakini hii imekuwa tafauti kabisa na matarajia yangu

Jibu langu la msingi kwako limejikita kwenye hizo hoja zako mkuu!

Televisheni yoyote ina target audience yake. Target audience ya Clouds TV haiwezi kamwe kufanana na Capital TV; na ndio maana wao waliamua kuanzisha Capital TV kwakua waliona kuna soko lao ambalo ni tofauti na wewe mkuu.
Bila shaka kuna watazamaji wengine wa Capital TV wanachukia vipindi vya CLOUDS TV kama ulivyo wewe kwa Capital.

Kurudia rudia mpira ambao naona ndio kero kubwa kwako au movies labda ni maombi ya watazamaji wao ambao wengi bila shaka ni Foreigners, Diplomats na wale wanaotema yai.

TV ziko nyingi mkuu, chagua hata SIBUKA kama nyingine zinakuboa. Ni vigumu TV moja kuwafurahisha watu wote kwa muda wote mkuu!

Ahsante
 
Capital ndo tv pekee bongo inayojitahd kuonesha documentaries, korean dramas na indian movies [hatukatai] but kula mihogo mchana na jion 24/7 kunaboa sana, muv za miaka kumi na tano ilopita?
 
vingamuzi vimeleta shida...chanel nyingi hazionekani.....tumerudi nyuma sana baada ya vingamuzi
 
vingamuzi vimeleta shida...chanel nyingi hazionekani.....tumerudi nyuma sana baada ya vingamuzi. Afu tena kila TV inataka iwe na kingamuzi chake..!!! tutafika kweli....hivi juzijuzi Stattimes wanapitisha tangazo eti Star TV hawatakuwa wakionyeswa na kingamuzi chao!
 
vingamuzi vimeleta shida...chanel nyingi hazionekani.....tumerudi nyuma sana baada ya vingamuzi. Afu tena kila TV inataka iwe na kingamuzi chake..!!! tutafika kweli....hivi juzijuzi Stattimes wanapitisha tangazo eti Star TV hawatakuwa wakionyeswa na kingamuzi chao! Sisi sijui Star tv watakuwa wapi...kuna chanel zilikuwa zinaonekana kabla ya vingammuzi lakini sasa wapiii!
 
vingamuzi vimeleta shida...chanel nyingi hazionekani.....tumerudi nyuma sana baada ya vingamuzi. Afu tena kila TV inataka iwe na kingamuzi chake..!!! tutafika kweli....hivi juzijuzi Stattimes wanapitisha tangazo eti Star TV hawatakuwa wakionyeswa na kingamuzi chao! Sisi sijui Star tv watakuwa wapi...kuna chanel zilikuwa zinaonekana kabla ya vingammuzi lakini sasa wapiii!

Mkuu nao wana king'amuzi chao kinaitwa Continental,mpaka sasa wanapatikana katika miji mitatu(DSM,Mwanza na Dododoma).Ila mpaka sasa bado wanapatikana free kwa wenye madishi;pia wanapatikana ktk DSTV kwa kulipia.TBC ndio wamesinzia kwenye madishi sasa ni wiki ya tatu wengi wetu hatuwapati.
 
Capital ndo tv pekee bongo inayojitahd kuonesha documentaries, korean dramas na indian movies [hatukatai] but kula mihogo mchana na jion 24/7 kunaboa sana, muv za miaka kumi na tano ilopita?

Msamehe bure tu mkuu.
Hajui alisemalo.
 
Back
Top Bottom